Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Hedhi salama

Hedhi Mara Mbili Katika Mwezi

hedhi mara mbili katika mwezi
kalenda ya hedhi

Mzunguko wa hedhi

Hedhi ya kawaida inachukua mzunguko wa siku siku 21 maka 35. Nikisema mzunguko namaanisha jumla ya siku kuanzia ulipopata hedhi mwezi mmoja, mpaka utakapopata hedhi tena katika mwezi unaofata. Makala hii itaongelea tatizo la kupata hedhi mara mbili katika mwezi na nini cha kufanya.

Japo siyo kawaida kupata mizunguko tofauti kila mwezi. Baadhi ya mizunguko yaweza kuwa mifupi au mirefu kuliko mingine, na hivo kupelekea upate hedhi mara mbili katika mwezi.

Tazama na dalili zingine

Katika nyakati nyingi kupata hedhi mara mbili ndani ya mwezi mmoja yaweza isiwe tatizo. Lakini kama inatokea kwa kujirudia ni muhimu kutazama na dalili zingine zinazoambatana. Endelea kusoma zaidi ili kujifunza kuhusu changamoto ya hedhi mara mbili katika mwezi

Hedhi mara mbili katika mwezi kwa mara ya kwanza

Watu wenye mzunguko mfupi mara nyingi sana wanapata hedhi mwanzoni na mwishoni mwa mwezi. Kwa mtu mwenye mzunguko wa kawaida wa siku 28 au zaidi, akipata hedhi mara mbili lazima ashituke.

Kumbuka hedhi isipotoka kwa wakati inaashiria changamoto ya kiafya. Ni ni rahisi sana kuchanganya hedhi na bleed ingine. Waweza kudhani ni hedhi kumbe unatokwa na damu tu kutokana na changamoto fulani.

Changamoto zinazoweza kupelekea bleed isiyo ya hedhi ni pamoja na

Mimba- mimba inapojishikiza kwenye ukuta wa kizazi yaweza kupelekea bleed. Ugonjwa wa zinaa: Magonjwa ya ngono yanaweza kupelekea upate bleed kidogo na kutokwa na uchafu usio wa kawaida ukeni.

Mimba kuharibika-Mimba inapoharbika inaambatana na maumivu makali na kutokwa na mabonge ya damu. Ni muhimu kwenda hospitali mapema ikiwa una mimba na umeanza kuona damu.

Mabadiliko ya uzito– Mazoezi kupita kiasi na mabadiliko makubwa ya uzito wa mwili yanaweza kupelekea hedhi mara mbili.

Uzazi wa mpango wa kisasa-Hedhi kuvurugika na kutoka mara mbili inatokea sana kwa wanaotumia njia za kisasa kuzuia mimba , mfano sindano, njiti na vidonge

Vimbe kwenye mlango wa kizazi na ukuta wa kizazi: Hizi ni vimbe ambazo siyo saratani kwenye kuta za mlango wa kizazi na kwenye ukuta wa kizazi, ambazo zaweza kupelekea upate hedhi zaidi ya mara moja.

Saratani ya mlango wa kizazi: kutokwa damu yaweza kuashiria uwepo wa saratani

Tofauti kati ya damu ya hedhi na bleed ya tatizo la via vya uzazi

Hizi dondoo zitakusaidia kujua kama damu unayopata ni hedhi ama siyo hedhi

Kama ni hedhi ya kawaida itakulazimu kubadili pedi au tampon kila baada ya masaa kadhaa. Na damu kawaida inakuwa nyekundu nzito au ya kungaa, brown au pink

Kama ni matone ya damu ambayo siyo hedhi, haitahitaji kubadili pedi au tamponi mara kwa mara, unaweza kutumia pedi moja tu kwa siku. Damu yake yaweza kuwa ya pick, brown na inakata mapema ndani ya siku moja au mbili

Chanzo kikubwa cha mzunguko mfupi na hedhi mara mbili katika mwezi

Nini kinapelekea hedhi mara mbili katika mwezi? inaweza kutokana na mzunguko mfupi ama changamoto ya kiafya inayopelekea bleed ukeni.

Baadhi ya mambo yanayopelekea hedhi mara mbili ni pamoja na

1.Kukaribia kukoma hedhi-Perimenopause

Perimenopause ni kipindi ambacho mwanamke anakarbia kukoma hedhi yake, wakati ambapo kunatokea mabadiliko makubwa ya homoni. Kipindi hichi waweza kupata hedhi mara mbili ndani ya mwezi mmoja. Perimenopasue inatofautiana kwa kila mwanamke.

Kuna wengine inachukua hata miaka 10 ndipo hedhi inakoma. Wakati wa kipindi hiki kuelekea kukoma, waweza kupata hedhi nzito sana, kuvusha miezi kadhaa bila hedhi, mzunguko kuwa mrefu , hedhi nyepesi sana. Menopause ndio kukoma hedhi kwenyewe. Mwanamke anakoma hedhi endapo atakosa hedhi kwa miezi 12 mfululizo.

2.Fibroids

Hizi ni vimbe zinazotokea kwenye kizazi. Ni vimbe zisizo saratani, na zaweza kuleta hedhi nzito, au ukavusha kabisa hedhi. Dalili zingine za fibroids ni pamoja na

  • kupata mkojo mara kwa mara
  • kuhisi uzito eneo la nyonga
  • maumivu chini ya mgongo
  • maumivu wakati wa tendo

Daktari atagundua kama una fibroids kwa kukufanyia kipimo cha utrasound.

3.Magonjwa ya tezi ya shingoni

Tezi huu huitwa thyroid, inakaa shingoni na ina umbo kama la kipepeo. Kazi ya tezi hii ni kuzalisha homoni ambazo zinaratibu mpangilio wa hedhi yako. Dalili za kwamba kuna tatizo kwenye tezi ya shingo ni pamoja na

  • kuhisi baridi mda wote
  • kuongezeka uzito
  • tumbo kujaa
  • kupungua mapigo ya moyo
  • kutoka na damu nyingi ya hedhi

Kwa upande mwingine ikiwa tezi yako inafanya kazi kupita kiasi utaanza kupata dalili hizi

  • kuhisi joto mda wote
  • macho kuvimba
  • moyo kwenda mbio sana
  • kukosa usingizi
  • kuharisha na
  • macho kuvimba

Hakikisha unaenda hospital, endapo utaanza kupata dalili hizi za tezi ya shingo.

Madhara zaidi ya kupata hedhi mara mbili

Watu wanaotoka kwenye familia zenye historia ya kuugua vimbe kwenye kizazi na kukoma hedhi mapema , wapo kwenye hatari zaidi ya kupata hili tatizo la hedhi mara mbili katika mwezi. Moja ya changamoto utakayopata kutokana na kupata hedhi mara mbili ni kupungukiwa damu. Dalili hizi zinaonesha kwamba umepungukiwa na damu.

  • mwili kuchoka sana
  • kizunguzungu
  • mapigo ya moyo kubadilika
  • kukosa pumzi
  • kuumwa sana kichwa

Je kuna umuhimu wa dawa kutibu hedhi mara mbili?

Hedhi mara mbili siyo tatizo ikiwa mzunguko wako ni mfupi. Japo ni muhimu sana kumuona daktari endapo kama utapata dalili hizi hapa chini

  • hedhi mara mbili kwa miezi mi2 au mi3 mfululizo
  • maumivu wakati wa tendo
  • hedhi nzito ya mabonge
  • damu ya kuganda
  • maumivu chini ya kitovu hasa kama maumivu hayaishi
  • maumivu makali kwenye hedhi
  • kupata matone ya damu katikati ya mzunguko ambayo yanajirudia mwezi unaofata

Kwa binti mdogo hakuna tatizo

Matibabu ya tatizo hili ya kupata hedhi mara mbili katika mwezi mmoja, yanategemea na chanzo cha tatizo. Watu wenye mzunguko mfupi au wanaopata hili tatizo kwenye miaka ya mwanzo ya kubalehe, hawahitaji tiba tatizo laweza kuisha lenyewe.

Tiba inalenga Chanzo cha Tatizo

Daktari anaweza kupendekeza akupe dawa za kurekebisha homoni zile za kupanga uzazi. Kama tayari unatumia dawa za kisasa za uzazi wa mpango, na unahisi ndio chanzo cha tatizo, mjulishe daktari ili akubadilishie njia ingine.

Kwa tatizo la tezi ya shingo: daktari anaweza kupendekeza vipimo zaidi na kukupa dawa kwa tatizo hili

Kama unakarbia kukoma hedhi: kuna dawa za hormone utapewa kupunguza ukali wa tatizo

Kwa vimbe yani fibroids: daktari anaweza kukupa dawa, ama akapendekeza upasuaji, kulingana na ukubwa wa tatizo.

Kubadili mtindo wako wa maisha pia utasaidia kurekebisha homoni zako, mfano kama una uzito mkubwa na kitambi, anza kufanya mazoezi na kupunguza vyakula vya sukari.

Tumia Evecare Kurekebisha hedhi yako ndani ya mwezi mmoja

evecare

Evecare ni dawa asili na imetengenezwa nchini India kupitia mimea ua Ashoka, Asaparagus na lodh tree. Kwa miaka zaidi ya mitano ambayo tumekuwa tukihudumia wagonjwa wetu wa matatizo ya hedhi na homoni, tumepokea shuhuda lukuki.

Dawa itakusaidia kurekebisha homoni na mzunguko wa hedhi ili uanze kupata hedhi vizuri. Evecare inakuwa na vidonge 30, unameza vidonge viwili kila siku kwa muda wa wiki mbili.

Gharama ni Tsh 75,0000/=. Kabla ya kukupa dawa, daktari atakusikiliza kwanza na kujua chanzo cha tatizo lako.

angalizo

Kuna wimbi kubwa la wajasiliamali mitandaoni wanauza vidonge fake vya evecare, tena wanauza kwa bei rahisi sana. Watu hao siyo madaktari wala siyo wataalamu wa afya na wanauza bidhaa feki ambazo ni hatari wa afya yako. Wengi wao hawana hata ofisi, ukipata madhara unakosa pa kuuliza. Kuwa makini na watu hao, wamejaa sana insta na fb

Ukiwa na maswali na uhitaji wa tiba Tuandikie whatsapp kwa namba 0678626254. Tupo Dar- Mwembechai

Bofya kusoma: Njia salama za kupunguza maumivu kipindi cha hedhi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *