Dalili za Mimba Changa

Je unajisi kwamba una dalili za mimba changa na huna uhakika? Njia pekee ya uhakika ni kufanya kipimo ndipo utajua mbivu na mbichi. Kabla ya kupima kuna dalili za awali ambazo waweza kuzitumia kukupa mwanga kwamba tayari una ujauzito.

kipimo cha mimba-Dalili za mimba changa
kipimo cha mimba

Je Kila Mwanamke anaweza Kupata dalili za mimba mapema?

Kila mwanamke anatofautiana na mwingine kimaumbile. Kuna wengine hawapati dalili kabisa hata mimba ifike miezi mitano. Lakini kuna wanawake wengine huona dalili mapema sana mimba ya miezi mwili tu.

Usichanganye hedhi na mimba

Wanawake wengi hushindwa kugundua mapema kama wana mimba kwasababu dalili nyingi za mimba hufanana na zile za kwenye hedhi mfano kizunguzungu na uchovu.

Dalili zifuatazo zitakupa mwanga iwapo tayari mimba imeingia, japo watakiwa kufahamu kwamba dalili hizi pia zaweza kuwa matokeo ya swala lingine la kiafya. Vipimo ni muhimu kufanyika ili kuwa na uhakika zaidi.

Na kumbuka muda mzuri wa kupima mimba kwa mkojo, ni wiki moja baada ya kuvusha hedhi. Endapo hedhi umpitiliza, ndipo subiri wiki ukapime UPT, utapata majibu sahihi zaidi.

Dalili za Mimba Changa ni hizi

1.Kupata matone ya Damu nyepesi

Baada ya mimba kutungwa yai lililorutubishwa hujishikiza kwenye ukuta wa kizazi. Kitendo hichi kinaweza kupelekea kutokwa na matone mepesi ya damu ukeni na maumivu kwa mbali ya nyonga. Damu hii huitwa implantation bleeding, inatokea siku 6 mpaka 12 baada ya mimba kutungwa.

2.Maumivu kwa mbali ya Nyonga

Maumivu ya nyonga kutokana na mimba changa yanaweza kufanana na yale hedhi. Wanawake huchanganya hilo na kudhani ni hedhi inaanza. Pamoja na kupata bleed nyepesi mwanamke anaweza kuona uchafu mweupe kama maziwa ukeni. Hiki ni kiashiria cha kuanza kuongezeka kwa ukuta wa kizazi ili kushikilia vyema kiumbe kilichotungwa.

Kumbuka uchafu waweza kuendelea kutoka wakati wote wa ujauzito hilo lisikupe mashaka. Lakini kama uchafu utakuwa na harufu mbaya, unaleta muwasho na kujikuna hapo unahitaji kuonana na daktari mapema iwezekanavyo. Kwani waweza kuwa na fangas au maambukizi ya bakteria ukeni.

3.Kubadilika Kwa Matiti

Mabadiliko ya matiti ni moja ya kiashiria kwamba tayari una ujauzito. Kutokanana mabadiliko ya homoni , matiti yanaweza kukua na kujaa week moja baada ya kushika mimba. Matiti pia yanaweza kuwa mazito kuliko kawaida na eneo la chuchu kuwa na weusi zaidi.

Ukiona dalili hizi usiwe na hofu, tambua tu kwamba matiti yataendelea kukua ili kujiandaa kunyonyesha.

4.Uchovu na Kuishiwa Nguvu

Moja ya dalili kubwa ya mimba changa ni kuhisi kuchoka na kusinzia ovyo. Mwanamke huanza kupata dalili hizi wiki moja baada ya kushika ujauzito. Kwanini hali hii itokee? ni kwa sababu ya kuongezeka kwa homoni ya progesterone.

Ukipata dalili hii hakikisha unapata muda mwingi wa kupumzika. Kula zaidi vyakula vya protini na madini chuma.

5.Kichefuchefu(morning sickness)

Kisababishi kikubwa cha kichefuchefu kwa mimba changa haijulikani lakini mabadiliko ya homoni wakati wa ujauzito inaweza kuchangia. Kichefuchefu yaweza kukupata muda wowote, na kuhisi kutapika, japo kwa wengi hutokea zaidi asubuhi.

Baadhi ya wanawake hushindwa kula baadhi ya vyakula baada ya kupata mimba. Hali hii huchangiwa zaidi na mabadiliko ya homoni. Inawezekana kabisa hali hizi za kuchagua chakula, kichefuchefu ikamuandama mwanamke katika siku zote za ujauzito mpaka pale atakapojifungua.

Hakikisha unakula lishe nzuri kila siku ili kumpa mtoto virutubisho vyote vinavyohitajika.

Kukosa Hedhi ni Dalili ya Mimba Changa

Dalili kubwa iliyo wazi ya kwamba tayari una ujauzito ni kupitisha hedhi. Japo siyo kila ukikosa hedhi ni mimba changa hapana. Unaweza kukosa hedhi kutokana na mabadiliko ya homoni, kuongezeka uzito ama kupungua kupita kiasi, mwili kuchoka sana, matumizi ya vidonge vya kuzuia mimba .

