Categories
Uncategorized

Dalili za yai Kupevuka kwenye siku za hatari

yai kupevuka

Ikiwa unatafuta kushika mimba, kukwepa kushika mimba isiyotarajiwa au pengine unataka tu kuelewa mwenendo wa mwili wako, kuelewa mzunguko wako ni jambo la muhimu sana. Yai kupevuka kitaalamu tunaita ovulation. Ni kipindi kifupi sana lakini chenye matokeo makubwa kwa mwili wako.

Nini maana ya yai kupevuka?

Kwanza muhimu kujua ovulation ni nini? Ovulation ni kipindi katika mzunguko wa hedhi wa mwanamke ambapo yai lililokomaa linatolewa kwenye mfumo wa mayai(ovari), kwa ajili ya kufanyiwa urutubishaji na mimba ifanyike. Yai likishatolewa kwenye ovari, linaenda mpaka kwenye mrija wa uzazi, hapo yai linaweza kuishi mpaka saa 48. Endapo hakuna mbegu imerutubisha yai basi litavunjika na kutolewa nje.

Je ni Lini yai linapevuka kwenye mzunguko wa hedhi?

Hili ni swali zuri sana ambalo kila mwanamke huwa anajiuliza. yai linatolewa hasa baada ya siku 14 hedhi ilipoanza, kwa mzunguko wa siku 28.

Lakini muhimu ujue kwamba siyo kila mwanamke basi siku yake ya hatari ni ya 14. Wengine wana mzunguko mfupi zaidi mpaka siku 21 na wengine mizunguko mirefu mpaka siku 35. Endapo hujui mzunguko wako basi bofya makala hii (Jinsi ya kufatilia siku za hatari kwa mizunguko yote) usome kwanza kisha urudi kumalizia makala ya sasa.

Je ovulation inaisha baada ya masaa mangapi?

Mchakato mzima wa yai kutolewa inachukua masaa 36. Kitendo chenyewe cha yai kutoka kwenye ovari ni cha haraka, ispokuwa mabadiliko ya homoni kuelekea zoezi husika yanaanza mapema zaidi.

Ni zipi dalili za yai kupevuka?

Habari njema ni kwamba mwili wa mwanamke unatoa viashiria vingi kuonesha kwamba hizi ni siku za hatari na yai limevevuka tayari kwa kurutubishwa. Siyo kila mtu atapata dalili hizi zote, lakini lazima kuna dalili kadhaa utaziona endapo utausikiliza mwili vizuri. Kwahivo usijione mnyonge na kuhisi yai halijapevuka endapo utapata dalili chache katika hizi nitakazokuelezea leo.

1.Uteute wa kuvutika

Lazima utakuwa umewahi kusikia kuhusu ute wa uzazi ama ute wa ovulation, ama kuona uchafu mwembemba unaovutika kwenye chupi. Huu ndio ute unaoashiria kwamba yai limepevuka na litatolewa ndani ya masaa 24 tangu ute umeanza kutoka. Uteute huu unakuwa mwepesi kama yai, unavutika na hauna harufu.

2.Tumbo kujaa kipindi ya yai kupevuka

Yawezekana umewahi kuhisi tumbo kujaa katika siku flani katikati ya mzunguko wa hedhi na usijue kwanini. Mabadiliko ya homoni hasa kuongezeka kwa homoni la LH inaweza kufanya tumbo kubakiza maji na hivo kuvimba kiasi. Lakini usiogope sana hali hii ni ya masaa machache na utakuwa sawa.

3.Kichefuchefu kwenye siku za yai kupevuka

Unaweza kupata hali ya kuhisi kichefuchefu ukiwa kwenye siku ya ovulation, hii pia ni kutokana tu na mabadiliko ya homoni. Endapo utapata na hali hii, jaribu kutembea nje upate hewa safi na utafune tangawizi.

4.Mabadiliko ya joto la mwili kipindi cha cha yai kupevuka

Kwenye siku za hatari, hasa siku yenyewe yai linapotolewa, joto la mwili huongezeka kidogo kwa centigrade 0.3. Unaweza kununua kipimajoto pharmacy ukajipima mwenyewe nyumbani na kuona mbadiliko haya.

5.Maumivu ya tumbo upande mmoja, kutokwa na matone ya damu

Je wafahamu kwamba unaweza kupata maumivu kipindi cha yai kutolewa? Maumivu haya yanatokana na kitendo cha yai kutoka kwenye kikonyo chake ambacho ni mfumo wa mayai(ovari). Kitendo hiki pia chaweza kupelekea damu itoke kwenywe kovu na hivo ukaona matone kidogo kwenye chupi. Kuanzia sasa endapo utaona damu kidogo katikati ya mzunguko basi usiogope, jua tu kwamba ni yai linatolewa.

Ni muda gani sahihi kufanya tendo endapo unatafuta mimba kwa mda mrefu bila mafanikio?

Pengine sasa unajiuliza wewe na mwenzi wako mkutane lini ili kuongeza chansi ya kupata mimba haraka? Siku nzuri na yenye chansi kubwa kupata mimba ni siku ambapo yai limetolewa na masaa 24 yanayofuatia. Na pia siku 5 kabla ya yai kutolewa.

Kwanini siku 5 kabla? kwasababu mbegu zinaweza kuishi mpaka siku 5 kwenye kizazi baada ya kufanya tendo. Kwahivo kumbe mbegu zaweza kulisubiri yai litolewe hukohuko ndani.

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Tendo la ndoa Uncategorized

Nini kinatokea baada ya kupoteza bikira yako?

kupoteza bikira

Bikira ni kitu gani??

Tafsiri iliyozoeleka ya bikira ni mwanamke ambaye hajawahi kabisa kufanya tendo la ndoa katika maisha yake. Kwahivo mwanamke anapoingiliwa ukeni kwa mara ya kwanza anapoteza ile bikira yake.

Nini kinatokea mwilini baada ya kupoteza bikira?

Tendo la ngono laweza kupelekea mabadiliko mengi ya mwili. Hapa chini ni maelezo ya kinatokea

1.Mabadiliko ya ukeni

Watu wengi huamini kwamba tendo la ndoa linafanya uke kutanuka na kuwa mkubwa ama kulegea. Kumbuka uke unaweza kutanuka na kuzaa mtoto na kisha ukarudia hali yake ya mwanzo. Uume ni mdogo sana ukilinganisha na mtoto na hauwezi kufanya uke kulegea.

Kwa baadhi ya wanawake wanapoanza tendo hawapati raha, hasa kama uke wako ni mkavu naa hukuandaliwa vizuri. Hakikisha unafanya michezo mingine ya kutomasana kwa mda mrefu kabla ya kuanza tendo lenyewe.

2.Matiti

Kwa baadhi ya watu kufanya tendo kunaweza kupelekea matitti na chuchu kuvimba. Hii inatokea kwasababu zile hisia na muhemko wa kutaka kufanya tendo inapelekea mzunguko wa kasi wa damu kuelekea kwenye matiti, uke na uume pia.

3.Mabadiliko ya homoni

Wakati wa tendo ubongo unatoa vichocheo vingi sana kuelekea kwenye damu.Kazi ya vichocheo hivi ni kukufanya ujiskie raha ya tendo lenyewe na kuongeza upendo kati yako na mpenzi wako.

Je unaweza kushika mimba siku ya kwanza kufanya tendo?

Jibu ni ndio, unaweza kushika mimba siku ile tu ya kwanza kukutana na mwanaume. Mbegu tu zikiingia ndani ya uke unaweza kushika mimba. Kama hutaki kushika mimba mapema basi hakikisha unatumia condom muda wote wa tendo ama waweza kumeza p2.

Je ni umri gani sahihi wa wanawake wengi kupoteza bikira?

Wastani wa umri wa kupoteza bikira kwa wanawake wengi ni kati ya miaka 16 na 17. Katika umri wowote ule, kufanya tendo kwa mara ya kwanza ni jambo la tofauti sana na hisia zake zinatofautiana. Siyo kila mtu hufurahi tendo siku ya kwanza, wengi hupata maumivu na kuhisi kujuta. Na wengine hupata mawazo sana na hofu pengine wameshapata mimba au magonjwa ya zinaa

Jinsi ya kufanya tendo na kupoteza bikira bila maumivu

Hakuna njia moja ya kuondoa maumivu asilimia 100 siku ya kwanza unapofanya tendo, ila kuna vitu vichache vya kufanya kupunguza maumivu. Ukiwa na mpenzi asiye na haraka ya kuingiza uume, na pia awe mwelewa itakusaidia sana kufurahia tendo na kupunguza maimivu siku ya kwanza. Kuna mambo mengine mengi waweza kufanya yakakusaidia, endelea kuyasoma hapa chini

1.Ongea na mpenzi wako kabla ya tendo

Usiogope kuongea na mtu wako namna unavojiskia, vitu unavyoogopa na usichokipenda. Una kila haki ya kujieleza kwa uwazi ili akuvumilie. Kuongea na mwenzio kunasaidia kupunguza ile hofu ulokuwa nayo kuhusu kufanya mapenzi.

2.Fanya maandalizi ya kutosha

Hakika uke unaloa vizuri na kuwa mlaini sana kabla ya kuingiliwa na mwenzako hii inapunguza sana maumivu. Maandalizi haya ni pamoja na michezo kadhaa mkiwa uchi, kushikana sehemu za siri, kunyonyana uke na uume, na ndimi na kuambiana maneno matamu.

Chukueni walau nusu saa mpaka lisaa la maandalizi kabla ya tendo, msiende haraka.

3.Jaribu mikao na style tofauti za kufanya tendo

Kama unapata maumivu kwenye aina moja ya style ya kufanya tendo jaribu kubadili na utumie style zingine. Hizi ni baadhi ya style za kufanya tendo.

Style ya kwanza:Tumia mto chini ya mgongo na kukufanya ubinuke kidogo. Kunja magoti kisha chanua miguu yako ili uke ubaki wazi.

Style ya pili:Mwanamke kushika ukuta, na kubinuka kidogo kisha mwanamume anakunja kwa nyuma na kumuingilia ukeni

Style ya kifo cha mende: Hii ni nzuri kwa kuanzia, karibu kila mwanafunzi wa mapenzi anaanzia hapa: ukizoea hii style ya mwanamke kulala chini na mwanaume kuja kwa juu ndipo uanze kujaribu style zingine

4.Usijiwekee malengo makubwa kivile

Kutokana na kukua kwa teknoligia, lazima utakuwa umeshatazama picha na video za ngono namna watu wanavoingiza kwenye movie chafu za ngono. Na kwenye akili yako umeweka matazamio flani, kwamba unachokiona ndicho kitatokea utakapioanza mapenzi. Hii siyo kweli, wanaoigiza na kurekodi vidoe za ngono wanatumia madawa kuamsha hisia zao na ni wazoefu sana kufanya tendo.

Usijilinganishe nao, kuwa mpole na jipe muda, huwezi kuwa mzoefu kwa siku moja. Siku ya kwanza unaweza kushindwa kabisa kufanya tendo na baadae ukaweza. Hivo tuliza mihemko na ufanye taratibu

5.Hakikisha Eneo la kufanya tendo ni tulivu

Siku yako ya kwanza kufanya tendo inatakiwa kufanyika mahali pazuri pasio na kelele wala vitu hatari.Yatakiwa iwe sehemu ambapo wote wawili mke na mme mnatulia kiakili. Siyo kwenu vichaka au kwenye gari.

Kitanda ni sehemu nzuri zaidi ya kufanya tendo siku ya kwanza. Fanya usafi kwenye chumba chako na kuondoa kelele zozote. Hakikisha hakuna watu wengi eneo hilo na uzime simu. Unaweza kufungulia redio kwa mbali ili upate mziki wa kukusindikiza.

Categories
Uncategorized

Maumivu ya kichwa baada ya tendo

maumivu ya kichwa

Japo inatokea kwa watu wachache sana, unaweza kupata maumivu ya kichwa baada ya kufanya tendo hasa baada ya kufika kileleni. Maumivu haya yanaweza kuisha ndani ya dakika chache ama yakaendelea kwa zaidi ya masaa mawili.

Je maumivu ya kichwa baada ya tendo yakoje?

Maumivu haya (orgasim headache)yanaweza kuanza taratibu kwenye shingo na kichwa kadiri unapopandwa na hisia na kuongezeka kadiri msisimko watendo unavoongezeka. Au maumivu yanaweza kuja kwa haraka na makali sana kwenye eneo la mbele kuzunguka macho, pindi tu ukifika kileleni.

Karibu asilimia 75 ya watu wanaopata maumivu ya kichwa, wanasema yanatokea pande zote za kicha kulia na kushoto.

Je nini chanzo cha tatizo?

Madakatari wanafikiri kwamba maumivu ya kichwa ni kutokana na mishipa midogo ya damu kuvimba (vascular headache). Pale mtu akifika kileleni.

Pale mtu anapofika kileleni, presha ya damu hupanda juu kwa kasi. Kupanda huku kwa presha kunapelekea mishipa midogo ya damu ya kichwa kutanuka haraka na hivo kupelekea maumivu ya kichwa.

Vihatarishi vinavyopelekea maumivu ya kichwa kwenye tendo

Kila mtu anaweza kupata maumivu ya kichwa baada au wakati wa tendo. lakini tafiti zinasema kwamba chansi ya wanaume kupatwa na tatizo ni zaidi ya mara 4 kwa wanawake.

Pia watu walio kwenye umri wa kuanzia miaka 40 na kuendelea wapo kwenye hatari zaidi ya kukutwa na tatizo ukilinganisha na vijana wadogo.

Watu wenye historia ya kuumwa kichwa mara kwa mara kutokana na mwanga mkali au kikohozi pia wanaweza kuumwa kichwa kwenye tendo.

Je maumivu yanaisha kwa muda gani

Kwa kiasi kikubwa maumivu ya kichwa kwenye tendo huisha yenyewe ndani ya dakika chache. Baadhi ya watu hupatwa na maumivu haya mara moja na wengine hupatwa mfululizo katika week au mwezi.

Kama maumivu yatendelea zaidi ya lisaa na yanajirudia mara kwa mara, unatakiwa ummwone daktari. Matibabu ni pamoja na dawa za maumivu kama ibuprofen na dawa za kupunguza presha (beta blockers)

Maumivu ya kichwa baada ya tendo inaweza kuashiria uwepo wa changamoto kubwa ya kiafya. Kwa mazingira hayo unatakiwa kutibu chanzo cha tatizo kwanza.

Lini Unatakiwa Kumwona Daktari?

Siyo kila maumivu ya kichwa kwenye tendo ni ya kawaida. Daktari atakusaidia kujua kama tatizo ni la kawaida ama kuna chanzo kingine cha tatizo. Baadhi ya changamoto zinazoweza kupelelekea upate maumivu ya kichwa kwenye tendo ni pamoja na

  • Maambukizi ya bakteria, fungus au virusi
  • Magonjwa ya moyo
  • Kulegea kwa mshipa wa damu kwenye ubungo
  • Kupungua kwa njia ya mshipa wa damu safi kwenye ubongo
  • Kuvuja kwa damu ndani ya kichwa
  • Kiharusi
  • Matumizi ya baadhi ya dawa kama za kupanga uzazi

Maumivu yasiyo ya kawaida kwa kiasi kikubwa yanaambatana na dalili zingine kama

  • kichefuchefu
  • kutapika
  • shingo kukakamaa na
  • kupoteza fahamu

Watu wanaopata hizi dalili wanatakiwa kupelekwa hospitali haraka

Categories
Uncategorized

Kiwango cha mayai ya mwanamke

yai la mwanamke

Mwanamke ana mayai mangapi?

Natambua una kiu sana ya kutaka kufahamu idadi ya mayai uliyonayo, na kama bado una uwezo wa kushika mimba kulingana na umri wako wa sasa. Makala hii itajibu maswal yako mengi kuhusu mayai ya mwanamke na uzazi.

Je watoto wa kike wanazaliwa na mayai?

Jibu ni ndio, watoto wa kike huzalishwa na mayai yote wanayotakiwa kuwa nayo. Hakuna mayai mapya yatazalishwa tena kwenye maisha yako kama mwanamke.

Mayai mangapi mwanamke anazaliwa nayo?

Pale kichanga kinapokuwa bado tumboni mwa mama kinakuwa na mayai karibu millioni 6. Mayai haya yanakuwa hayajapevuka na huitwa oocytes. Mpaka kufikia kuzaliwa mayai yanapungua mpaka milioni 1 mpaka 2.

Kwanini mtoto mdogo hapati hedhi wakati tayari ana mayai?

Hili ni swali zuri sana, kwamba nini sasa kinazuia mtoto asianze hedhi wakati tayai ana mayai? Mzunguko wa hedhi husubiri mpaka kipindi cha kubalahe ama kuvunja ungo. Balehe huanza pale ubongo unapoanza kuzalisha homoni ya GnRH-Gonatrophin-releasing hormone.

GnRH inachochea tezi ya pitutary ambayo huzalisha homoni ya FSH-follicle stimulating hormone. FSH ndio inachochea sasa mayai kuanza kupevuka.

Hedhi huanza kama miaka miwili baada ya matiti kuota. Wanawake wengi huvunja ungo na kuanza hedhi wakiwa na miaka 12 mpaka 15. Wachache sana huvunja ungo mapema wakiwa na miaka 8.

Mwanamke ana mayai mangapi anapovunja ungo?

Pale mwanamke anapofikia balehe, anakuwa na idadi ya mayai laki 3 mpaka laki 4. je nini kimetokea kwenye mayai mengine? Hili ndio jibu sahihi:- ni kwamba mayai mengi karibu 10000 yanakufa kila mwezi kabla ya balehe, yaani hayafikii kwenye kupevuka.

Mayai mangapi yanakufa kila mwezi baada ya mwanamke kuvunja ungo?

habari njema ni kwamba idadi ya mayai uanayokufa kila mwezi inapungua sana baada ya kuvunja ungo. Tafiti zinasema kwamba mwanamke anapoteza mayai 1000 kila mwezi baada ya kuanza hedhi/kuvunja ungo. Hii ni kama kusema unapoteza asilimia 30 mpaka 35 ya mayai kila mwezi.

Kila mwezi ni yai moja tu linapevuka na kuwa tayari kwa mimba kutunga kwenye siku za hatari. Ni mara chache sana inatokea mayai mawili yakawa tayari kwa kurutubishwa. Hapo ndipo wanapatikana mapacha wasiofanana.

Mwanamke ana mayai mangapi kwenye miaka ya 30s?

Mwanamke anapofikia miaka 32 uwezo wake wa kushika mimba unapungua sana na unashuka zaidi anapofika 37. Kuanzia miaka 35 mpaka 37 mayai yanakuwa chini ya laki 1. Hii ni sawa na kusema mayai yamebaki asilimia 3 tu ya hifadhi yote.

Mayai mangapi yanabaki kwa mwanamke wa miaka 40?

Pengine uko na miaka 40 na bado una kiu ya kushika mimba. Sasa unawaza umebakiwa na mayai kiasi gani. Tafiti zinasema kwamba kikawaida mwanamke anapofika miaka 40, idadi ya mayai inapungua chini ya 18,000/=. japo chansi ya kushika mimba iko chini, haimaanishi kwamba huwezi kushika mimba, bado inawezekana kubeba ujauzito katika umri huu.

Nini kinatokea baada ya kukoma hedhi?

Pale unapokoma hedhi na mayai kuisha, mifuko ya mayai inakoma kuzalisha homoni ya estrogen. Na hivo utaanza kupata dalili za tofauti kama ukavu ukeni, uchovu, kukosa hamu ya tendo. Endapo ulizaliwa na mayai mengi, kuna chansi kubwa ukaweza kushika mimba na ukapata mtoto hata kwenye miaka ya 40s.

Hitimisho

Umri mzuri wa kubeba mimba na kuzaa ni miaka ya 20s. Hapo ndipo mwanamke anakuwa na mayai ya kutosha na chansi ya kushika mimba ni kubwa sana. Kama unatafuta mimba kwa muda mrefu bila mafanikio, inahitaji uonane na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake. Wote wawili me na ke mfanyiwe vipimo kujua chanzo cha tatizo.

Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Unataka kusafisha kizazi na kuongeza uzalishaji mayai? bofya hapa upate dawa asili zenye ubora