Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Makovu kwenye kizazi

makovu kwenye kizazi
kizazi

Makovu kwenye kizazi kitaalamu Asherman’s syndrome ni tatizo analopata mwanamke ukubwani kwenye mfuko wa uzazi. Tishu hizi za makovu huanza kujitengeneza na kukua kupita kaisi mpaka kupunguza ile nafasi ya ndani ya kizazi kuwa kidogo kuliko kawaida.

Hali hii yaweza kuleta maimivu sana ya nyonga na tumbo, hedhi nyepesi sana na kushindwa kushika mimba.

Nani anaweza kupata makovu kwenye kizazi?

Muhimu ifahamike kwanza ugonjwa huu siyo wa kurithi, unaupata kulingana na changamoto za kiafya unazopitia ukubwani. Hatari ya kupata tatizo inaongezeka zaidi endapo

  • uliwahi kufanyiwa upasuaji kwenye kizazi mfano kuondoa uvimbe
  • kutolewa mimba kwa vyuma (dilation & currettage) au upasuaji wakati wakujifungua(c-section)
  • historia ya kuugua PID mda mrefu
  • unatibiwa saratani

Zipi ni dalili kwamba una makovu kwenye kizazi?

Ukiwa na ugonjwa wa makovu kwenye kizazi unaweza kupata dalili nyingi. Dalili hizi ni pamoja na

  • kupata hedhi nyepesi sana(hypomenorrhea)
  • kukosa hedhi kabisa au kutokwa na damu nyingi kupita kiasi
  • kuhisi maumivu makali ya tumbo na nyonga
  • kushindwa kushika mimba mapema

Kwa baadhi ya wanawake hawapati dalili zozote kabisa, na wengine wanapata hedhi vizuri tu. Kama unahisi hitilafu kwenye via vya uzazi na hedhi yako na unatafuta mimba mda mrefu, muone daktari ili akupime kujua shida iko wapi.

Nini kinapelekea makovu kwenye kizazi?

Makovu kwenye kizazi yanaweza kusababishwa na changamoto mbalimbali. Sababu hizi ni pamoja na

1.Upasuaji kwenye kizazi kitaalamu (hysterectopy):– huu ni upsuaji ambapo daktaru anaingiza kifaa kidogo chenye camera kupitia kwenye uke kwenda kwenye kizazi. Lengo ni kukata vimbe mfano fibroids.

2.Kusafisha kizazi kwa vyuma baada ya kutoa mimba(Dilation & curretege): Unapotoa mimba kuna mabaki ya tishu yaweza kusalia kwenye kizazi. Hivo hospitali utafanyiwa upasuaji mdogo wa kutanua mlango wa kizazi kisha kukwangua mabaki yaliyopo kwenye kuta za kizazi. Kitendo hichi chaweza kuacha makovu kwenye kizazi chako ukasindwa kushika mimba siku zijazo.

3.Upasuaji wakati wa kujifungua(C-section): Upasuaji huu unafanyika pale inaposhindikana kujifungua kwa njia ya kawaida ya uke. Katika baadhi ya wanawake, upasuaji huu waweza kupelekea kuota kwa makovu kwenye kizazi. Kwa mama anayejifungua kwa upasuaji, makovu hutokea hasa kama akipata maambukizi baada ya hili zoezi.

4.Maambukizi kwenye kizazi: Maambukizi pekee hayapelekei upate makovu kwenye kizazi. Lakini maambukizi yanapotokea wakati unafanyiwa upasuaji, hatari inaongezeka zaidi. Maambukizi haya ni pamoja na PID na cervicitis

4.Matibabu ya mionzi: Matibabu kwenye saratani ya shingo ya kizazi yanayohusisha mionzi yanaweza kuacha makovu.

Je kitanzi chaweza kupelekea makovu kwenye kizazi?

Kitanzi ni kifaa kidogo mfano wa herudi T ambacho hutumika kupanga uzazi. Kifaa hiki huwekwa ukeni na mtalamu wa afya hospitali na kinaweza kukukinga usipate mimba hata kwa miaka 7. Kitanzi kinapowekwa ukeni kunakuwa na hatari ya kupata maambukizi na makovu kwenye kizazi.

Je vipimo gani huafanyika kugundua uwepo wa makovu kwenye kizazi?
Vipimo vya picha

Vipimo vya picha humsaidia daktari kupata undani wa tatizo lako kwa kulinganisha na dalili unazopata. Vipimo hivi vya picha vyaweza kufanya juu ya ngozi ama kuhitaji kuingiziwa kifaa ndani ya uke. Vipimo hivi ni pamoja na

1.Utrasound: Aina hii ya kipimo inahusisha mawimbi ya sauti kutengeneza picha ya ndani ya viungo vyako. Utrasound yaweza kufanyika eneo la juu la ngozi ama kwa ndani ya uke(trans-vaginal utrasound)

2.Hysteroscopy: Kwenye kipimo hiki mtoa huduma, anaingiza kifaa kidogo chenye camera kupitia uke ili kuchunguza uwepo wa makovu.

Je tatizo linatibiwaje Hospital

Daktari wako atachukua maelezo na vipimo kisha atapendekeza tiba sahihi ya taizo lako. Kumbuka ukiwa na daktari ni muhimu ujieleze dalili zote unazopata na historia yako. usiogope kumweleza daktari kama ulishatoa mimba mbili ay hata tano.

Lengo kubwa la tiba ni kuondoa makovu na kurudisha kizazi kwenye shape yake ya mwanzo. Tiba hii itasaidia

  • kuondoa maumivu unayopata
  • kurejesha mpangilio wako wa hedhi
  • kurejesha tena chansi ya kushika mimba endapo hujafikia menopause

Daktari anaweza kuingiza kifaa kidogo hysteroscope ili kuondoa makovu kwenye kizazi. Kifaa cha hysteroscope kinakuwa na cemara ya kutazama kuta za kizazi, lakini pia chaweza kutumika kuondoa makovu. Hatari iliyopo kwenye nnia hii ni kuharbu kuta mpya, yani kutengeneza makovu mengine tena.

Je naweza kushika mimba baada ya kutibiwa makovu?

Kwa kiasi kikubwa jibu ni ndio, unaweza kushika tena mimba baada ya tiba. Ugumba sometime ni tatizo gumu sana maana chanzo cha tatizo chaweza kutojulikama kabisa. Kama muhudumu ameona makovu ndio chanzo, maana yake kuyatoa makovu ni tiba yako kushika tena mimba.

je makovu kwenye kizazi yanaweza kupelekea mimba kuharibika?

Kumbuka bado waweza kupata mimba hata kama una makovu kwenye kizazi. Makovu kwenye kizazi yanaweza kupunguza ukubwa wa chumba cha kizazi. Hii inaweza kuleta shida kwenye ukuaji wa mimba, na kupelekea matatizo kama mimba kuharbika, kuzaa njiti ama kukatika kondo la nyuma. Pia tishu za makovu zaweza kuziba mlango wa kizazi na mtoto kutozaliwa vizuri.

Ushauri kutoka Maisha Doctors

Kama utahisi maumivu makali wakati wa hedhi, maumivu chini ya kitovu au kukosa mimba mda mrefu na uliwahi kufanyiwa upasuaji ama kutoa mimba, muone daktari.

Tiba asili kupitia Vidonge vya Uterus Cleansing Pills

Kwa wanawake wenye changamoto ya makovu kwenye kizazi tunawashauri kutumia tiba zetu hizi asili ili kuweka sawa mazingira ya kizazi. Dawa pia zinasaidia kusafisha uchafu na kuimarisha kizazi ili kuongeza chansi ya kushika mimba.

Matumizi: Dawa zipo kwenye mfumo wa vidonge 6 vya kuweka ukeni. Unaweka kidonge kimoja ukeni kinakaa siku 3 kisha unakitoa kupitia uzi mlaini. Baada ya masaa 24 unaweka kidonge kingine. Kumbuka usitumie wakati wa hedhi. Gharama ya dawa ni Tsh 150,000/=

Kwa ushauri na Tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *