Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Tendo la ndoa Uncategorized

Nini kinatokea baada ya kupoteza bikira yako?

kupoteza bikira

Bikira ni kitu gani??

Tafsiri iliyozoeleka ya bikira ni mwanamke ambaye hajawahi kabisa kufanya tendo la ndoa katika maisha yake. Kwahivo mwanamke anapoingiliwa ukeni kwa mara ya kwanza anapoteza ile bikira yake.

Nini kinatokea mwilini baada ya kupoteza bikira?

Tendo la ngono laweza kupelekea mabadiliko mengi ya mwili. Hapa chini ni maelezo ya kinatokea

1.Mabadiliko ya ukeni

Watu wengi huamini kwamba tendo la ndoa linafanya uke kutanuka na kuwa mkubwa ama kulegea. Kumbuka uke unaweza kutanuka na kuzaa mtoto na kisha ukarudia hali yake ya mwanzo. Uume ni mdogo sana ukilinganisha na mtoto na hauwezi kufanya uke kulegea.

Kwa baadhi ya wanawake wanapoanza tendo hawapati raha, hasa kama uke wako ni mkavu naa hukuandaliwa vizuri. Hakikisha unafanya michezo mingine ya kutomasana kwa mda mrefu kabla ya kuanza tendo lenyewe.

2.Matiti

Kwa baadhi ya watu kufanya tendo kunaweza kupelekea matitti na chuchu kuvimba. Hii inatokea kwasababu zile hisia na muhemko wa kutaka kufanya tendo inapelekea mzunguko wa kasi wa damu kuelekea kwenye matiti, uke na uume pia.

3.Mabadiliko ya homoni

Wakati wa tendo ubongo unatoa vichocheo vingi sana kuelekea kwenye damu.Kazi ya vichocheo hivi ni kukufanya ujiskie raha ya tendo lenyewe na kuongeza upendo kati yako na mpenzi wako.

Je unaweza kushika mimba siku ya kwanza kufanya tendo?

Jibu ni ndio, unaweza kushika mimba siku ile tu ya kwanza kukutana na mwanaume. Mbegu tu zikiingia ndani ya uke unaweza kushika mimba. Kama hutaki kushika mimba mapema basi hakikisha unatumia condom muda wote wa tendo ama waweza kumeza p2.

Je ni umri gani sahihi wa wanawake wengi kupoteza bikira?

Wastani wa umri wa kupoteza bikira kwa wanawake wengi ni kati ya miaka 16 na 17. Katika umri wowote ule, kufanya tendo kwa mara ya kwanza ni jambo la tofauti sana na hisia zake zinatofautiana. Siyo kila mtu hufurahi tendo siku ya kwanza, wengi hupata maumivu na kuhisi kujuta. Na wengine hupata mawazo sana na hofu pengine wameshapata mimba au magonjwa ya zinaa

Jinsi ya kufanya tendo na kupoteza bikira bila maumivu

Hakuna njia moja ya kuondoa maumivu asilimia 100 siku ya kwanza unapofanya tendo, ila kuna vitu vichache vya kufanya kupunguza maumivu. Ukiwa na mpenzi asiye na haraka ya kuingiza uume, na pia awe mwelewa itakusaidia sana kufurahia tendo na kupunguza maimivu siku ya kwanza. Kuna mambo mengine mengi waweza kufanya yakakusaidia, endelea kuyasoma hapa chini

1.Ongea na mpenzi wako kabla ya tendo

Usiogope kuongea na mtu wako namna unavojiskia, vitu unavyoogopa na usichokipenda. Una kila haki ya kujieleza kwa uwazi ili akuvumilie. Kuongea na mwenzio kunasaidia kupunguza ile hofu ulokuwa nayo kuhusu kufanya mapenzi.

2.Fanya maandalizi ya kutosha

Hakika uke unaloa vizuri na kuwa mlaini sana kabla ya kuingiliwa na mwenzako hii inapunguza sana maumivu. Maandalizi haya ni pamoja na michezo kadhaa mkiwa uchi, kushikana sehemu za siri, kunyonyana uke na uume, na ndimi na kuambiana maneno matamu.

Chukueni walau nusu saa mpaka lisaa la maandalizi kabla ya tendo, msiende haraka.

3.Jaribu mikao na style tofauti za kufanya tendo

Kama unapata maumivu kwenye aina moja ya style ya kufanya tendo jaribu kubadili na utumie style zingine. Hizi ni baadhi ya style za kufanya tendo.

Style ya kwanza:Tumia mto chini ya mgongo na kukufanya ubinuke kidogo. Kunja magoti kisha chanua miguu yako ili uke ubaki wazi.

Style ya pili:Mwanamke kushika ukuta, na kubinuka kidogo kisha mwanamume anakunja kwa nyuma na kumuingilia ukeni

Style ya kifo cha mende: Hii ni nzuri kwa kuanzia, karibu kila mwanafunzi wa mapenzi anaanzia hapa: ukizoea hii style ya mwanamke kulala chini na mwanaume kuja kwa juu ndipo uanze kujaribu style zingine

4.Usijiwekee malengo makubwa kivile

Kutokana na kukua kwa teknoligia, lazima utakuwa umeshatazama picha na video za ngono namna watu wanavoingiza kwenye movie chafu za ngono. Na kwenye akili yako umeweka matazamio flani, kwamba unachokiona ndicho kitatokea utakapioanza mapenzi. Hii siyo kweli, wanaoigiza na kurekodi vidoe za ngono wanatumia madawa kuamsha hisia zao na ni wazoefu sana kufanya tendo.

Usijilinganishe nao, kuwa mpole na jipe muda, huwezi kuwa mzoefu kwa siku moja. Siku ya kwanza unaweza kushindwa kabisa kufanya tendo na baadae ukaweza. Hivo tuliza mihemko na ufanye taratibu

5.Hakikisha Eneo la kufanya tendo ni tulivu

Siku yako ya kwanza kufanya tendo inatakiwa kufanyika mahali pazuri pasio na kelele wala vitu hatari.Yatakiwa iwe sehemu ambapo wote wawili mke na mme mnatulia kiakili. Siyo kwenu vichaka au kwenye gari.

Kitanda ni sehemu nzuri zaidi ya kufanya tendo siku ya kwanza. Fanya usafi kwenye chumba chako na kuondoa kelele zozote. Hakikisha hakuna watu wengi eneo hilo na uzime simu. Unaweza kufungulia redio kwa mbali ili upate mziki wa kukusindikiza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *