Categories
Magonjwa ya viungo

Miguu kujaa maji, Chanzo, Ushauri na Tiba

miguu kujaa maji
mguu uliovimba

Nini maana ya miguu kujaa maji?

Kujaa maji kitaalamu edema, ni kitendo cha kuvimba kwa maneneo mbalimbali ya mwili. Unaweza kujaa maji kwenye miguu, enka, usoi na hata mikono. Yatokana na kukusanyika kwa majimaji yasiyohitajika eneo husika. Makala yetu itajikita zaidi kwenye miguu kujaa maji na nini kifanyike kutibu shida yako.

Miguu yako inavimba kwa sababu kubwa mbili

1.Maji kujikusanya(edema)

Hapa inatokea pale tishu au mishipa ya damu inaposhikiia maji mengi kuliko inavotakiwa. Kukaa mda mrefu wakati unafanya kazi, au ukiwa kwenye ndege, mabadiliko ya homoni wakati wa mimba hata kusimama mda mrefu yaweza kupelekea hali hii.

Mwili wako kumbuka umetengenezwa kwa maji asilimia 60. Sasa inapotokea hakuna uwiano mzuri wa amji, inapelekea kiwango fulani cha maji kuegemea eneo lingine zaidi.

2.Kututumka(inflammation)

Hii inatokea pale tishu za miguu zinapochokozwa na kitu kigeni na hivo kuvimba. Ni kawaida eneo la mwili kuvimba pale kunapotokea hitilafu. Endapo utavunjika mfupa eneo la maungio, ama kuna baridi yabisi, lazima eneo husika livimbe kukupa ishara kwamba kuna shida.

Magonjwa na changamoto zinapelekea miguu kujaa maji

1.Moyo kufeli

Hii inatokea pale moyo wako unapokuwa dhaifu katika kupump damu kwenda maeneo mbalimbali ya mwili. Dalili zingine za kufeli kwa moyo ni pamoja na

  • pumzi kukata na kushindwa kupumua vizuri
  • mwili kuchoka sana
  • kukohoa kupita kiasi

2.Matatizo kwenye mishipa ya damu

Matatizo makubwa mawili kwenye mishipa ya damu ambayo kitaalamu tunaiata Deep vein thrombosis(DVT) na thrombophlebits yanaweza kupelekea miguu kuvimba. Ukiwa na hizi changamoto maana yake kuna kipande cha damu kimegamda kwenye mshipa na hivo kuzuia usafirishaji.

Muone daktari mapema endapo utaona dalili

  • maumivu kwenye miguu na mguu kuwa laini
  • ngozi kuwa nyekundu au blue
  • ngozi yenye hali ya joto kuliko kawaida
  • maumivu baada ya kukaa au kusimama mda mrefu
  • ngozi kuwa kavu na inayobabuka na
  • malengelenge kwenye ngozi ya mguu

3.Magonjwa ya figo

Figo zinapopata hitilafu kwa mda mrefu, zinafeli kufanya kazi yake ya kuchuja maji. Na matokeo yake kiwango kikubwa cha maji kinahifadhiwa kwenye mwili badala ya kutolewa nje.

Maji yanayobaki yanaweza kujikusanya kwenye miguu na mikono. Ukiwa na tatizo kwenye figo na kisha maji yamejaa waweza pia kupata dalili zingine kama

  • mwili kuishiwa nguvu
  • kushindwa kupumua vizuri
  • kiu kupita kiasi
  • kichefuchefu
  • kuwashwa na kutoa damu

4.Mimba

Kwa wajawazito wengi, mimba inapofikia wiki 25, inakuwa ni mimba kubwa na inaleta mgandamizo kwenye mishipa yako ya damu. Mgandamizo huu unapunguza kiwango cha damu kinachosafiri na hivo kupelekea miguu na mikono kujaa maji.

Endapo una mimba na umeona dalili hizi hakikisha unaenda hospitali haraka, kwani siyo dalili njema. Dalili mbaya ni

  • kuvimba kupita kiasi hasa maeneo ya macho
  • maumivu ya kichwa kupita kiasi
  • macho kushindwa kuhimili mwanga na kushindwa kuona vizuri

Kama umepata dalili za miguu kuvimba, kukosa pumzi baada tu ya kujifungua, ongea na daktari kama unaweza kuwa na changamoto ya moyo. Atakupangia vipimo na utapata uhakika wa afya yako.

5.Baridi yabisi na magonjwa mengine ya joints

Magonjwa haya yamegawanyika: Nitayaelezea kila moja na dalili zake

Gout

Gout ni ugonjwa unaosababishwa na kuongezeka kwa uric acid kwenye damu. Acid hii inapojikusanya maeneo ya maungio huleta maumivu makali sana na kupelekea eneo hilo kuvimba. Utajiona kama una gout endapo unaamka asbhi, dole gumba la mguuni lina maumivu makali kama sindano inachoma.

Osteoarthritis

Hii ni aina ya baridi yabisi ambapo mgonjwa anapata maumivu na kuvimba kutokana na kuchoka kwa maungio. Hii inawapat zaidi wazee

Rheumatoid arthritis

Ugonjwa huu ni aina ya baridi yabisi ambapo kinga ya mwili inapambana na tishu za mwili. Ugonjwa unaweza kumtokea mtu wa umri wowote.

Majeraha

Kama mfupa umevunjika, au enka kuteguka, inaweza kupelekea eneo hilo kuvimba. hii ni namna ya kawaida kabisa ya mwili kuvimba kutokana na shambulizi. Kitendo cha kuvimba ni ishara kwamba mwili unapambana kulitibu eneo husika.

Cellulitis

Haya ni maambukizi ya bakteria kwenye eneo la ndani la ngozi. Dalili zingine za cellulitis ukiacha kuvimba ni pamoja na

  • homa
  • maumivu ya ngozi
  • eneo la ngozi kutengeneza dimple yani mbonyeo
  • ngozi kuwa laini sana kupita kiasi
  • wekundu kwenye ngozi unaoongezeka kila siku

Nini cha kufanya endapo miguu yangu imevimba?

Unaweza kujaribu huduma hizi za kwanza wakati ukijiandaa kwenda hospitali

  1. Punguza vyakula vyenye chunvi
  2. Weka ratiba ya kufanya mazoezi mepesi kila siku
  3. Usikae mda mrefu bila kusimama na kutembea
  4. Kama una uzito mkubwa na kitambi, lenga kurekebisha uzito wako kwanza

Lakini kwasbaabu kuvimba kwa miguu kunaweza kuashiria tatizo kubwa la kiafya, usipuuze dalili zake. Hakikisha unaenda hospitali mapema kupimwa kujua shida iko wapi.

Bofya kusoma kuhusu: Miguu kuwaka moto

Categories
Magonjwa ya viungo

Miguu kuwaka moto

miguu kuwaka moto
ganzi mguuni

Nini maana ya miguu kuwaka moto?

Miguu kuwaka moto ni tatizo kubwa sana kwa sasa. Maumivu haya yanaweza kuwa ya mda mfupi au yakakaa mda mrefu bila kuisha. Miguu yako itahisi hali ya kuungua na kufa ganzi. Maumivu huwa makali sana hasa nyakati za usiku.

Matibabu ya changamoto ya miguu kuwaka moto yanategemea na chazo cha tatizo lako. Endelea kusoma zaidi makala hii ili ujue chanzo cha tatizo lako na tiba sahihi inayokufaa.

Sababu 10 zinazokufanya upate tatizo la miguu kuwaka moto

1.Miguu kuwaka moto kwasababu ya kisukari-Diabetic Neuropathy

Kisukari kinapokusumbua kwa mda mrefu kinapelekea mishipa midogo ya fahamu kuathirika. Mishipa inapoathirika inakwamisha pia usafirishaji wa taarifa ndani ya mwili.

Taarifa zisiposafirishwa vyema inapelekea changamoto kwenye kuhisi matukio ya ndani na nje ya mwili. Pia kisukari kinaharibu mishipa ya damu ambayo inabeba hewa safi ya oksijeni ndani ya mwili.

Mishipa ya fahamu inaweza kuathiriwa maeneo mbalimbali ya mwili. Na athari hii inaongeza endapo una

  • uzito mkubwa na kitambi
  • presha ya kupanda imeongezeka
  • unavuta sigara
  • kunywa pombe

Aina za ganzi ya kisukari

Athari za mishipa ya fahamu kitaalamu tunaita neuropathy, lakini kuna aina za neuropathy. Aina kubwa ambayo inawatokea zaidi wagonjwa kisukari ni peripherial neuropathy.

Peripherial maana yake ni maeneo ya pembezoni, hivo ni athari ya mishipa ya fahamu iliyo kwenye viungo vya pembezoni mwa mwili. kama vidole vya miguuni na mikononi.

Dalili zingine za hii peripherial neuropathy ni pamoja na

  • kuhisi mguu na mikono kufa gani
  • kuhisi kama umevaa kitu cha kubana mfano wa sox
  • maumivu makali ya haraka na kupotea
  • kutokwa jasho jingi kupita kiasi na
  • miguu na mikono kukosa nguvu

Ni muhimu sana kumwona daktari endapo umegundua una dalili za ganzi ya kisukari. Kwenye kutibu tatizo lako utatakiwa kurekebisha kwanza kisukari ili mishipa isiendelee kuathirika zaidi.

2.Matumizi ya pombe

Watu wanaokunywa sana pombe wapo kwenye hatari ya kuathirika mishipa ya fahamu, na hii kitaalamu inaitwa alcoholic neuropathy. Aina hii ya ganzi inaweza kusababisha maumivu kwenye unyayo na miguu kukosa nguvu.

