Categories
Afya ya Meno na Kinywa

Ulimi Kuchubuka

ulimi kuchubuka
ulimi

Ulimi wako ni umetengenezwa kwa msuli wa tofauti sana na kipeke sana na umejishika kwenye mfupa eneo moja tu la mwishoni. Ngozi yake imejaa testa za ladha.Mwisho wa makala hii utakuwa umejua chanzo cha ulimi kuchubuka na hatua 7 za kutibu tatizo.

Kazi kubwa za ulimi ukiwa ni

  • kusaidia utafunaji wa chakula na kukizungusha chakula kwenye mdomo
  • kuonja chunvu, tamu na kitu kichungu
  • kutamka maneno vizuri na sauti

Ulimi kuchubuka yaweza kusababishwa na vitu vifuatavyo

1.Majeraha kwenye ulimi

Endapo ngozi ya ulimi ilipata majeraha, kinga ya mwili inaanza kupambana ili kutoa zile seli ziliokufa. Kitendo hichi kinaweza kupelekea ulimi wao kuchubuka.

Kuna njia nyingi zaweza kupelekea ukapata mejeraha kwenye ulimi wako, njia hizi ni pamoja na

  • kunywa kitu cha moto sana mfano chai
  • kunywa au kula kitu chenye tundikali kwa wingi mfano vinegar, malimau nk
  • kula au kunywa vyakula vichachu mfano pilipili
  • kujin’gata ulimi nyakati za kuongea au kula, ama umepata ajali ya kujigongesha

2.Fungus ya ulimi-oral thrush

Fungus ya ulimi inasababishwa na vimelea wa candida. Dalili kubwa ya ulimi wako kuwa na fungus ni utando mweupe na pia kuchubuka ngozi

3.Vidonda vya mdomo-canker sores

Vidonda vya mdomo vinaleta maumvu sana kwenye ulimi. Na vidonda hivi tunaweza kuvigawanya katika makundi matatu

Minor. Hivi ni vidonda vidongo vya ukubwa wa ml 2 mpaka 8, na huwa vinapona vyenyewe.

Major: hivi ni vikubwa na vinafikia cm 1, vikipona vinaacha alama

Herpetiform: hivi bi vidonda vingi vinajikusanya pamoja na kufanya kidonda kikubwa.

4.Mabaka kwenye ulimi -geographic tongue

Mabaka haya yanaweza kuwa na rangi tofauti na ngozi ya kawaida ya ulimi. Mabaka haya mengi hayaumi na ni ya kawaida hata siyo saratani. Yanaweza kubabuka na kuisha yenyewe.

Lini unatakiwa kumwona Daktari

Unatakiwa kumwona daktari endapo unapata dalili mbaya zaidi, na vidonda vinazidi kukua kila siku bila kuonesha nafuu. Pia watakiwa kwenda hospitali haraka endapo unapata

  • homa kali
  • unashindwa kunywa maji vizuri au kula
  • ulimi unapata vidonda mara kwa mara
  • maumivu ya ulimi yasiyoisha hata kwa dawa za kununua dukani
  • unanuka mdomo kupita kiasi
  • ulimi unavimba na unashindwa kupumua vizuri

Huduma ya kwanza kwa tatizo la ulimi kuchubuka

  1. Usitumie vyakula na vinywaj vya moto sana
  2. Uache kunywa pombe na kuvuta sigara
  3. Safisha meno yako mara kwa mara na hakikisha kinywa chako ni kisafi
  4. Epuka kula vyakula vilivyokaangwa kwenye mafuta, vichachu na vyenye tindikali kwa wingi
  5. Nunua supliment ya vitamin C na B-complex pharmacy utumie
  6. Weka maji ya vuguvugu na chunvi kiasi, kisha yazungushe mdomoni na uteme
  7. Weka kipande cha barafu kwenye kwenye kidonda kupunguza maumivu.

Bofya kusoma kuhusu: Fungus mdomoni