Categories
Ulaji mzuri na Afya ya Tumbo

Njia 7 za kulainisha choo

Kukosa choo na choo kigumu ni moja ya matatizo makubwa zaidi hapa kwetu. Kwani kila siku zaidi ya wagonjwa watano hunitafuta kwa shida hii. Pamoja na kwamba kuna dawa nyingi za kulainisha choo unazoweza kuzipata pharmacy, bado utakuwa hujasolve chanzo cha tatizo. Utaendelea kukosa choo na kupata choo kigumu baada tu ya kumaliza dawa zako.

Tiba na njia asli za kurekebisha mfumo wako wa chakula ndio suluhisho la kudumu. Njia hizi asili zinajumuisha vajula, mimea tiba na hata vitu unavyokunywa.

Mfumo wa ulaji ni tatizo

Dunia ya sasa imebadili mfumo wa ulaji na kutamnguliza biashara zaidi. makampuni makubwa ya kutengeneza vyakula yanashindana kupata faida na kufanya mauzo zaidi ya vyakula vyao, bila kuzingatia afya ya mlaji.

Miili yetu imeumbwa kwa namna ya kipekee sana ya kusafisha sumu, tunachotakiwa tu kuupa mwili malighafi stahiki na maji salama ili mtambo ufanye kazi. Muhimu sasa ujue kwanza chanzo cha tatizo lako kabla hujaanza kujitibia. Tuendelee..

Nini kinapelekea ukose choo na kupata choo kigumu?

Sababu hizi ndio chanzo cha tatizo lako

  • kula vyakula vya kusindikwa kiwandani visvyo na kambakamba
  • msongo wa mawazo
  • kukosa usingizi wa kutosha na
  • kutokunywa maji ya kutosha
  • kutoshugulisha mwili-mazoezi

Je Unatakiwa Kunya Mara ngapi kwa siku/wiki?

Wataalamu wengi wanapendekeza kwamba ni muhimu kwenda haja kubwa walau mara tatu au zaidi kwa wiki. Japo hili linatofautiana sana kwa kila mtu, kulingana na aina ya kazi anazofanya, chakula anachokula na hata mazingira aliyopo mtu huyu.

Kiujumla kama huendi kunya walau mara 3 kwa wiki, unatakiwa kufanya mabadiliko kwenye lishe yako na kutibu tatizo. Endelea kusoma kujua njia 10 zilizothibitishwa kukutibu choo kigumu.

Njia 7 za kulainisha choo na kukufanya upate choo kila siku

1.Kambakamba/fibers zinasaidia kulainisha choo

Hii ni hatua ya kwanza kabisa kwenye kurekebisha mfumo wako wa chakula. Anza kwa kuongeza vyakula vyenye kambakamba kwenye mlo wako kila siku. Na hakikisha unapata kambakamba hizi kutoka kwenye vyakula asili(ambavyo havijakobolewa na kusindikwa)

Matunda na mboga zenye kambakamba kwa wingi ni pamoja na

  • maparachichi
  • zabibu
  • bamia
  • spinach na

2.Kunywa maji ya kutosha

Kumbuka viungo vyako kama ini na figo vinahitaji maji mengi ili kusafisha damu, kuzalisha mkojo na kutoa taka mwilini.
Kama hutumii maji mengi, anza kubadili sasa ratiba yako, kunywa maji kila unapopata kiu, usinywe soda au pombe.

3.Tumia zaidi Vyakula vinavyoongeza bakteria wazuri tumboni

Kwenye tumbo kuna uwiano wa bakteria wazuri na wabaya. Endapo bakteria wabaya wataongezeka kupita kiasi, mazingira ya uchakataji chakula yatavurugika. Hapo taanza kupata dalili mbaya kama kukosa choo na choo kigumu, tumbo kujaa gesi na chakula kutosagwa vizuri.

Kuimarisha uwiano huo hakikisha unakula zaidi vyakula kama maziwa mtindi, chiaseed na flaxseed. Hakikisha tu unaoponunua maziwa, nunua yale asili. Achana na maziwa ya pakiti siyo salama kwako.

4.Aloe vera

Ukiniambia ni mmea gani utalainisha choo kwa haraka zaidi, nitakwambia ni Alo vera. Ni mmea unaotumika tangu miaka ya kale. Aloe vera pia inasaidia kupambana na vimelea wabaya, gesi tumboni na kuharakisha usagaji wa chakula.

Kwavile mmea wa aloe vera ni mchungu sana hakikisha unapata vidonge, ama juisi yake kutoka kwenye chanzo cha kuaminika. Unaweza pia kufika ofsini kwetu tukakupa vidonge vya aloevera.

5.Chia Seeds

chakula cha kulainisha choo

Moja ya faida ya chia seeds ni uwezo wake wa kufyonza maji kwenye mfumo wa chakula, na hivo kukuletea choo kilaini.

Chia seed zinatoa gram 10 za kambakamba kwa ujazo wa kijiko kimoja cha chakula. Muunganiko wake na majimaji unatengeneza jelly inafofanya choo kisukumwe kwa uzuri sana bila kutumia nguvu. Hakikisha unatumia vijiko vi3 kwa siku.
Matumizi: zioshe mbegu zako vizuri kisha ziloweke kwenye maji kwa nusu saa(vijiko viwili kwa ujazo wa kikombe kimoja cha chai). Tengeneza juis yako au salad, kisha weka chia seeds na blend pamoja.

6.Mboga za majani za kijani

Ukiacha kambakamba, mboga zilizokolea ukijani zina madini mengi ya magnesium. Magnesium ni madini muhimu kwenye kulainisha choo chako. Pasipo magnesium, ni ngumu kwa choo kusafiri kwenye mfumo wako.

7.Tui la nazi

Tui la nazi pamoja na maji ya madafu ni mazuri sana kwako wewe mwenye shida ya choo. Pamoja na utamu wake kutokana na sukari yake asili, maji haya yanalainisha choo kwasbaabu ya uwepo wa madini ya potasium ndani yake. Anza sasa kunywa maji ya mdafu na tui la nazi. Unaweza kuongeza viungo kama tangawizi, kisha ukachemsha kidogo tui pamoja na machicha kwa dakika 5 kabla ya kuchuja na kunywa.

Maelezo ya mwisho

Dawa za hospital za kulainisha choo siyo tiba kwako, ni suluhisho la mda mfupi tu, kisha unarudi kule kule. dawa hizi ukitumia mda mrefu zitavuruga mazingira ya tumbo na tatizo kuwa kubwa zaidi.

Baadhi ya vyakula na mimea tiba zitakusaidia kurekebisha mfumo wa ko wa chakula, bila dawa za pharmacy. Na njia hizi ni salama na zinapatikana sokoni tu.

Kurekebisha mfumo wa chakula siyo jambo la siku moja. inataka kujiwekea malengo ya mda mrefu na kufatilia kila siku. Ukishajijengea tabia ya kula vyakula asili usiache endelea nayo siku zote, hapo hautapata tena shida ya choo.

Muhimu kwa mgonjwa wa Choo kigumu

Wagonjwa wenye tatizo la mda mrefu zaidi ya wiki mbili tunawashauri kutumia tiba hizi asili kutibu tatizo haraka. Kwasababu usipopata tiba, itapelekea uugue magonjwa mengine mabaya kama bawasili.

Dozi moja tu inatosha kukupa matokeo mazuri ndani ya siku 3. Dawa ni Tsh 50,000/=

Tuandikie kwa Whatsapp number 0678626254 uanze dozi kwa Tsh 50,000/= tu.