Categories
Uzazi wa Mpango

Je Kitanzi ni Njia Salama Kupanga Uzazi?

Jinsi ya kutumia Kitanzi
kitanzi

Kama wewe ni mwanamke unayetafuta njia gani salama ya kutumia upange uzazi wako, basi bilashaka umewaza kuhusu njia ya kitanzi. Kitanzi ni njia salama kwa wanawake wengi sana kwa sasa japo siyo wote.

Wengi inawakaubali na haina madhara makubwa ukilinganisha na njia zingine kama njiti, vidonge na sindano.

Kitanzi ni Nini

Kitanzi ama intrauterine device ni kifaa chenye umbo la T kinachoingizwa kwenye kizazi cha mwanamke ili kuzuia mimba isitunge. Kinfanya kazi kwa kuzuia mbegu ya kiume isilifikie yai lililokomaa na kulirutubisha. Kitanzi kikitumika ipasavyo uwezo wake wa kuzuia mimba ni zaidi ya asilimia 99.

Aina za Kitanzi

Kuna aina kuu mbili za kitanzi cha Copper na kile cha homoni

Kitanzi cha homoni (Hormonal IUD)

Kitanzi cha homoni kinaitwa hivo kwasababu kinatoa kichocheo kiitwacho progestin. Kazi ya kichocheo hiki ni kufanya ute wa ukeni kuwa mzito kiasi ya kuzuia mbegu kulifikia yai. Progestin pia inafanya ukuta wa kizazi uwe mwembemba sana na hivo kuzuia upandikizaji.

Kitanzi cha copper (Copper IUD)

Kitanzi cha copper kinafanya kazi kwa kuua mbegu zinazoingia kwennye kizazi kabla hazijafikia kulirutubisha yai.

Faida za kitanzi cha Copper ni kwamba

  • haivurugi mpangilio wa homoni
  • kinaanza kufanya kazi mapema tu ukiweka
  • Kinaweza kukaa mda mrefu mpaka miaka 10 na kikafanya kazi ya kuzuia mimba

Hasara zake ni pamoja na

Kupelekea upate hedhi nzito sana: Hii ni kwa baadhi ya wanawake na siyo wote. Aina hii ya kitanzi haifai kama unapataga hedhi nzito yenye maumivu makali.
Aleji ya copper: watu wenye aleji na madini ya copper njia hii haitawafaa

Ni zipi faida za Kutumia Kitanzi?

  • kinaweza kutumika kwa muda mrefu bila kubadilisha
  • huhitaji kukagua ama kufatilia mara kwa mara, ukishaweka mara moja tu kwa usahihi inatosha
  • gharama yake ni nafuu na unalipia mara moja tu
  • ni salama kutumia hata kama unanyonyesha

Ni watu gani wanapaswa kutumia kitanzi?

Wanawake wote wenye afya njema wanaweza kutumia kitanzi. Muhimu kumbuka kitanzi hakizuii kutoambukizwa magonjwa ya zinaa. Na usitumie kitanzi kama

  • unaugua ugonjwa wa zinaa ama umeugua PID hivi karibuni
  • ni mjamzito
  • una saratani ya kizazi au ya shingo ya kizazi
  • una tatizo la kutokwa damu kusiko kawaida

Je hedhi yangu itabadilika baada ya kuweka kitanzi?

Baadhi ya wanawake hupata maumivu kiasi kwenye hedhi baada ya kuweka kitanzi na hedhi kuwa nzito sana. Kwa miezi michache ya mwanzoni baadhi wanaweza kuona hedhi ikivurugika. Wanawake wengi hupata hedhi kidogo ama wengine hukosa kabisa hedhi.

Je Mwanaume Atakigusa Kitanzi Wakati wa Tendo la ndoa?

Kama kitanzi kimewekwa vizuri basi mwanaume ni ngumu kugusa kitanzi wakati wa tendo. Lakini hata kama ikitokea hivo basi haiwezi kupunguza ladha ya penzi kwasababu pia kamba fupi za kitanzi zinazobaki nje ya uke huendelea kuwa laini zaidi kadiri muda unavoenda.

Je kuna Madhara ya Kutumia kitanzi?

Kitanzi ni njia salama zaidi ya kisasa kupanga uzazi. Wanawake wengi hupata madhara madogo madogo ya kawaida kama kizunguzungu ambayo huisha ndani ya muda mfupi. Mwanzoni unapoweka kitanzi tegemea kupata maumivu kama vile yale ya hedhi.

Kama unapata maumivu makali sana ya tumbo ama kutokwa damu, tembelea hospitali mapema kupata ushauri wa dakari.

Mmoja kati ya wanawake kumi waliowekewa kitanzi anaweza kupata vimbe ndogo ndogo kwenye mayai(ovarian cyst). Kwa kisi kikubwa vimbe hizi hazina madhara na huisha zenyewe bia dawa.

PID

Kama utapata dalili za tumbo kujaa, kuvimba na maumivu makali chini ya kitovu muhimu uende hospitali haraka.
Kwa kiasi fuani matumizi ya kitanzi huongeza hatari ya kuugua PID, ambayo ni maambukizi kwenye kizazi, mirija na mifuko ya mayai.

Dalili za PID ikiwa ni pamoja na

  • maumivu wakati wa tendo
  • kutokwa na uchafu wenye harufu mbaya ukeni
  • hedhi nzito kupita kiasi na homa.

Muone daktari mapema kama unaanza kupata dalili hizi ili utibiwe na kuepusha madhara zaidi ikiwemo kuziba kwa mirija.

Je kitanzi kinaweza kutoka chenyewe ?

Daktari atakuchunguza kama kitanzi hakipo sawa kila mara unapotembelea hospitali. Kitanzi kinatakiwa kishikiliwe na shingo ya kizazi. Kwa baadhi ya wanawake kitanzi kinaweza kutoka nje ya kizazi.

Hali hii hutokea hasa kama

  • hujawahi kuzaa
  • una umri chini ya miaka 20
  • umewekewa kitanzi mapema sana baada tu ya kuzaa au baada ya mimba kuharibika
  • una vimbe(fibroids) kwenye kizazi
  • kizazi chako kimeinama ama kina shape isiyo ya kawaida

Je vipi kama Nahitaji kuzaa kwa siku za baadae?

Kutumia kitanzi kwa watu wengi haitaathiri uwezo wako wa kushika mimba siku za baadae. Kama utafikia wakati unahitaji kubeba mimba ingine, tembelea hospitali onana na daktari muombe akutolee kitanzi. Baada ya hapo hedhi yako itarudi kuwa kawaida na utashika mimba mapema.

Je vipi kama sitashika mimba mapema?

Inatokea kwa wanawake wachache kupata madhara ya kitanzi, hasa kuvurugika kwa mazingira ya kizazi na hivo mimba kutoshika. Kwa grupu hili la wanawake tunawashauri kutumia hizi tiba asili ili kusafisha kizazi na kusaidia mayai kupevuka.

Asilimia 90 ya wanawake tuliowapa dawa hizi walishika mimba ndani ya miezi miwili. Kushoto ni dawa ya UCP kwa ajili ya kusafisha kizazi, ni dawa ya kuweka ukeni. Kulia Evecare ni dawa asili ya kurekebisha homoni, kuleta, ute na kusaidia mayai kupevuka.

Gharama ni Tsh 125,000/= kwa dozi hii ya wiki mbili.
Baada ya dozi utajipa miezi miwili ya kushika mimba

Makundi yasiyotakiwa kutumia Kitanzi

Japo kitanzi ni njia ya kisasa kupanga uzazi, haifai kwa kila mwanamke. Hutakiwi kutumia kitanzia endapo

  • una magonjwa ya zinaa ambayo hayajatibiwa
  • una saratani ya shingo ya kizazi na kizazi kwa ujumla
  • una matatizo kwenye kizazi chako kiasi inakuwa ngumu kwa daktari kukipachika
  • una magonjwa ini
  • una mimba

angalizo

Kuna wimbi kubwa la wajasiliamali mitandaoni wanauza vidonge fake vya evecare na ucp, tena wanauza kwa bei rahisi sana. Watu hao siyo madaktari wala siyo wataalamu wa afya na wanauza bidhaa feki ambazo ni hatari wa afya yako. Wengi wao hawana hata ofisi, ukipata madhara unakosa pa kuuliza. Kuwa makini na watu hao, wamejaa sana insta na fb

Unahitaji ushauri ama unataka tiba? Tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *