Categories
Natural remedies

Faida 8 za kunywa Green Tea

green tea
green tea

Green tea inasemekana kwamba ni moja ya kinywaji chenye afya sana duniani, na kinachopendwa zaidi.

Chai hii imejaa viondoa sumu vingi sana ambavyo vitakusaidia kuimarisha afya ya ubongo, kupunguza mafuta mabaya mwilini, kukulinga dhidi ya saratani na kupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo. Hapa chini ni maelezo ya nane za kunywa green tea.

1.Green tea ina viambata hai muhimu kwa ajili ya afya yako

Green tea ni zaidi tu ya chai kama ulivozoea. Ina viambata vya polyphenols, ambavyo vitakusaidia kupunguza mpambano(inflammation) kwenye mwili na pia kupambana na saratani.

Pia green tea ina viambata vya epigallocatechin-3-gallate(EDCCG). Viamabata hai hivi husaidia kuzuia madhara ya sumu mwilini na kulinda seli za mwili dhidi ya sumu.

2.Kuimarisha afya ya ubongo

Green tea inafanya kazi nzuri katika kukuweka kuwa mchangamfu na kuimarisha uwezo wa ubongo. Kiambata kikubwa ambacho kinaboost ubongo ni caffeine.

Usiogope kwamba ina caffeine nyingi kama kahawa hapana. Green ina kiwango kidogo tu cha caffeine ambacho kitachochea uzaishaji wa kemikali za dopamine na norepinephrine ambazo hufanya ubongo wako upige kazi zaidi.

Pia green tea inachochea ufanyaji kazi wa kemikali ya GABA. GABA ni ant-anxiety yaani inazuia msongo wa mawazo na hivo kukufanya ujisikie vizuri.

3.Kuondoa mafuta mabaya mwilini

Licha ya kuwa kiburudisho kizuri, green tea inachochea uwezo wa mwili kuunguza mafuta mabaya na hivo kupunguza uzito na nyama uzembe. Green tea inachochea shughuli za mwili na kupelekea mafuta kuunguzwa kuwa nishati.

4.Kupunguza hatari ya kuugua baadhi ya aina za saratani

Saratani husababishwa kukua kupita kiasi kwa seli za mwili. Ni moja ya ugonjwa unaaongoza kwa kusababisha vifo vingi sana duniani.

Tafiti zinasema kwamba seli zinapoathiriwa na sumu hupelekea seli hizi kuvimba na kuanzia kukua kupita kiasi. Viambata amana antioxidants zilizopo kwenye green tea husaidia kuzuia madhara ya sumu ambazo hupelekea saratani.

Tafiti zimebaini kwamba viondoa sumu vya kwenye green tea husaidia kupunguza hatari ya kupata aina hizi za saratani

Ili upate faida zaidi za green tea, epuka kuchanganya na maziwa. Baadhi ya tafiti zinasema kwamba unapochanganya na maziwa inapunguza ufyonzaji wa viondoa sumu.

5.Kulinda ubongo dhidi ya magonjwa ya uzee

Pamoja na kuimarisha ufanyaji kazi wa ubongo, green tea inasaidia kupunguza ubongo kuzeeka. Magonjwa makubwa yanayowakumba wazee kutokana na ubongo kuzeeka ni pamoja na Alzheimer na Parkinson. Magonjwa haya hupelekea ubongo kupungua uwezo wa kumbukumbu na pia kupunguza uwezo wa kufikiri.

6.Green tea itakusaidia kutibu harufu mbaya mdomoni.

Streptococcus mutans ni bakteria wanaopatikana sana kwenye mdomo. Bakteria hawa husababisha uchafu kuganda kinywani na kupelekea harufu mbaya na meno kuoza.

Kiamabata hai cha catechins kilichopo kwenye green tea kinasadia kudhibiti ukuaji wa bakteria hawa na hivo upunguza athari yake kwenye kinywa ikiwemo kuondoa harufu mbaya.

7.Green tea yaweza kukukinga na Kisukari cha Ukubwani.

Kisukari cha ukubwani ama type 2 diabetes ni aina ya kisukari inayompata mtu kuanzia miaka 20 kwenda juu. Aina hii husababishwa na mwili kushindwa kutumia insulini inayomwagwa kwenye damu ili kushusha sukari. Au mwili kutozalisha kiwango kinachotakiwa cha insulini.

Tafiti zinasema kwamba green tea husaidia kuongeza mwitikio wa mwili kwenye insulini na hivo kuzuia sukari kupanda kupita kiasi kwenye damu.

8.Green tea yaweza kuzuia magonjwa ya moyo

Magonjwa ya mfumo wa damu ikiwemo ikiwemo magonjwa ya moyo na stroke, ni moja ya chanzo kikubwa acha vifo duniani kote.

Tafiti zinasema kwmaba green tea yanweza kupunguza hatari ya kuugua magonjwa haya, kwa kupunguza mafuta mabaya mwili (bad cholesterol).

Green tea pia inaongeza viondoa sumu kwenye damu, na hivo kulinda mishipa ya damu dhidi ya athari ya mafuta mabaya(LDL). Mafuta haya mabaya huweza kusababisha damu kuganda na hivo kuzuia usambazaji wa hew aya oxygen mwilini.

Unahitaji Green kutibu changamoto zako? Agiza kutoka kwetu green tea zenye ubora mkubwa kwa Tsh 50,000/=

Hapa chini ni picha na maelezo mafupi kwa kila green tea zetu. Kumbuka hizi ni zaidi ya chai, ni tiba kwa magonjwa yako ya kiafya. Chagua unayohitaji kisha fika ofsini kuchukua. Ikiwa upo mkoani tutakutumia. Kila chai tiba ni tsh 50,000/=

Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Bofya kusoma makala inayofuata: Chanzo cha fangasi mdomoni+tiba

2 replies on “Faida 8 za kunywa Green Tea”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *