Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Tendo la ndoa Uncategorized

Nini kinatokea baada ya kupoteza bikira yako?

kupoteza bikira

Bikira ni kitu gani??

Tafsiri iliyozoeleka ya bikira ni mwanamke ambaye hajawahi kabisa kufanya tendo la ndoa katika maisha yake. Kwahivo mwanamke anapoingiliwa ukeni kwa mara ya kwanza anapoteza ile bikira yake.

Nini kinatokea mwilini baada ya kupoteza bikira?

Tendo la ngono laweza kupelekea mabadiliko mengi ya mwili. Hapa chini ni maelezo ya kinatokea

1.Mabadiliko ya ukeni

Watu wengi huamini kwamba tendo la ndoa linafanya uke kutanuka na kuwa mkubwa ama kulegea. Kumbuka uke unaweza kutanuka na kuzaa mtoto na kisha ukarudia hali yake ya mwanzo. Uume ni mdogo sana ukilinganisha na mtoto na hauwezi kufanya uke kulegea.

Kwa baadhi ya wanawake wanapoanza tendo hawapati raha, hasa kama uke wako ni mkavu naa hukuandaliwa vizuri. Hakikisha unafanya michezo mingine ya kutomasana kwa mda mrefu kabla ya kuanza tendo lenyewe.

2.Matiti

Kwa baadhi ya watu kufanya tendo kunaweza kupelekea matitti na chuchu kuvimba. Hii inatokea kwasababu zile hisia na muhemko wa kutaka kufanya tendo inapelekea mzunguko wa kasi wa damu kuelekea kwenye matiti, uke na uume pia.

3.Mabadiliko ya homoni

Wakati wa tendo ubongo unatoa vichocheo vingi sana kuelekea kwenye damu.Kazi ya vichocheo hivi ni kukufanya ujiskie raha ya tendo lenyewe na kuongeza upendo kati yako na mpenzi wako.

Je unaweza kushika mimba siku ya kwanza kufanya tendo?

Jibu ni ndio, unaweza kushika mimba siku ile tu ya kwanza kukutana na mwanaume. Mbegu tu zikiingia ndani ya uke unaweza kushika mimba. Kama hutaki kushika mimba mapema basi hakikisha unatumia condom muda wote wa tendo ama waweza kumeza p2.

Je ni umri gani sahihi wa wanawake wengi kupoteza bikira?

Wastani wa umri wa kupoteza bikira kwa wanawake wengi ni kati ya miaka 16 na 17. Katika umri wowote ule, kufanya tendo kwa mara ya kwanza ni jambo la tofauti sana na hisia zake zinatofautiana. Siyo kila mtu hufurahi tendo siku ya kwanza, wengi hupata maumivu na kuhisi kujuta. Na wengine hupata mawazo sana na hofu pengine wameshapata mimba au magonjwa ya zinaa

Jinsi ya kufanya tendo na kupoteza bikira bila maumivu

Hakuna njia moja ya kuondoa maumivu asilimia 100 siku ya kwanza unapofanya tendo, ila kuna vitu vichache vya kufanya kupunguza maumivu. Ukiwa na mpenzi asiye na haraka ya kuingiza uume, na pia awe mwelewa itakusaidia sana kufurahia tendo na kupunguza maimivu siku ya kwanza. Kuna mambo mengine mengi waweza kufanya yakakusaidia, endelea kuyasoma hapa chini

1.Ongea na mpenzi wako kabla ya tendo

Usiogope kuongea na mtu wako namna unavojiskia, vitu unavyoogopa na usichokipenda. Una kila haki ya kujieleza kwa uwazi ili akuvumilie. Kuongea na mwenzio kunasaidia kupunguza ile hofu ulokuwa nayo kuhusu kufanya mapenzi.

2.Fanya maandalizi ya kutosha

Hakika uke unaloa vizuri na kuwa mlaini sana kabla ya kuingiliwa na mwenzako hii inapunguza sana maumivu. Maandalizi haya ni pamoja na michezo kadhaa mkiwa uchi, kushikana sehemu za siri, kunyonyana uke na uume, na ndimi na kuambiana maneno matamu.

Chukueni walau nusu saa mpaka lisaa la maandalizi kabla ya tendo, msiende haraka.

3.Jaribu mikao na style tofauti za kufanya tendo

Kama unapata maumivu kwenye aina moja ya style ya kufanya tendo jaribu kubadili na utumie style zingine. Hizi ni baadhi ya style za kufanya tendo.

Style ya kwanza:Tumia mto chini ya mgongo na kukufanya ubinuke kidogo. Kunja magoti kisha chanua miguu yako ili uke ubaki wazi.

Style ya pili:Mwanamke kushika ukuta, na kubinuka kidogo kisha mwanamume anakunja kwa nyuma na kumuingilia ukeni

Style ya kifo cha mende: Hii ni nzuri kwa kuanzia, karibu kila mwanafunzi wa mapenzi anaanzia hapa: ukizoea hii style ya mwanamke kulala chini na mwanaume kuja kwa juu ndipo uanze kujaribu style zingine

4.Usijiwekee malengo makubwa kivile

Kutokana na kukua kwa teknoligia, lazima utakuwa umeshatazama picha na video za ngono namna watu wanavoingiza kwenye movie chafu za ngono. Na kwenye akili yako umeweka matazamio flani, kwamba unachokiona ndicho kitatokea utakapioanza mapenzi. Hii siyo kweli, wanaoigiza na kurekodi vidoe za ngono wanatumia madawa kuamsha hisia zao na ni wazoefu sana kufanya tendo.

Usijilinganishe nao, kuwa mpole na jipe muda, huwezi kuwa mzoefu kwa siku moja. Siku ya kwanza unaweza kushindwa kabisa kufanya tendo na baadae ukaweza. Hivo tuliza mihemko na ufanye taratibu

5.Hakikisha Eneo la kufanya tendo ni tulivu

Siku yako ya kwanza kufanya tendo inatakiwa kufanyika mahali pazuri pasio na kelele wala vitu hatari.Yatakiwa iwe sehemu ambapo wote wawili mke na mme mnatulia kiakili. Siyo kwenu vichaka au kwenye gari.

Kitanda ni sehemu nzuri zaidi ya kufanya tendo siku ya kwanza. Fanya usafi kwenye chumba chako na kuondoa kelele zozote. Hakikisha hakuna watu wengi eneo hilo na uzime simu. Unaweza kufungulia redio kwa mbali ili upate mziki wa kukusindikiza.

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Tendo la ndoa

Maumivu ukeni wakati wa tendo

maumivu ukeni wakati wa tendo

Tendo la ndoa ni moja na tukio tamu na la kufurahisha sana katika maisha ya mwandamu. Tendo linaimarisha ukaribu na upendo baina ya mke na mume. Pamoja na hayo ,watu wengi wanapata maumivu makali wakati wa tendo na hawafurahii kabisa. Kuna mambo mengi yanapelekea maumivu ukeni wakati wa tendo. Soma zaidi kujua nini cha kufanya kuondoa tatizo.

Maumivu kwenye tendo la ndoa ni kitu gani hasa?

Kitaalamu huitwa dyspareunia ni neno linalomaanisha maumivu ya via vya uzazi wakati wa tendo au baada ya tendo. Tatizo hili linawapata karibu asilimia 75 ya wanawake wote duniani.

Maumivu kwenye tendo yanaweza kuvuruga mahusiano, kukufanya ujihisi mpweke na huna thamani na kukosa kujiamini mbele ya mpenzi wako. Baadhi ya wanawake huamua kutojihusisha tena na tendo la ndoa baada ya kupata maumivu.

Pamoja na kwamba tatizo linatibika kwa kiasi kikubwa, watu wengi ni waoga sana kuelezea changamoto hii kwa kuogopa aibu ama kudharaulika.

Dalili za maumivu kwenye tendo

  • maumivu ya haraka
  • hali ya kuungua ukeni
  • kukosa hamu ya tendo
  • kushindwa kufika kileleni
  • maumivu ya tumbo

Je haya maumivu yanatokea ukeni tu?

Maumivu kwenye tendo yanatofautiana kwa kila mtu. Baadhi ya wanawake wanahisi maumivu wakati uume unaingia, na wengine wanapata maumivu wakiguswa tu kwenye via vya uzazi. Baadhi wanapata maumivu ya tendo baada ya kukoma hedhi.

Maumivu yanaweza kutokea

  • ndani ya ukeni
  • kwenye mashavu ya ukeni
  • chini ya mgongo
  • ndani ya kizazi
  • kwenye nyonga
  • tumboni chini ya kitovu na
  • kwenye ukuta unaotenganisha uke na mkundu

Baadhi ya wanawake wanapata maumivu baada tu ya kumaliza tendo, na wengine wakati wa kukojoa.

Nini kinapelekea maumivu kwenye tendo?

Baadhi ya sababu kubwa zinazopelekea mwanamke kupata maumivu ni pamoja na

1.Ukavu ukeni

Hii ni sababu kubwa zaidi ya maumivu kwenye tendo kutokana na kukosekana na ute ukeni na hivo msuguano kuwa mkubwa. Ukavu ukeni inatokea zaidi baada ya kukoma hedhi. Mabadiliko ya homoni yanapelekea kupungua kwa uzalishaji wa ute kwenye uke baada ya kukoma hedhi.

Sababu zingine zinazopelekea ukavu ukeni ni pamoja na kutumia njia za kisasa kupanga uzazi, kunyonyesha, stress na mwanamke kutoandaliwa vya kutosha.

2.Maambukizi

Maambukizi aina tofauti yanaweza kupelekea maumivu kwenye tendo. Maambukizi haya ni pamoja na

  • maambukizi ya bakteria ya ni bacterial vaginosis
  • fungus ukeni: dalili zake ikiwa ni pamoja na kutokwa uchafu unaoganda mzito, muwasho
  • kisonono
  • UTI kali
  • PID na
  • Chlaydia

Pia magonjwa mengine kwenye kizazi yanaweza kupelekea maumivu kwenye tendo. Magonjwa haya ni pamoja na

  • Endometriosis- yani ukuta wa ndani wa kizazi kuvimba
  • vaginismus: hii ni hali ya uke kugoma kuruhusu kitu chochote kuingia
  • Fibroids: Vimbe kwenye ukuta wa kizazi
  • Ovarian cyst: Vimbe kwenye mayai
  • Bartholin abscess: hizi ni vimbe kweye tezi za uke
  • Cervicitis: yani maambukizi kwenye mlango wa kizazi na kupelekea kuvimba kwake

Kumbuka magonjwa haya ni ngumu kwako kuyagundua ukiwa nyumbani. Ni mpaka kwenda hospitali, na kufanyiwa vipimo ndipo daktari atakwmabie endapo una uvimbe nk

Nini cha kufanya kuondoa maumivu?

Tiba ya tatizo inategemea na chanzo chake. Unapojiskia vibaya, hatua ya kwanza ni kwenda hospital na kuonana na daktari ili akusaidie kugundua chanzo cha tatizo.
Daktari atakuuliza baadhi ya maswali kujua historia ya tatizo, na aatapendekeza vipimo vya kufanyiwa.

Baada ya vipimo ndipo utapewa dawa sahihi ili uanze tena kufurahia tendo la ndoa.

Mawasiliano baina ya wapenzi

Mawasiliano ni nguzo muhimu sana kwenye mahusiano, itasaidia wapenzi kujuana kuhusu changamoto zao. Mpenzi wako ataweza kukuvumilia wakati unaendelea na tiba. Kumbuka kuendelea kufanya tendo wakati unapata maumivu ni mbaya, kwani itakuathiri kisaikolojia na kukfanya uchukue tendo la ndoa.

Kama chanzo cha tatizo ni ukavu ukeni, ni muhimu sana mtumie muda mwingi kwenye kuandaana.

Weka kwenye akili kwamba kutumia vilainishi vya kuganda kulainisha uke, yaweza kuleta madhara kwenye tishui laini za uke. Ni vizuri kutumia vilainishi vye maji maji pamoja na condom.

Kama maumivu unapata siku kadhaa tu, basi jaribu kubadili style ya kufanya mapenzi. Ongea na mwenzi wako akuingilie taratibu bila nguvu nyingi.

Lini unatakiwa kumwona daktari?

Muone daktari haraka endapo tatizo linajitokeza mara kwa mara, na maumivu yanazidi kila unapojaribu kufanya tendo. Pia kama unajihisi unaugua magonjwa kama fungus, unatokwa uchafu usio kawaida ana unapata maumivu ya tumbo muone daktari haraka.

Categories
Nguvu za Kiume Tendo la ndoa

Viagra,Matumizi, Faida na Madhara

viagra
viagra

Naamini umekuwa ukisikia hili neno kwa muda mrefu sana, pasipo kujua undani wa dawa hii ya viagra. Leo nitakweleza kwa undani kuhusu viagra, ikiwemo matumizi, upatikanaji, madhara yake ya mda mrefu na kitu gani waweza kutumia kama mbadala wa viagra.

Viagra ni kutu gani?

Endapo unawahi kufika kileleni ama unashindwa kusimamisha uume vizuri wakati wa tendo la ndoa. Ukienda hospitali, daktari anaweza kukuandikia utumie viagra. Hii ni dawa daktari anakwandikia kusaidia nguvu za kiume.

Viagra inakuja katika mfumo wa vidonge na hutakiwi kutumia mpaka uandikiwe na daktari, na utatumia kabla ya tendo siyo kila siku.

Viagra inafanyaje kazi?

Uume unasimama pale protini inayoitwa cyclic guanosine monophosphate(cGMP) inapotolewa kwenye damu, na kupelekea mzunguko mkubwa wa damu kuelekea kwenye uume. Mzunguko wa damu ukiwa mkubwa kuelekea kwenye uume hapo utaweza kudindisha vizuri na kupiga show mda mrefu bila kuchoka.

Je inachukua mda gani kwa Viagra kufanya kazi?

Viagra inaleta matokeo haraka sana baada tu ya kumeza dozi yako. Viagra inafanya kazi ndani ya lisaa. Kwa watu wachache inaweza kuanza kazi ndani ya nusu saa tu baada ya kumeza, na wengine mpaka baada ya masaa ma4.

Je vipi kama Viagra haitafanya kazi?

Endapo viagra haitafanya kazi, hakikisha unamjulisha daktari aliyekuhudumia. Daktari anaweza kupendekeza utumie dozi kubwa zaidi ya dawa, kisha ataendelea kukufatilia kama dozi hiyo kubwa imefanya kazi.

Je Nguvu a Viagra inaisha Ndani Ya Muda Gani?

Viagra inafanya kazi vizuri ndani ya masaa kadhaa baada ya kumeza. Kwa watu wengi dawa inafanya kazi ndani ya lisaa tu na kwa tu wachache dawa itaendelea kukupa nguvu mpaka masaa ma4. Kadiri mda unavosogea nguvu ya viagra inapungua na baadae kuisha. Hapo utahitaji kumeza tena ikiwa unataka kushiriki.

Kwahivo ieleweke hii siyo tiba ya tatizo lako. Ni booster tu ya mda mfupi ili ufurahie tendo, kisha utarudi kule kule.

Je Vigra inatumika Kwa Wanawake?

Pengine unajiuliza je mwanamke naye anatumia kuimarisha nguvu za kike? Dawa hii imethibitishwa kutumika kwa wanaume tu kwenye tatizo la uume kutosimama imara.

Je Kuna Matokeo/madhara Gani Kutumia Viagra?

Kama ilivo kwa dawa zingine zote, Viagra yaweza kuwa na madhara madogo na hata makubwa pia. Hapa chini ni list ya madhara yanayoweza kujitokeza. Kumbuka madhara haya yanatofautiana na umri wa mtu. Magonjwa mengine aliyonayo na pia dawa anazotumia kwa sasa.

Dalili/matokeo Ya Mda Mfupi

Dalili mbaya au matokeo yanaweza kujitokeza baada ya kumeza viagra ni pamoja na

  • kichwa kuuma
  • makamasi kwenye koo
  • maumivu chini ya mgongo na misuli
  • kizunguzungu
  • kiungulia na
  • mabadiliko kweneye kuona

Madhara Makubwa ya Viagra

Madhara makubwa yanaweza kujitokeza ukimeza viagra, ila usiogope, hayajitokezi mara kwa mara. ikiwa umepata matokeo haya, mweleze daktari mapema. Matokeo haya ni pamoja na

  • kushindwa kuona
  • kupata aleji
  • presha kushuka sana
  • kupata shambulizi la moyo
  • kupungua uwezo wa kusikia na pia
  • kuumia sana wakati wa kukojoa mbegu
  • uume kukosa nguvu kabisa kwenye tendo hasa ukitumia viagra kwa mda mrefu

Jinsi ya Kutumia Viagra

Kwasababu dawa unaandikiwa hospitali, ni lazima daktari, ni lazima akwandikie matumizi ya dawa. Muhimu sana kufatilia maelekezo uliopewa na daktari wako. Viagra zinapatikana wa nguvu za ujazo tofauti, yani mg 25, mg 50 na mg 100.

Muda gani unatakiwa kumeza viagra

Viagra inatakiwa kumezwa pale tu inapohitajika, yani lisaa limoja kabla ya kwenda kufanya ngono. Haitakiwi kumezwa mara kwa mara. Hutakiwi kabisa kumeza viagra zaidi ya mara moja kwa siku.

Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu viagra

1.Je viagra inaongeza hamu ya tendo la ndoa?

Jibu ni hapana, viagra haiongezi hamu ya tendo. Unatakuwa uwe na msisimko tayari wa kuifanya tendo ili viagra ifanye kazi . Kazi ya viagra ni kuongeza msukumo wa damu kuelekea kwenye uume ili usimame vizuri kwenye tendo.

2.Je viagra inazuia kumwaga mbegu? au kukufanya umwage mbegu mara nyingi zaidi?

inawezekana kabisa viagra kubadili mfumo wa utoaji mbegu kama ilivokuwa mwanzo/ mabadiliko haya ni pamoja na

  • kukuzuia kumwaga mbegu
  • kufanya umwage mbegu mara nyingi zaidi

Kama unapata changamoto baada ya kutumia viagra, ongea na daktari aliyekuhudumia.

3.Je Viagra inafanya uume uendelee kusimama hata baada ya kumwaga mbegu?

Ndio, viagra yaweza kukufanya uendelee kusimamisha hata baada ya kumwaga mbegu. Lakini endapo uume utasimama zaidi ya masaa ma4 muone daktari haraka. Hii inaweza kuwa hali ya hatari inayohitaji usaidizi wa haraka, maana itaharibu uume wako.

4.Je Viagra inaongeza ukubwa wa uume wako?

Hapana, ni ngumu sana viagra kuongeza ukubwa wa uume wako kuliko kawaida. Uume utavimba tu wakati una hisia za tendo, ukimaliza tendo uume unarudi kawaida. Viagra itafanya tu uume usimame na uwe imara kuliko kawaida ila siyo kuongeza maumbile.

Makundi ya watu wasiotakiwa kutumia Viagra

Viagra yaweza isikufae endapo una matatizo baadhi ya kiafya. Ongea na daktari vizuri na mweleze historia yako yote kabla hujaanza kumeza viagra. Magonjwa ama changamoto hizo ni pamoja na

  • magonjwaya moyo, stroke ama umefanyiwa upasuaji wa moyo ndani ya miezi 6
  • uume wako una maumbile yasiyo kawaida , mfano umejikunja sana, ama unapata mjeraha mara kwa mara.
  • Magonjwa ya damu kama sickle cell
  • magonjwa ya moyo
  • una presha ya kushuka
  • una changamoto za kutokwa damu mfano puani na kwingine kwenye matundu
  • vidonda vya tumbo: Hakikisha unamweleza daktari ikiwa unaumwa vidonda tumbo
  • magonjwa ya figo na ini: kama figo na ini zina hitilafu, kumeza dawa yaweza kuongeza sumu mwilini na kuleta shida zaidi.

Viagra Na Pombe

Kunywa viagra na huku unaendelea na pombe yaweza kuleta shida ya kupungua zaidi kwa presha ya damu. Kama wewe ni mnywaji wa pombe hakikisha unamjulisha daktari kuhusu hilo mapema.

Bofya kusoma kuhusu; Kwanini unawahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo

Categories
Tendo la ndoa

Tendo la Ndoa wakati wa Ujauzito

tendo la ndoa wakati wa ujauzito
mjamzito

Kama mwanamke unaweza kuwa unanjiuliza kama ni salama kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito ama siyo salama.

Pengine unafikiri yaweza kupekea mimba kuharibika? Au mtoto kupata majeraha? Pengine wajiuliza kuna staili fulani za tendo ambazo ni salama zaidi kwa mjamzito? Hapa chini ni taarifa muhimu ambazo watakiwa kuzifahamu.

Je Kufanya Tendo la Ndoa Wakati wa Ujamzito Ni Salama?

Jibu ni ndio, kufanya tendo wakati wa ujauzito ni salama kabisa. Uume kuingia ndani ya uke,zile pilika za kuingiza na kutoa haziwezi kuathiri mtoto, kwa sababu analindwa na tumbo na misuli ya ukuta wa kizazi pia.

Lakini pia mtoto analindwa na majimaji mazito(amniotic fluid).
Usijali kuhusu kusinyaa na kutanuka kwa uke pale unapofikia kilele, hakuwezi kufanya mimba ikatoka. Kutanuka huku ni tofauti na wakati wa kuzaa.

Mazingira gani inashauriwa usifanye tendo la ndoa wakati wa ujauzito?

Daktari anaweza kushauri usifanye tendo la ndoa kama

  • una historia ya mimba kuharibika mara kwa mara
  • uko kwenye hatari ya kupata uchungu mapema kabla ya week 37 za ujauzito
  • unatokwa na damu na maumivu yasijulikana sababu yake
  • chupa imepasuka na maji yanavuja
  • mlango wa kizazi umefunguka mapema zaidi
  • una tatizo kitaalamu placenta previa yani tishu za mirija unaomlisha mtoto chakula na hewa safi, umekuwa mpaka kuziba mlango wa kizazi
  • kama unatarajia kujifungua watoto mapacha

Je naruhusiwa kupiga punyeto badala ya tendo?

Fahamu kwamba daktari akishauri usifanye tendo anamanisha pia usifanye kitu chochote ambacho kinakuamsha hisia na kukufikisha kileleni mfano kutumia dildo an vidole/ kupiga punyeto.

Hamu ya Tendo la Ndoa wakati wa Ujauzito

Kila mwanamke mwanamke mjamzito anatofautiana namna anavojisikia kuhusu tendo. Baadhi hamu ya tendo hupotea kabisa. Wengine hufurahia zaidi tendo na kupata msisimko zaidi wa mapenzi wakati huu.

Kipindi cha ujauzito ni kawaida kwa hamu ya tendo kubadilika. Muhimu zungumza na mpenzi wako namna unavojisikia. Mueleze unapenda staili ipi nzuri ya kufanya tendo isiyokuumiza.

Staili za Kufanya Tendo Kwa Mjamzito

Baada ya miezi minne ya mimba,usifanye tendo kwa njia ya kawaida ya baba na mama kwa kulala kitandani na mme wako akaja kwa juu. Itakusaidia kuepuka changamoto za mzunguko wa damu..

Staili nzuri ya kufanya tendo ni kwa wote kulala kwa ubavu. Kisha mwanaume akaingiza uume kwenye uke kupitia nyuma yako na pia dogie style,yani mwanamke kupiga magoti na mwanamume kuingiza uume kwa nyuma.

Kama huna uhakika na mwanaume unayekutana nae kipindi hiki cha ujauzito basi hakikisha anavaa kondomu. Kuwa na mimba haizuii kutoambukizwa magonjwa ya zinaa kama ukimwi, kisonono na chlamydia-maana maambukizi haya huathiri mtoto moja kwa moja.

Tendo la Ndoa Baada Ya Kujifungua

Kwa week 6 za mwanzo baada ya kujifungua inashauriwa usifanye tendo la ndoa. Sababu zikiwa unahitaji:-

  • kupona kidonda wendapo njia ya uke ilikatwa kidogo kuongeza mlango wa mtoto kutoka
  • kupona kidonda cha tumbo endapo kama ulijifungua kwa upasuaji
  • uchovu kutokana na kujifungua
  • mabadiliko ya homoni yatapelekea ukose hamu ya tendo kwa muda
  • baaada ya kuzaa ni kawaida kuendelea kupata bleed kwa week 4 mpaka 6
  • Stress kutokana na kuwaza sana kuhusu majukumu mapya kama mzazi

Kwa ujumla tendo la ndoa lifanyike baada ya mama kupona kabisa. Ongea na daktari wako akupe ushauri lini itakuwa sawa. Kwa kiasi kikubwa week 6 zinafaa kusubiri kabla ya kuanza tena tendo la ndoa. Muhimu hakikisha tu una utulivu kihisia na kimwili kabla ya kuanza .

Bofya kusoma makala inayofuata: Bawasili kwa mjamzito, Ushauri na tiba