Tiba kwa ganzi ya aina hii kuacha kwanza pombe na kubadili lishe yako kwa kula mlo kamili. Endapo utaacha pombe itapunguza athari zaidi na pia kuondoa zile dalili mbaya.

3.Upungufu wa lishe.

Upungufu wa Vitamin B kwenye lishe yako kunaweza kupelekea upate tatizo la miguu kuwaka moto.
Kupungukiwa damu pia inatokana na upungufu wa vitamin B.

Dalili zingine za kwamba una upungufu wa damu na kupelekea ganzi ni pamoja na kukosa nguvu, uchovu, kushindwa kupumua vizuri na kizunguzungu

4.tatizo kwenye tezi ya shingo-thyroid

Kuna changamoto mbili za tezi ya shingoni. Ni aidha tezi inafanya kazi chini ya kiwango- hypothyrpoidsm au inafanya kazi kupita kiasi-hypethyrodism. Tezi inapofanya kazi chini ya kiwango, yaweza kupelekea mishipa ya fahamu kuathirika na hivi kukufanya miguu yako iwake moto.

5.Magonjwa ya kuambukiza

Mishipa ya fahamu inaweza kuathiriwa kutokana na magonjwa mbalimbali ya kuambukiwa, na hivo kukufanya upate ganzi kwenye miguu. Magonjwa haya ni pampja na

Kama unahisi una magonjwa haya ya kuambukiza, ongea na daktari ili aweze kukupima.

6.Fungus ya Miguu-athletes foot

Hii ni aina ya fungus ya miguu inayoambukizwa kwa kasi sana, na inaathiri unyayo, mikono na kucha pia. Ugonjwa huu pia huitwa tinea pedis.

Dalili kubwa ya fungus kwenye miguu mi kuwasha kwenye unyayo na dali zingine ni pamoja na

  • malengelenge kwenye unyayo
  • ngozi kunyonyoka katikati ya vidole na kwenye unyayo
  • ngozi kuwa kavu pembeni ya mguu na kwenye unyayo
  • kucha kugeuka rangi kuwa yeusi na nene sana kuliko mwanzo

7.Magonjwa ya figo

Kazi ya figo ni kuchuja mkojo na kutoa taka kupitia njia ya mkjo na jasho. Kama figo hazifanyi kazi vizuri, inapelekea sumu kujikusanya kwenye mfumo wako. Sumu zinapojikusanya zaweza kupelekea ganzi kwenye na miguu kuwaka moto.

Karibu asilimia kumi ya watu wenye magonjwa ya figo wanapata hili tatizo la kuvimba miguu kunakoambatana na kuwaka moto.

Wagonjwa wa figo waliopo kwenye huduma ya kusafisha damu yani dialysis, wanapta hii changamoto ya miguu kuwaka moto. Hii ni kwasababu wanakuwa na upungufu mkubwa wa virutubishi mwilini. Tiba ya kusafisha damu-dialysis inaondoa vitami B1 kwenye damu.

Kufeli kwa figo oia kunasababisha dalili hizi

  • kuvimba miguu
  • muwasho
  • kichwa kuuma
  • maumivu
  • joint kuwa ngumu na kujaa maji
  • kuhisi ganzi na viungo kukosa nguvu

8.Peripherial artery disease

Artery ni mishipa inayosafirisha damu yenye hewa safi ya oksijeni mwilini. Kwahivo kama damu isipofika eneo fulani la mwili, inapelekea ganzi na hali ganzi na kuwaka moto maeneo ya miguu na vidole vya mikono.

9.Matibabu ya Chemotherapy

Tiba hii inahusisha matumizi ya dawa zenye nguvu sana ili kuharbu seli za saratani. Chemotherapy ina madhara kiasi kwenye mwili, ikiwamo kuleta matokeo mabaya kama

10.Kukaa kwenye mazingira yenye sumu

Unapofanya kazi maeneo yenye kemikali nyingi, mfano viwandani au kwenye mionzi yaweza kukupelekea uathirike mishipa ya faham na hivo kupelekea miguu kuwaka moto. Pia dawa baadhi mfano za ukimwi na kifafa zaweza kupelekea athari kwenye mishipaya fahamu.

Tiba ya nyumbani itakayokupa nafuu kwa miguu kuwaka moto

  1. Chovya miguu yako kwenye maji baridi au kwenye barafu kwa dakika chache kisha utoe
  2. Chovya miguu yako kwenye maji yenye chunvi au apple cider vinegar. Kama una kisukari muulize kwanza daktari wako kama njia hii ni sahihi
  3. Tumia chai ya manjano. Manjano ya kiambata cha curcumin ambacho kinapunguza maumivu kwenye neva
  4. Fanya masaji kwenye mguu ili kurahishisha usafirishaji wa damu.