Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Hedhi salama

Maumivu ya Tumbo la Chango

tumbo la chango

tumbo la chango

Chango ni kitu gani hasa?

Tumbo la chango au mchango, wengi husema wakimaanisha maumivu makali ya tumbo kipindi cha hedhi. Kitalamu maumivu haya huitwa dysmenorrhea, ikimaanisha maumivu kutokana na kujikaza kwa ukuta wa kizazi ili ubomoke na kutoa damu kipindi upo kwenye hedhi.

Aina za tumbo la chango

Kuna aina kuu mbili za maumivu haya ya hedhi ama mchango, ambayo ni primary dysmenorrhea na secondary dysmenorrhea.

Primary Dysmenorrhea (Tumbo la Chango la kawaida)

Chango hili la uzazi ni yale maumivu ya kawaida yanayokupata kila mwezi kwenye hedhi na hayatokani na ugonjwa wowote. Maumivu haya huanza siku moja ama mbili kabla hujapata hedhi yako. Waweza kuhisi maumivu kwenye nyonga, kiuno na tumbo pia.

Pia chango la namna hii huchukua masaa 12 mpaka 73 yani siku 3 kuisha, na inaambatana na dalili zingine kama kichefuchefu na kutapika na hata kuharisha. Chango la namna hii huwa linapungua kadiri unazozeeka ama pale utakapozaa.

Secondary Dysmenorrhea (Tumbo la Chango lisilo Kawaida)

Chango lako linaposababishwa la ugonjwa fulani kwenye via vya uzazi. Chango hili huanza mapema zaidi kwenye mzunguko hata wiki kabla na inachukua mda mrefu sana kuisha. Mara nyingi chango hili halina dlaili za kuchefuchefu, kutapika kukosa nguvu na kuharisha.

Nini kinapelekea upate maumivu makali sana kwenye hedhi?

Maumivu hutokea pale kemikali inayoitwa prostaglandin inapofanya ukuta wa kizazi kujikaza. Ukuta wa kizazi ambapo mtoto hujishikiza na kukua,umetengenezwa kwa misuli, na unajikaza kwenye hedhi ili kubomoka kutoa damu isiyohitajika.

Ukuta unapojikaza sana, unaleta mgandamizo kwenye mishipa ya karibu ya damu, na hivo kupunguza kiwango na hewa safi ya oksijen kwenda kwenye misuli. Na misuli inapokosa hewa ndipo unapata maumivu makali.

Chango la uzazi kutokana na ugonjwa

Chango hili laweza kutokea kwa kusababishwa na ugonjwa fulani, changamoto hizi ni pamoja na

  1. Endometriosis: Changamoto ambapo kuta za kizazi zinakua na kwenda nje ya kizazi. Tishu hizi nyakati za hedhi zitapelekea maumivu makali na kuvimba.
  2. Adenomysis: Hili ni tatizo ambapo kuta za kizazi zinakua kuelekea kwenue misuli ya kizazi. Tatizo hili kaweza kupelekea kizazi kutanuka na hivo kuletea bleed nyingi yenye maumvu
  3. PID: Haya ni maambukizi ya bakteria kwenye njia ya uzazi. PID yaweza kuleta maumivu makali chini ya kitovu, kwenye tendo na maumivu nyakati za hedhi yani chango.
  4. Fibroids: Hizi ni vimbe ambazo siyo za saratani ndani au nje ya kizazi, zinazopelekea chango kali sana
  5. Cervical stenosis: Hiki ni kitendo cha mlango wa kizazi kusinyaa na hivo kuzuia damu kutoka kwa kasi nzuri hivo kuleta maumivu ya chango kwenye hedhi.

Vipimo: Utajuaje kama Chango lako la kawaida au ni hatarishi?

Kama chango lako linachukua zaidi ya siku 3, hakikisha unaenda hospitali kufanyiwa vipimo. Kumbuka aina zote za chango zinaweza kutibiwa hospital na hata kwa tiba asili. Muhimu kwanza ni kujua nini kipo nyuma ya chango lako.

Kwanza kabisa daktari atakwambia ujieleze dalili zote unazopata kwenye hedhi pamoja na mzunguko wako ukoje. Pili daktari atakufanyia vipimo ndani ya via vya uzazi(pelvic exam) ambapo ataingiza kifaa ukeni kucheki kama kuna hali yoyote isiyo ya kawaida kwenye uke, mlango wa kizazi na kizazi chenyewe.

Daktari anaweza pia kuchukua kiwango cha majimaji kwenye uke na kupeleka maabara kwa ajili ya vipimo zaidi.

Nini kinatokea kama kuna ugonjwa?

Kama daktari atahisi pengine kutokana na dalili zako una chango la ugonjwa, hapo utafanyiwa utrasound. Na ikionekana kuna shida, daktari atajikita zaidi kukutibu tatizo husika.

Nini cha Kufanya ili Kupunguza Maumivu ya Chango kwa Muda

Kuna njia nyingi ambazo husaidia kupunguza maumivu ya hedhi ambazo unaweza kutumia ukiwa nyumbani kwako kabla ya kwenda hospitali. Kama maumivu ni makali sana unaweza:-

  • Kumeza dawa za kukata maumivu kama ibuprofen kwa ahueni ya haraka. Angalizo: dawa za maumivu isiwe ni nia ya kutumika kila mara kwani madhara yake ni makubwa kiafya, dawa hizi zitumike kwa uangalifu.
  • Tumia maji ya uvuguvugu kukandakanda mahali pa tumbo la chini
  • Epuka kuvuta sigara na kunywa pombe kipindi cha hedhi
  • Usitumie vinywaji na vyakula vyenye caffeine mfano majani ya chai na kahawa
  • Fanya masaji kwenye upande wa chini wa mgongo na sehemu ya tumbo la chini.
  • Pata muda mwingi wa kupumzika
  • Weka ratiba ya kufanya mazoezi mara kwa mara: Tafiti zinasema wanawake wanaofanya mazoezi hupunguza maumivu ya hedhi kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na wasiofanya mazoezi.

Lini natakiwa Kumwona Daktari?

Chango linapokuwa kali sana linapelekea baadhi ya wanawake washindwe kufanya kazi zao na kushindwa kwenda darasani. Huhitaji kabisa kuvumilia mateso ya namna hii, unahitaji kuishi vizuri na kufurahia maisha. Kama maumivu hayavumiliki hakikisha unaenda hospital haraka.

Jua mzunguko wako

Ni muhimu sana kujua mzunguko wako, pia ujue maumivu huwa yanaanza siku ngapi kabla ya hedhi. Kama chango linaambatana na dalili zingine mfano maumivu makali ya kichwa, bleed nzito sana na nyingi, nenda hospitali.

Je Tumbo la Chango Linapelekea Ugumba?

Kama tulivoona kwamba chango siyo ugonjwa bali ni dalili za maumivu makali ya tumbo la hedhi. Sasa kama unapata chango la kwanza (primary amenorrhea) hapo hakuna kikwazo cha kushika mimba. Lakini kama chango lako ni ile aina ya pili yani secondary amenorrhea, hapo lazima kuwe na kikwazo kushika mimba mapema.

nini ufanye kama umetafuta mimba mda mrefu bila mafanikio?

Endapo wewe na mme wako mmetafuta mimba kwa zaidi ya mwaka mmoja, nendeni hospitali wote wawili kupimwa kujua chanzo cha tatizo. Mwanamke utapima mirija, kizazi na homoni na mwanaume atapimwa mbegu kuona kama zina hitilafu.

Unahitaji ushauri na tiba? Tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Hedhi ya kuteleza kama mlenda

hedhi ya kuteleza

Kama hujawahi kupata hedhi ya kuteleza mithili ya mlenda, inaweza kukuchanganya sana akili siku ya kwanza.

Kwa mwanamke kuwa na mzunguko mzuri wa hedhi ni jambo la kujivunia na linaloleta heshima sana. Mzunguko wa hedhi unaweza kutoa picha kamili nini kinaendelea kwenye mwili wa mwanamke. Kama mfuko wa mimba unapata mzunguko mzuri wa damu, homoni zako zinbalansi, au kama mayai yanatolewa kwenye ovari

Makala hii itaongelea kwa kina juu ya hedhi ipi ni salama na ipi siyo salama. Karibu tujifunze kwa ajili ya afya yako.

Hedhi ya kuteleza kama mlenda.

Kwa kiasi kikubwa kupata hedhi ya mlenda ni kutokana na damu iliyoganda kwenye ukuta wa kizazi inetolewa nje. Endapo unapata mabonge madogo madogo ya damu ujue ni jambo la kawaida kabisa.

Kumbuka kwamba unapoanza hedhi ndio mwanzo wa mzunguko wako. Ni kipindi ambacho ukuta wa kizazi unabomoka kwasababu yai halikurtubishwa. Hedhi ni mchanganyiko wa damu ya ukuta wa mji wa mimba, maji maji ya ukeni na yai lisilorutubishwa.

Kumbuka pia kwamba siku ya kwanza ya hedhi inaweza kutoka nyingi na nzito kuliko siku zingine.

Hedhi kidogo inayoambatana na maumivu makali ya tumbo

Kama unapata hedhi nyepesi, nyekundu inaweza kuashiria kwamba mzunguko wa damu kwenye mfuko wa mimba ni mdogo. Unaweza kupunguza hali hii kwa kufanya masaji kwenye eneo la tumbo ukitumia mafuta ya mnyonyo, ama kitambaa kilicholowekwa kwenye maji ya moto.

Hedhi ya vipande vipande vya damu

Kadiri hedhi inavoendelea, unaweza kuanza kupata hedhi kama ya damu iliyoganwanyika vipande. Hii ni kawaida na inatokana na kuganda kwa damu kwenye ukuta wa kizazi. Hii ni kawaida kabisa na isikupe hofu. Damu hizi za kuganda zinaweza kuwa nyekundu sana, nyekundu mpauko au brown.

Hedhi nzito yenye weusi ama brown

Hii inaonesha kwamba kuna masalia ya damu ya zamani kwa hedhi iliyopita. Kubaki kwa damu husababishwa na flow ya polepole sana na mzunguko mdogo wa damu ndani ya mfuko wa mimba. Unaweza kurekebisha tatizo hili kwa kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha, kufanya masaji eneo la tumbo na pia unaweza kujaribu uterus cleansing package yetu.

Hedhi nyepesi ya majimaji

Pale unapoelekea kumaliza hedhi yako, unaweza kupata damu nyepesi sana na nyembamba. Damu hii inaweza kuwa nyeusi pia kutokana na mwingiliano wa hewa ya oksijen na damu.

Kama hedhi inatoka ni damu mbichi na nyekundu ya kung’aa. inaonesha inatoka moja kwa moja kwenye kizazi. Na inaweza kuashiria jeraha kwenye kizazi au pengine mimba kuharibika.

Nenda hospitali mapema endapo utaona damu mbichi na nyepesi ikitoka kwenye kizazi, hasa kama umepitisha hedhi kwa siku kadha,maana yake kuna uwezekano kulikuwa na mimba.Pia kama unatoa mabonge ya damu mfululizo na ni makubwa, hakikisha unaenda hospitali.

Je hedhi ya mabonge inaashiria nini??

Kutokwa na mapande ya damu kwenye hedhi mfululizo ni kitu hatari na inaashiria changamoto fulani ya kiafya. Hedhi nzito kisha inachukua zaidi ya siku 5 inaweza kuashiria dalili za

  • Vimbe kwenye kizazi (fibroids)
  • Kutanuka kwa kizazi (adenomysis)
  • Vimbe kwenye mayai (PCOS)
  • Saratani kwenye kizazi
  • Changamoto ya tezi ya shingoni (thyroid condition)
  • Majeraha kutokana na kitanzi
  • Upungufu wa vitamin K

Lini unatakiwa kumwona daktari?

Endapo unapata dalili ambazo hujazoea kweye hedhi yako, pamoja na dalili zinazokunyima uhuru, unatakuwa kumwona daktari dalili hizi ni pamoja na

  • Kukosa nguvu na kuishiwa pumzi kwenye hedhi-hii yaweza kuashiria upungufu wa damu
  • Maumivu na kutokwa damu kwenye sex
  • Mabonge ya damu makubwa
  • Kutumia zaidi ya pedi mja kwa lisaa
  • Hedhi ya maji maji ya kung’aa au kijivu
  • Kupata hedhi nyingi zaidi ya siku 7

Kwa maoni na ushauri tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254.

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Fahamu Kina cha Uke

kina sahihi cha uke wako
uke

Ni kipi kina cha uke ambacho ni sahihi?

Kuna imani potofu nyingi sana kuhusu maumbile, kina cha uke wako na namna ya kutunza afya ya uke. Baadhi ya watu wanafikiri uke ni mrefu kuelekea tumbo la chakula.

Kama na wewe umekuwa ukijiuliza maswali mengi kuhusu afya na maumbile ya uke wako, endelea kusoma makala hii utapata majibu yote.

1.Uke wako una urefu kiasi gani?

Uke wako siyo mrefu kihivyo kama unavowaza. Kikawaida urefu wa uke kuelekea ndani ni nchi tatu mpaka 6. Ni sawa na urefu wa mkono wako. Kina cha uke kinaweza pia kubadilika katika nyakati tofauti mfano wakati wa tendo la ndoa na kipindi cha kujifungua.

2.Je kina cha uke wako kinaongezeka ukiwa na hisia za kimapenzi?

Wakati wa tendo la ndoa, mwili huamshwa na hisia za mapenzi na hivo kupelekea kina cha uke kuongezeka ili kuruhusu uume kuingia vizuri.
Hisia za mapenzi hufanya shingo ya kizazi na kizazi kupanda juu kidogo na hio nafasi hiyo kuchukuliwa na uke.

Kama unahisi uume umeingia na unagusa shingo ya kizazi, inawezekana kabisa hujaandaliwa vizuri na haupo tayari kuingiziwa uume. Japo hii siyo sababu pekee ya kuguswa kizazi. Sababu ingine yaweza kuwa ni urefu kupita kiasi wa uume , zaidi ya inch 5.

Unataka kujifunza namna ya kupima urefu wa uume? bofya hapa kusoma zaidi

3.Uke unawezaje kutanuka wakati wa kuzaa?

Wakati wa kujifungua misuli ya uke wako inaweza kutanuka mpaka mwisho wake, kuruhusu mtoto kuzaliwa. Baadhi ya wanawake waliozaa kwa njia ya uke huona mabadilko. Mabadiliko kama kuhisi uke ni mpana kuliko kawaida baada ya kuzaa.

Baada ya kuzaa uke wako unatakiwa kurejea hali ya mwanzo baada ya siku chache. Japo uke uke wako hautarudi kwa asilimia mia kama mwanzo ila misuli itajikaza na utaweza tena kufurahia tendo.

4.Kuna haja ya kufanya mazoezi kukaza misuli ya uke?

Kadiri umri unazoenda, misuli ya uke wako itaanza kulegea kutokana na sababu mbali mbali kama

  • Kujifungua
  • Upasuaji
  • Kujikaza wakati wa kukohoa na kutoa choo
  • kuongezeka uzito

Mazoezi ya kegel yatakuzaidia kukaza misuli ya ndani ambayo inashikilia uke, kibofu, kizazi , na utumbo. Mazoezi ya kegel pia yatakusaidia kuongeza uwezo wa kubana mkojo na kuzuia kutokwa na mkojo na kinyesi bila kujitambua.

5.Je kisimi hubadilika ukubwa na kuvimba?

Jibu ni ndio! Unapokuwa kwenye hisia za mapenzi, kisimi chako ama kinembe huvimba na kuongezeka ukubwa. Hii ni kutokana na kuongezeka kwa mzunguko wa damu kuelekea kwenye via vya uzazi.

6.Je wanawake wote wanafanana maumbile ya uke?

Jibu ni hapana. Maumbile ya uke, mashavu ya uke, na urefu wa kuma unatofautiana kwa kila mwanamke. Uke wako unaweza kuwa mweusi kuliko maeneo mengine ya mwili, kisimi chako chaweza kuwa kidogo na hiyo ni kawaida, usijilinganishe na mwanamke mwingine.

7.Kwanini rangi ya ngozi chini kwenye uke ni nyeusi zaidi?

Ni kawaida kabisa kwa maeneo ya huko chini kuwa na rangi nyeusi zaidi kuliko maeneo mengine ya mwili. Mfano baadhi ya wanawake huwa na mashavu ya uke ya brown na wengi rangi nyeusi, wengine ya pink. Kama unahofu na rangi ya uke wako muone daktari mapema.

8.Je kuna faida yoyote ya mavuzi?

Kuwa na kutokuwa na nywele zehemu za siri hakuna athari yoyote kwa afya ya uke. Ila tu kuna changamoto unaweza kupata kwa kunyoa mavuzi kulingana na aina ya kifaa ulichotumia. Unaweza kupata muwasho na malengelenge.

9.Je ni salama kuosha uke mpaka ndani kwa maji?

Japo kitendo hichi ni maarufu sana kama kuflush uke au douching, madaktari wanapendekeza usijizoeshe kuosha uke kwa namna hii. Kuosha uke mpaka ndani kunaondoa na bakteria wazuri na hivo kukuweka katika hatari ya kutokwa na harufu mbaya na kuugua fangasi.

10.Je harufu ya uke inatofautiana kila siku kwenye mzunguko?

Najua waweza kuwa unashtuka sana na kupata hofu pale unapopata harufu fulani ukeni. Ni kawaida kabisa uke kuwa na harufu. Mfano unaweza kuona mabadiliko ya harufu baada ya kula samaki, tangawizi au kutumia virutibisho fulani.

Kama harufu ni mbaya sana na imekutoka kwa siku nyingi, harufu pengine inaabatana na uchafu wa kijani. Hapo muone daktari mapema. Dalili hizi zaweza kuashiria maambukizi ya bakteria na magonjwa ya zinaa

Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Bofya kusoma makala inayofuata: Faida na hasara za uzazi wa mpango

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Chanzo cha Maumivu ya Tumbo kwa Mjamzito

maumivu ya tumbo kwa mjamzito
mjamzito

Maumivu ya tumbo kwa mjamzito siyo jambo la kawaida hata kidogo.maumivu yanaweza kuwa ya haraka na kuisha ama yanaweza kuwa ya muda mrefu.

Ni muhimu kwa wewe mjamzito kujua kipi ni kawaida na kipi siyo cha kawaida wakati huu una mimba ili ujue muda gani umwone daktari kabla hujachelewa.

Maumivu ya Tumbo kwa Mjamzito kutokana na gesi nyingi

Gesi kwenye tumbo la chakula inaweza kuwa sababu ya tatizo lako. Maumivu yanaweza kuwa eneo moja ama yakasambaa kwenye kifua mpaka mgongoni. Tafiti zinasema kwamba wanawake wanapata gesi nyingi kwasababu ya kuongezeka kwa homoni ya progesterone kipindi hiki cha ujauzito.

Homoni hii inafanya misuli kulegea na hivo kupunguza kasi ya kutembea kwa chakula kwenye utumbo. Chakula kinachukua muda mrefu kuchakatwa na hivo kuzalisha gesi. Pia kadiri mimba inavokuwa kubwa inatengeneza mgandamizo kwenye utumbo na viungo vya karibu na hivo kuruhusu gesi kujikusaya.

Tiba Ya gesi Tumboni Kwa Mjamzito

Kama chanzo cha maumivu yako ya tumbo ni gesi nyingi tumboni, yatakiwa ubadili mtindo wa maisha. Jaribu kula kidogo kidogo katika siku. Usile milo mitatu mizito kama ambavo ulizoea mwanzo. Gawanya hata milo sita lakini midogo midogo.

Fanya mazoezi mepesi kama kutembea na yoga. Mazoezi yanachochea chakula kusagwa haraka na hivo kuzuia gesi kujikusanya. Punguza kula vyakula vilivyokaushwa kwa mafuta kama chips na vyakula kama mharage na kabeji ni chanzo cha gesi. Acha pia kunywa soda, jusi za viwandani na bia

Maumivu ya Maungio ya Nyonga hupeleka Maumivu ya Tumbo kwa Mjamzito

Eneo la nyonga linaweza kuuma kutokana na kutanuka ili kusapoti mtoto. Maumivu haya yanaweza kuwa ya haraka na kupita au yanaweza kuwa ya muda mrefu na kusambaa mpaka kwenye tumbo. Hali hii hutokea sana miezi minne ya mwisho kuelekea kujifungua.

Tiba ya Maumivu Ya nyonga

Kupunguza maumivu eneo la nyonga, jizoeshe kuamka taratibu ikiwa umetoka kulala ama ulikaa kwenye sofa/ kiti. Kama unajiskia kukohoa au kupiga chafya jikunye kidogo kwa magoti itasaidia kupunguza mgandamizo kwenye eneo la nyonga.

Fanya mazoezi ya yoga kila siku yatasaidia kunyoonya maungo ya mwili na kupunguza maumivu

Kukosa Choo Na Kupata Choo Kigumu(Constipation)

Hii ni adha mojawapo kubwa inawapata sana wajawazito wengi. Mabadiliko ya homoni, lishe, vidonge vya madini chuma na kukosa mazoezi ni chanzo cha mjamzito kukosa choo na kupelekea maumivu ya tumbo.

Tiba ya Constipation wakati wa ujauzito

Ongeza ulaji wa vyakula vya kambakamba kwenye lishe yako. Kunywa maji ya kutosha. Kula milo kidogo kidogo, usile mlo mkubwa kwa mara moja. Na usimeze vidonge vya kulanisha choo mpaka umeongea na daktari. Maana kumeza dawa ovyo yaweza kupelekea mimba kuharibika.

Sababu Zingine Za Maumivu ya Tumbo Kwa mjamzito

Maumivu ya tumbo inaweza kuwa ni ishara ya changamoto fulani kubwa ya kiafya kama

  • Mimba kuharibika
  • Mimba kutunga nje ya kizazi
  • Kukatika kwa kondo la nyuma
  • Kupanda kwa shiniko la damu kupita kiasi
  • Matatizo haya yote yanahitaji upate usaidizi wa hospitali haraka sana.

Matatizo mengine ya kiafya yanayoweza kupelekea uumwe tumbo, ambayo hayahusiani moja kwa moja na mimba ni pamoja na

Onana na Daktari mapema endapo maumivu yako ya tumbo yanaambatana na

  • Homa
  • Kutokwa na damu
  • Tumbo kubana na kuachia kama vile wajifungua
  • Kichefuchefu na kutapika
  • Maumivu wakati wa kukojoa

Bofya kusoma makala inayofuata kuhusu:Hamu ya tendo la ndoa kwa mjamzito

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Kupona Mapema Baada Ya Kujifungua Kwa Upasuaji

Kujifungua mtoto ni jambo la furaha sana kwa kila mwanmke aliyekuwa mjamzito. Maana mwisho wa siku unapata kiumbe chako baada ya kukibeba tumboni kwa shida miezi tisa yote. Kujifungua kwa uke kuna tofauti na kujifungua kwa upasuaji.

Pamoja na furaha yote lakini kumbuka kwamba kujifungua kunakuja na mzigo mwingine hasa mabadiliko ya mwili wako. Shepu itabadilika sana na utahitaji kuzoea tabia mpya. Kama umejifungua kwa upasuaji utahitaji mda nwingi zaidi wa kupumzika. Hapa chini ni

Hatua za tano za kukusaidia kupona mapema baada ya kujifungua kwa upasuaji

1.Pata Muda Zaidi Wa Kupumzika

Kama ilivyo kwa upasuaji mwingine, upasuaji wa kujifungua unataka upumzike zaidi ili kupona mapema. Baada ya kujifungua unaweza kukaa hospitali kwa siku 3 mpaka 5, na baada ya hapo itachukua mpaka week 6 kupona kabisa.

Hakikisha unalala kila wakati mtoto anapopata usingizi, maana akiamka atahitaji uwepo wako. Pata usaidizi kutoka kwa ndugu ama uwe na mfanyakazi(beki tatu) kwa ajili ya kumbeba mtoto na kubadilisha nguo, itakusaidia kupumzika zaidi

2.Usifanye Kazi Ngumu

Unapojifungua kwa upasuaji mwili unalegea na wahitaji matunzo kama ya mtoto mdogo. Usipandishe ngazi wala kuinua vitu vizito sana. Hakikisha kila kitu inachohitaji kwa haraka kama nepi, pampasi na chakula kipokaribu yako.

Usibebe kitu chochote kizito zaidi ya mtoto wako. Waambie ndugu wa karibu wakusaidie kubeba maji kupeleka bafuni na vitu vingine vizito. Unapotaka kukohoa au kupiga chanya basi hakikisha unashikilia tumbo lako ili kuulinda mshono.

Ongea na daktari akujulishe ni baada ya muda gani utaruusiwa kuanza kazi zako na pia mazoezi ili kutengeneza tena shepu yako.

3.Usianze mazoezi magumu haraka

Fanya mazoezi mepesi, kama kutembea kila siku kadiri utakavoweza. Pia usianze kufanya tendo mapema, subiri mpaka pale daktari atakapokuruhusu.

Usisahau pia kuwa makini na afya ya akili kama vile unavotunza mwili wako, tunza na hisia zako pia. Kuwa na mtoto mchanga itakupa hisia mbalimbali ikiwemo hasira za hapa na pale, uchovu na zingine. Zungumza na rafiki yako wa karibu namna unavojisikia au mshauri wa afya ya akili.

4.Tumia dawa za Maumivu inapobidi

Ongea na daktari kabla ya kumeza dawa pale maumivu yanapokuwa makali sana. Kumeza dawa kiholela kwa kipidi hii unaponyonyesha ni hatari.

Pata Lishe Ya Kutosha

Mlo kamili ni muhimu sana kwa kipindi hiki unaponyonyesha na unapouguza kidonda chako. Kumbuka kwamba mtoto wako anategemea sana chakula unachokula.

Hakikisha unakula aina nyingi za vyakula katika siku husika. Tafiti zinasema kwamba kutumia mboga za majani kwa wingi wakati wa kunyonyesha zinafanya ladha ya maziwa kwa mtoto kuwa nzuri na mtoto ufurahia zaidi anaponyonya. Pia muhimu kunywa maji ya kutosha ili usipate choo kigumu ama kukosa choo.

Lini Watakiwa Kumwona Daktari?

Wakati unajiuguza unaweza kupata hali ya kidonda kupata malengelenge na damu kutoa kidogo hiyo ni kawaida. Lakini ukiona dalili hizi hapa chini hakikisha unaenda hospitali haraka.

Dalili mbaya ni pamoja na

  • kidonda kuwa chekundu, kuvimba na kutoa usaha
  • maumivu makali sana eneo la kidonda
  • homa kali ya zaidi ya nyuzijoto 38
  • kutokwa na uchafu wenye harufu kali ukeni
  • kutokwa na damu nyingi ukeni
  • miguu kuvimba
  • kushindwa kupumua vizuri
  • maumivu ya kifua
  • maumivu kwenye eneo la matiti

Kama kuna ndugu au rafiki yako aliwahi kujifungua kwa upasuaji usijilinganishe nae katoka kupona kwako. Kila mwanamke ana mwili wa tofauti, wekeza nguvu na hisia zako katika afya yako itakusaidia kupona mapema.

Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Bofya kusoma makala inayofuata kuhusu: Maandalizi ya kujifungua kwa upasuaji