Categories
Hedhi salama Siku za hatari

Kumeza P2, Maswali na Majibu

vidonge vya p2
vidonge vya p2 kuzuia mimba

Nini Kinatokea P2 isipofanya kazi?

P2 ni vidonge vya kumeza kwa dharula tu ili kuzuia mimba isiyotarajiwa endapo hukutumia kinga. Lakini unaweza kuwa unajiuliza je kuna uhakika gani kama p2 zinakusaidia kuzuia mimba? Uwezo wake ni asilimia ngapi? Na vipi kama haitafanya kazi nini kitatokea?

Hapa chini kuna majibu ya maswali yako yote kuhusu p2 kutoka kwa watalamu na wabobezi wa afya ya uzazi. Tusome zaidi.

Je unaweza kushika mimba hata baada ya kumeza p2?

P2 ama morning after pill au plan B, ni dawa zilizopo kwenye kundi la levonorgestrel. Ambazo kazi yake ni kuzuia usishike mimba baada ya tendo endapo umesahau kinga, au kondomu imepasuka au ulifanya tendo ukiwa umelewa.

Dawa zinafanya kazi kwa kuzuia yai kutolewa kwenye ovary wakati wa ovulation, na hivo kuzuia mbegu na yai zisikutane kufanye kiumbe.

Muda sahihi wa kumeza p2 ni upi?

Kumbuka mbegu inapoingia kwenye uke inachukua saa 12 mpaka 48 kwenda kurutubisha yai. Na dawa inafanya kazi vizuri endapo utameza ndani ya masaa 12 baada ya kufanya tendo. Ukimeza ndani ya masaa 24 chansi ya kuzuia mimba ni asilimia 95 na zaidi.

Ukimeza kuanzia masaa 48 mpaka 72, yani siku 2 mpaka 3 baada ya kufanya tendo, chansi ya kuzuia mimba inapunguza mpaka asilimia 61 pekee. Kumbe sasa uwezekano wa kushika mimba hata kama ulimeza p2 unaongezeka kadiri unavochelewa kumeza kidonge.

Dalili gani nitapata baada ya kumeza p2?

Baada ya kumeza p2 tegemea kupata dalili ama side effects kama

  • kichefuchefu
  • maumivu ya tumbo
  • kichwa kuuma
  • kizunguzungu na
  • kutapika

Kama utatapika ndani ya masaa mawili bada ya kumeza dawa, unatakiwa umeze tena kidonge kingine ama utumie njia ingine ya kuzuia mimba kama condom.

Je uzito mkubwa na kitambi ni kikwazo cha p2 kufanya kazi?

Jibu ni ndio, tafiti zinaonesha kwamba wanawake wenye uzito mkubwa na kitambi wapo kwenye hatari ya kushika mimba hata kama wametumia p2 vizuri. Inashauri kama wewe ni mnene tumia kitanzi cha copper kama njia ya kisasa kuzuia mimba.

Dawa Zinapelekea P2 isifanye Kazi

Ni muhimu pia kujua kwamba baadhi ya dawa zinaweza kuathiri utendaji wa P2. Dawa kama za fungus, HIV, dawa za kifafa na baadhi ya antibiotic,. Sasa unapoenda dukani kununua P2, hakikisha unamweleza muhudumu hali yako ya kiafya na dawa unazotumia kwa muda huo.

Je p2 zinafanya kazi kwenye ovulation?

Dawa za p2 zinafanya kazi vizuri kabla ya ovulation, yani kabla yai halijatolewa. Hii ni kwasababu inazuia kabisa yai kutolewa kwenye ovari na hivo kuzuia urutubishaji.

Lakini hata kama yai limeshatolewa, kidonge kinazuia mbegu kulifikia yai, kwa kufanya ute wa ukeni uwe mzito sana kiasi mbegu zinashindwa kuogelea.

Kama pengine umechelewa kumeza kidonge, na tayari yai limerutubishwa, basi kidonge kinazuia kiumbe kujishikiza kwenye ukuta wa kizazi na hivo mimba haitakuwepo.

Je kuna madhara kwa mjamzito kumeza P2?

Ni muhimu pia kujua kwamba, endapo umemeza kidonge bahati mbaya bila kujua kumbe kuna mimba, haitakuwa na madhara. Kiumbe kitaendelea kukua pasipo shida.

Maelezo ya Mwisho Kuhusu P2

Meza p2 kwa emergency tu na siyo kila siku. P2 ziapelekea hedhi kuvurugika na homoni kuvurugika. Tumia kwa tahadhari na usizoee kuzimeza kila siku.

Endapo unatafuta njia ya kupanga uzazi ya mda mrefu, tafadhali tembelea hospitali uonane na muhudumu akupe maelekezo.

Kwa ushauri zaidi na tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Soma hapa ikiwa hedhi yako Imevurugika na unataka kuiweka sawa.

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Siku za hatari

Je Unaweza Kushika Mimba Kwenye Hedhi?

kushika mimba kwenye hedhi
Upt

Endapo unatafuta mimba kwa muda mrefu bila mafanikio au unataka kushika mimba haraka, ni muhimu kufatilia kwa makini mzunguko wako wa hedhi kujua zipi siku za hatari. Moja ya imani potofu sana kwa wengi ni kuamini mwanamke hawezi kushika mimba kwenye hedhi.

Japo uwezekano ni mdogo wa kushika mimba wakati wa hedhi lakini inawezekana. Hapa chini ni maelezo ya kina unayotakiwa kufahamu kuhusu kufanya tendo na kushika mimba wakati wa hedhi.

Mimba inatungwaje?

Mchakato wa kushika mimba kwa mwanamke ni moja ya maajabu makubwa sana ya uumbaji wa binadamu. Yahitaji mbegu kutoka kwa mwanaume iungane na yai kutoka kwa mwanamke.

Yai likishapevuka na kutolewa kutoka kwenye mfumo wa mayai, linaweza kushi kwa masaa 12 mpaka 48 kabla ya kuharibika. Mbegu ya amwanaume ikishatolewa inaweza kuishi ndani ya kizazi cha mwanamke kwa siku mpaka tatu mpaka tano.

Siku za hatari

Wanawake wengi hupata hedhi kila baada ya siku 28 mpaka 33 za mzunguko. Na wengi wao mayai hukomaa siku ya 14 baada ya hedhi . Siku yai kutolewa inaweza pia kuwa ya 12, 13 14 au 15, siku hizi ndizo tunaziita siku za hatari.

Kitendo cha yai kupevuka na kutolewa kwa ajili ya urutubishaji huitwa ovulation. Na endapo kama yai na mbegu vitakutana basi uwe na uhakika mimba itatungwa.

Nini kinapelekea kushika mimba kwenye hedhi?

Siku ya yai kupevuka na kutolewa inatofautiana kulingana na mzunguko wako. Baadhi ya wanawake wenye mzunguko mrefu wa siku mpaka 35, ovulation yaweza kutokea siku ya 21 . Na wanawake wenye mzunguko mfupi zaidi wanaweza kushika mimba hata siku ya 7 ya hedhi.

Sasa kwa mantiki hii, chukulia hedhi yako inachukua siku 6 kuisha. Umefanya mapenzi na mtu katika siku ya tano ya hedhi, na yai ikapevuka siku ya 7, na tunajua mbegu zinaweza kukaa siku mpaka 6 ndani ya kizazi. Maana yake unaweza ukashika mimba ukikutana na mwanaume kwenye siku za hedhi yako.

Sababu ingine ni kuchanganya bleed ya ovulation na bleed ya hedhi.

Wakati wa ovulation mwanamke anaweza kupata matone kidogo ya damu kwa siku moja . Wanawake wengi waaweza kuhisi ni damu ya hedhi. Kufanya tendo bila kinga katika muda huu utaweza kushika mimba.

Kama unahitaji kufatilia vizuri kujua siku zako za hatari, anza kwa kuweka rekodi ya mizunguko yako ya hedhi kwa miezi walau mi4. Andika lini unaanza hedhi, unamaliza baada ya muda gani, hedhi yako ikoje?.
Ukifatilia kwa miezi kadhaa ni rahisi kujua siku zako za hatari na ukaweza kucheza salama.

Uwezekano ukoje wa kushika mimba kwenye hedhi?

Chansi ya kushika mimba kwa mwanamke unaongezeka na kupungua kulingana na mwenendo wa siku zako za yai kupevuka. Uwezekano wa kushika mimba siku ya kwanza na ya pili ya hedhi ni mdogo sana chini ya asilimia 1.

Baada ya kuanza hedhi kwenye siku ya 13 uwezekano wa kushika mimba ni karibu asilimia 9 na chansi kuongezeka zaidi siku ya ovulation.

Tumia uzazi wa mpango kuepuka kushika mimba kwenye hedhi

Endapo bado hujajiandaa kabisa kushika mimba unaweza kuamua kutumia uzazi wa mpango. Nenda hospitali, onana na daktari atakupa maelekezo ya njia zote zinazopatikana ikiwemo faida na hasara za kila njia ya kupanga uzazi.

Baada ya maelezo ya daktari, utaweza kuchagua njia sahihi ya kutumia itakayokufaa ili kuzuia kushika mimba kwenye hedhi. Kumbuka tu kwamba njia nyingi za uzazi wa mpango haziwezi kukuzuia kupata magonjwa ya zinaa.

Zitakukinga tu dhidi ya miba isiyotarajiwa. Kama huna uhakika na mwenzi wako, hakikisha unatumia kinga kama kondomu, itakusaidia kukukukinga na magonjwa ya zinaa na mimba pia.

Hitimisho

Mzunguko wa hedhi unatofautiana kwa kila mwanamke, hivo inawezekana kabisa ukashika mimba siku za hedhi. Japo chansi ya kushika mimba ni ndogo mwanzoni mwa hedhi ila kadiiri unavokarbia siku ya ovulation chansi inaongezeka.

Kama umeshajaribu kutafuta mimba kwa zaidi ya mwaka mmoja bila mafanikio, muone daktari kupata vipimo na tiba. Daktari anaweza kukwelekeza vizuri namna ya kufatilia siku za hatari ili ushike mimba mapema.
Daktari pia anaweza kukufanyia vipimo kadhaa na kukupa dawa za kuchochea upevushaji wa mayai na kuongeza chansi ya kushika mimba.

Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Bofya kusoma makala inayofuata: Jinsi ya kugundua siku za hatari kushika mimba