Ukikosa hedhi zaidi ya week mbili ulizozoea, basi hakikisha unanunua kipimo na kupima mkojo kujua kama mimba ipo.

Dalili zingine ya Kuonesha una Mimba Changa

Kukojoa mara kwa mara: Kwa wanawake wengi hali hii huanza baada ya week 6 mpaka 8 ukishika mimba. Lakini kumbuka dalili hii yaweza pia kusababishwa na UTI na kisukari, muhimu kupima.

Kukosa choo ama kupata choo kigumu: kutokana na mabadiliko ya homoni, chakula hupunguza kasi ya kupita kwenye utumbo mdogo. Kupunguza tatizo hakikisha unakunywa maji ya kutosha, fanya mazoezi na kula vyakula visivyokobolewa na vya kambakamba kwa wingi.

Kubadilika kwa mood yako; hasa katka miezi mitatu ya mwanzo

Maumivu ya kichwa na mgongo,inatokea zaidi kwa wanawake wengi wenye ujauzito

Fahamu kwamba mwanamke mjamzito anaweza kuwa na dalili zote hizi ama akawa na dalili baadhi. Kama moja ya dalili hizi itakuboa na kukufanya ujisikie vibaya, ongea na daktari wako atakupa ushauri vizuri.

Bofya kusoma kuhusu: Njia salama ya kusafisha kizazi baada ya kutoa mimba

58 replies on “Dalili za Mimba Changa”

Je kuvimba ndani ya uke na kuhisi maumivu makali wakati wakukojoa hiyo ni dalili ya ugonjwa gani?

Sasa kwa mwanamke aliye lala na mwanaume kwa siku zakumaliza hedhi yake yani siku ya kwanza na kuendeleya mbaka siku ya kumi mwanamke anaweza kuchukuwa mimba??

Ugonjwa gan mbaya uki mkuta mwana mke mwenye mimba ni hatar kwa afya yake na mtoto

je ukiona dam inatoka ukeni na uke kuwa mkavu hivi na ute kuwa kam yai na nyonga kuuma ni dalili ya mimba

Najisikia mate kujaa mdomoni na hezi yangu inatoka nyepesi na ni nyeusi maumivu ya kichwa inaweza ikawa ni nn

Nina mwezi sasa sijaona hedhi natumekua tukitumia withdrawal baada ya kutoa family shida inaezakua gani

Toka mwezi huu uanze nikiamka asubuhi tumbo linakuwa zito, nahisi njaa kila muda na nahisi kiungulia kila muda je ni dalili ya mimba?

Mke wang wakat wa buridi huziona daliliza mimba changa ila bada ya wik mbili analudi hali ya kawaida hili ni tatizo gan?

nimeshiriki tendo LA ndoa kW mda was miezj mitatu na make wng akila chakula anatapika akiamka siku zengine anahisi amechoka tatizo inaeza kuwa nn

Nilishiriki tendo la ndoa tare 25 hadi28 nilikua bado sijaona hedhi. Date 29 nkaona nkama inakuja nkaenda kama kawa siku tatu” sai sion nkiwa sawa tumbo ina uma na kuguruma na kuumwa na mgongo apo chin, je shida ni?

Nilishiriki ndoa wakati wa henzi tarehe 25 mbaka ikaisha date 27 na siku ya 28 bado tulishiriki na mpenzi wangu na sasa ni mwezi mwingine na nimepitisha siku ya tarehe ya period 27 na chuchu na uvivu pia ute unaokaa maziwa unatoka. Hii ni dalili ya kuwa nizapata mimba ama ni nini?

Me kila mdaa njaa inauma alaf kiuno kinauma sana na kichw kinaum sana chn ya kitov tumbo linauma ni wiki sas na mwili unaishiw nguv nime pima mimb sina ivi itakuw nn

nina miezi 3 sasa sija pata hedhi na sihisi dariri zozote zile za mimba je? nini taizo.

mimi nahisi mgongo inauma tumbo chini ya kitovu nahisi maumivu naishiwa na nguvu nahisi njaa kila wakati na kusinzia je inaweza kua dalili ya mimba

Mke wangu kuumwa na tumbo ya chini,mgongo na kiuno, kuumwa na matiti,kichwa kuumwa na uchovu mwingi na kutokwa na matone ya damu ukeni. na alimaliza family planing juzi

Samahan naswali kipimo cha utrasound njia ya uzaz”ke” kina galama gan na kahama tawi lenu lipo?

mimi na nyonyesha mtoto sasa ana miez 10 kasoro ,mwezi wa kwanza niliona period 27 _31january,mwezi wa pili sijaona kabisa naeza nikawa mjamzito au

Ujambo docta..mi nnatokwa na kitu kama maziwa huku chini ya uzaz wangu alafu kitovu imetoka nje na nnaumwa chini ya 2mbo na kiuno na nkiamka asubui naskia2 mdomo nkal alf 2mbo ni ngumu na inashnda ikinguruma shda inaweza kuwa nn?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *