Categories
Ulaji mzuri na Afya ya Tumbo

Njia 7 za kulainisha choo

Kukosa choo na choo kigumu ni moja ya matatizo makubwa zaidi hapa kwetu. Kwani kila siku zaidi ya wagonjwa watano hunitafuta kwa shida hii. Pamoja na kwamba kuna dawa nyingi za kulainisha choo unazoweza kuzipata pharmacy, bado utakuwa hujasolve chanzo cha tatizo. Utaendelea kukosa choo na kupata choo kigumu baada tu ya kumaliza dawa zako.

Tiba na njia asli za kurekebisha mfumo wako wa chakula ndio suluhisho la kudumu. Njia hizi asili zinajumuisha vajula, mimea tiba na hata vitu unavyokunywa.

Mfumo wa ulaji ni tatizo

Dunia ya sasa imebadili mfumo wa ulaji na kutamnguliza biashara zaidi. makampuni makubwa ya kutengeneza vyakula yanashindana kupata faida na kufanya mauzo zaidi ya vyakula vyao, bila kuzingatia afya ya mlaji.

Miili yetu imeumbwa kwa namna ya kipekee sana ya kusafisha sumu, tunachotakiwa tu kuupa mwili malighafi stahiki na maji salama ili mtambo ufanye kazi. Muhimu sasa ujue kwanza chanzo cha tatizo lako kabla hujaanza kujitibia. Tuendelee..

Nini kinapelekea ukose choo na kupata choo kigumu?

Sababu hizi ndio chanzo cha tatizo lako

  • kula vyakula vya kusindikwa kiwandani visvyo na kambakamba
  • msongo wa mawazo
  • kukosa usingizi wa kutosha na
  • kutokunywa maji ya kutosha
  • kutoshugulisha mwili-mazoezi

Je Unatakiwa Kunya Mara ngapi kwa siku/wiki?

Wataalamu wengi wanapendekeza kwamba ni muhimu kwenda haja kubwa walau mara tatu au zaidi kwa wiki. Japo hili linatofautiana sana kwa kila mtu, kulingana na aina ya kazi anazofanya, chakula anachokula na hata mazingira aliyopo mtu huyu.

Kiujumla kama huendi kunya walau mara 3 kwa wiki, unatakiwa kufanya mabadiliko kwenye lishe yako na kutibu tatizo. Endelea kusoma kujua njia 10 zilizothibitishwa kukutibu choo kigumu.

Njia 7 za kulainisha choo na kukufanya upate choo kila siku

1.Kambakamba/fibers zinasaidia kulainisha choo

Hii ni hatua ya kwanza kabisa kwenye kurekebisha mfumo wako wa chakula. Anza kwa kuongeza vyakula vyenye kambakamba kwenye mlo wako kila siku. Na hakikisha unapata kambakamba hizi kutoka kwenye vyakula asili(ambavyo havijakobolewa na kusindikwa)

Matunda na mboga zenye kambakamba kwa wingi ni pamoja na

  • maparachichi
  • zabibu
  • bamia
  • spinach na

2.Kunywa maji ya kutosha

Kumbuka viungo vyako kama ini na figo vinahitaji maji mengi ili kusafisha damu, kuzalisha mkojo na kutoa taka mwilini.
Kama hutumii maji mengi, anza kubadili sasa ratiba yako, kunywa maji kila unapopata kiu, usinywe soda au pombe.

3.Tumia zaidi Vyakula vinavyoongeza bakteria wazuri tumboni

Kwenye tumbo kuna uwiano wa bakteria wazuri na wabaya. Endapo bakteria wabaya wataongezeka kupita kiasi, mazingira ya uchakataji chakula yatavurugika. Hapo taanza kupata dalili mbaya kama kukosa choo na choo kigumu, tumbo kujaa gesi na chakula kutosagwa vizuri.

Kuimarisha uwiano huo hakikisha unakula zaidi vyakula kama maziwa mtindi, chiaseed na flaxseed. Hakikisha tu unaoponunua maziwa, nunua yale asili. Achana na maziwa ya pakiti siyo salama kwako.

4.Aloe vera

Ukiniambia ni mmea gani utalainisha choo kwa haraka zaidi, nitakwambia ni Alo vera. Ni mmea unaotumika tangu miaka ya kale. Aloe vera pia inasaidia kupambana na vimelea wabaya, gesi tumboni na kuharakisha usagaji wa chakula.

Kwavile mmea wa aloe vera ni mchungu sana hakikisha unapata vidonge, ama juisi yake kutoka kwenye chanzo cha kuaminika. Unaweza pia kufika ofsini kwetu tukakupa vidonge vya aloevera.

5.Chia Seeds

chakula cha kulainisha choo

Moja ya faida ya chia seeds ni uwezo wake wa kufyonza maji kwenye mfumo wa chakula, na hivo kukuletea choo kilaini.

Chia seed zinatoa gram 10 za kambakamba kwa ujazo wa kijiko kimoja cha chakula. Muunganiko wake na majimaji unatengeneza jelly inafofanya choo kisukumwe kwa uzuri sana bila kutumia nguvu. Hakikisha unatumia vijiko vi3 kwa siku.
Matumizi: zioshe mbegu zako vizuri kisha ziloweke kwenye maji kwa nusu saa(vijiko viwili kwa ujazo wa kikombe kimoja cha chai). Tengeneza juis yako au salad, kisha weka chia seeds na blend pamoja.

6.Mboga za majani za kijani

Ukiacha kambakamba, mboga zilizokolea ukijani zina madini mengi ya magnesium. Magnesium ni madini muhimu kwenye kulainisha choo chako. Pasipo magnesium, ni ngumu kwa choo kusafiri kwenye mfumo wako.

7.Tui la nazi

Tui la nazi pamoja na maji ya madafu ni mazuri sana kwako wewe mwenye shida ya choo. Pamoja na utamu wake kutokana na sukari yake asili, maji haya yanalainisha choo kwasbaabu ya uwepo wa madini ya potasium ndani yake. Anza sasa kunywa maji ya mdafu na tui la nazi. Unaweza kuongeza viungo kama tangawizi, kisha ukachemsha kidogo tui pamoja na machicha kwa dakika 5 kabla ya kuchuja na kunywa.

Maelezo ya mwisho

Dawa za hospital za kulainisha choo siyo tiba kwako, ni suluhisho la mda mfupi tu, kisha unarudi kule kule. dawa hizi ukitumia mda mrefu zitavuruga mazingira ya tumbo na tatizo kuwa kubwa zaidi.

Baadhi ya vyakula na mimea tiba zitakusaidia kurekebisha mfumo wa ko wa chakula, bila dawa za pharmacy. Na njia hizi ni salama na zinapatikana sokoni tu.

Kurekebisha mfumo wa chakula siyo jambo la siku moja. inataka kujiwekea malengo ya mda mrefu na kufatilia kila siku. Ukishajijengea tabia ya kula vyakula asili usiache endelea nayo siku zote, hapo hautapata tena shida ya choo.

Muhimu kwa mgonjwa wa Choo kigumu

Wagonjwa wenye tatizo la mda mrefu zaidi ya wiki mbili tunawashauri kutumia tiba hizi asili kutibu tatizo haraka. Kwasababu usipopata tiba, itapelekea uugue magonjwa mengine mabaya kama bawasili.

Dozi moja tu inatosha kukupa matokeo mazuri ndani ya siku 3. Dawa ni Tsh 45,000/=

Tuandikie kwa Whatsapp number 0678626254 uanze dozi kwa Tsh 50,000/= tu.

Categories
Mifupa na Joints

Mifupa kusagika

mifupa kusagika

Mifupa kusagika kitaalamu tunaita osteoarthritis, ni ugonjwa uliopo kwenye kundi la degenerative disease. Haya ni magonjwa yanayosababishwa na kuchoka au kuharibika kwa muundo wa kiungo mpaka kupelekea kuzorota kwa ufanisi wake siku hadi siku.

Mifupa kusagika ama osteoarthritis inatokea zaidi mtu anavozeeka ama umri kwenda. Mabadiliko yanayopelekea mifupa kusagika yanatokea taratibu sana na yanaweza kuchukua miaka mingi mpaka kuleta athari. Japo katika mazingira flani hali yaweza kujitokeza katika umri mdogo.

Kuvimba na majeraha kwenye joint kunapelekea mabadiliko ya mifupa, kulegea na kuvunjika kwa maungio na hivo kupelekea maumivu na kuvimba kwa joint.

Kuna aina kuu mbili za mifupa kusagika (osteoarthritis)

Primary osteoarthritis ambayo inaathiri zaidi vidole, uti wa mgongo,hips, magoti na kidole gumba.
Secondary: hii inatokea kutokana na tatizo lililokwepo awali mfano jeraha la kujirudia, baridi yabisi kama gout na rheumatoid arthritis na magonjwa ya kurithi ya joints.

Nani anaweza kupata shida ya kusagika mifupa?

Karibu asilimia 80 ya watu wazima wenye umri zaidi ya miaka 55 wanapata osteoarthritis. Kati ya hawa, asilimia 60 wana dalili za mifupa kusagika. Na inakadiriwa kwamba zaidi watu milioni 240 duniani kote wana dalili za mifupa kusagika. Wanawake waliokoma hedhi wapo kwenye hatari zaidi kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa homoni ya estrogen.

Magonjwa au vitu gani hatarishi hupelekea mifupa kusagika?

Ukiacha swala la umri na magonjwa ya joints kama baridi yabisi, kuna mazingira na magonjwa yanayoongeza hatari ya kutokea kwa tatizo la mifupa kusagika. Fatilia maelezo yake kwa kina hapa chini.

1.Uzito mkubwa na kitambi: uzito mkubwa na kitambi unapelekea sana mifupa na jonits kusagika hasa eneo la magoti. Mwili unapokuwa mzito unaleta mgandamizo mkubwa eneo la joint na kupelekea tatizo. Ni muhimu kuweka sawa uzito wako ili upunguze hatari ya mifupa kusagika.

2.Kisukari na mafuta mengi. Kisukari na mafuta mengi kwenye mwili yanaongeza hatari ya kututumka ama kuvimba viungo vya ndani na kwenye joints na hivo kuongeza hatari ya mifupa kusagika. Kuongezeka kwa sukari kunapelekea sumu kuongezeka na kuleta hatari kwenye maungio.

3.Kupungua kwa homoni ya estrogen baada ya kukoma hedhi: Estrogen ni kichocheo ama homoni inayosaidia kulinda mifupa na maungio ya mifupa. Mwanamke anapofikia umri wa kukoma hedhi, kichocheo hiki kinapungua uzalishaji wake na hivo kuongeza hatari ya tatizo.

4.Magonjwa ya kurithi: Baadhi ya watu wanaweza kuugua magonjwa ya mifupa kwa kurithi kutoka kwa mababu. Hili ni ngumu kuepukika.

Je nitajuaje kama nina tatizo la mifupa kusagika?

Tofauti na magonjwa mengine ya joints, tatizo la osteoarthritis linaanza kukutafuna taratibu na kuchukua mika mingi mpaka kujionesha. Linaongezeka zaidi kutokana na kazi unazofanya na namna unavoshugulisha zaidi mwili kwako mfano kutembea na kukimbia. Hali ya maumivu na kuvimba kwenye maungio pia kunaongezeka siku hadi siku.

Kusagika kwa mifupa haisababishi wekundu kwenye kiungo kama ilivyo kwa baridi yabisi.

Unapoenda hospital daktari atachukua historia yako ya kuumwa na dalili unazopata. Anaweza kukufanyia kipimo cha X ray na MRI endapo ataona inafaa zaidi. Kama maungio yako yamejaa maji, daktari anaweza kuamua kufyonza maji yaliyopo .

Kwa ushauri na Tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Hedhi salama Menopause

Kukoma hedhi mapema

kukoma hedhi

Kukoma hedhi kitaalamu menopause ni kipindi katika ukuaji wa mawanamke ambapo damu ya kila mwezi inakata kutoka. Jambo hili hutokea hasa miaka ya 40 au wengine mpaka 50. Ni kipindi ambacho kinaambatana na mabadiliko mengine makubwa ya mwili ikiwemo kupungua hamu ya tendo, mashavu ya uke kusinyaa na mifupa kuwa dhaifu.

Kukoma hedhi mapema zaidi

Kwa wanawake wengi kukoma hedhi hata siyo jambo la kuliwazia mpaka pale utakapofikia miaka 40s au 50s. Japo mmoja kati ya wanawake 100 anaweza kukoma hedhi mapema zaidi akiwa na miaka 20s au 30s, kuliko ilivozoeleka.

Menopause inapoanza mapema zaidi kabla hujafikisha miaka 40, tunaita primary ovarian insufficiency au primary ovarian failure.

Kundi gani la wanawake wanaweza kukoma hedhi mapema zaidi?

Wakati unaanza kukoma hedhi, mifuko ya mayai yani ovary zinapunguza uzalishaji wa homoni za estrogen. Kukoma hedhi siyo kipindi kifupi, ni mlolongo wa miaka inaweza kuchukua hata miaka 5 au 10 kukoma kabisa hedhi. Utaanza kwa kukosa hedhi miezi mi3 mpaka 6 kisha baadae unakoma mwaka mzima.

Hichi kipindi cha kukosa hedhi ndicho chaweza kudumu mpaka miak 5 au 10 kabla hujakoma moja kwa moja.

Sababu nyingi zinaweza kupelekea mwanamke akome hedhi mapema kabla ya mda wake. Sababu hizi ni pamoja na

Dalili za kukoma hedhi mapema

Wanawake waliokoma hedhi mapema wanapata dalili za

Kumbuka siyo kawaida kwa mwanamke aliye kwenye umri wa kuzaa kupata dalili hizi, hivo hakikisha unamwona daktari mapema apate kupima homoni zako”

Daktari atahitaji kupima kiwango cha homoni ya estrogen na FSH kujiridhisha kama kweli umekoma hedhi.

Ushauri gani wa kuzingatia na Lishe ukiwa kwenye menopause?

Vyakula vya kutumia mara kwa mara ukishakoma hedhi

Unapojaribu kuekebiusha homoni zako zilizovurugika na kupunguza madhara ya menopause, lishe yako inatakiwa kujumuisha madini ya kutosha na mafuta mazuri. Unapokula lishe hii kwa wingi itakusaidia kuweka sawa homoni na pia kukupunguzia mafuta mabaya mwilini.

Weka akili kwamba kadri unavozeeka utahitaji kupunguza kiwango cha mlo wako kwasababu kasi ya shuguli za mwili inapungua na umri. Ni muhimu sana kujizuia vyakula vilivyosindikwa na kupendelea kula chakula safi. Vyakula vitakavyokusaidia ni pamoja na

1.Vyakula vyenye madini ya calcium kwa wingi

Mifupa kudhoofika ni moja na changamoto inayotokea baada ya kukoma hedhi. Japo mwanzoni huwezi kuona lakini madhara yake yanaweza kuonekana miaka ya baadae.

Mwili wako unajenga mifupa kuanzia ukiwa mdogo mpaka kufikia miaka 30. Baada ya hapo unaanza kupoteza mifupa. Kwa mwanamke kutokana na kupungua kwa homoni ya estrogen, kasi ya kumomonyoka mifupa inakuwa kubwa zaidi baada ya kukoma hedhi.

Ndiomaana tunashauri upendelee kula kwa wingi vyakula vyenye madini ya Calcium kama

  • maziwa
  • yogurt
  • mboga za majani za kijani kilichokolea na
  • dagaa
  • mboga zingine jamii ya kabeji kama broccoli, cauliflower na asparagus

2.Vyakula vyenye fiber/kambakamba kwa wingi

Vyakula vyenye kambakamba ni muhimu sana kwa afya ya moyo na mfumo wa chakula, pamoja na kuweka sawa uzito wako. Baadhi ya tafiti zinasema ulaji wa vyakula vya kamba kwa wingi unasaidia pia uzalishaji wa homoni ya estrogen. Homoni ambayo inapungua sana kwa walikoma hedhi.

Vyanzo vizuri vya kambakamba ni pamoja na karanga, parachichi, mbegu, maharage, nafaka, mbogamboga na matunda.

3.Mafuta yenye omega 3

Omega 3 ni kiambata kinachopatikana kwenye samaki na mbegu za maboga. Kiambata hiki kinasaidia kuimarisha moyo , kumarisha ngozi na kuzuia mwili kututumka . Mafuta haya yanapatikana zaidi kwenye samaki aina ya saladini na salmon. Tafiti zinasema kwamba kutumia omega 3 mara kwa mara kunasaidia uzalishaji wa homoni na kuzuia makali ya menopause.

4.Vyakula vya mafuta mazuri

Ni kweli kwamba vyakula vya mafuta havipandishi sukari kwenye damu ukilinganisha na vyakula vya sukari na wanga. Ndiomaana hata wenye uzito mkubwa na kitambi na wenye kisukari tunawashauri wale zaidi vyakula vya mafuta.

Pia vyakula hivi vinapunguza mpambano ndani ya mwili. Mafuta ndio yanayounda homoni zako mwilini. Hakikisha unapata mafuta mwali ambayo hayajachakachuliwa wala kuongezwa kemikali mbaya. Mafuta haya ni yale ya nazi, olive, vyakula kama nazi, parachichi, karanga ,ufuta na mbegu za maboga.

Kwa ushauri na Tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya uke Aina za Uchafu Ukeni

Uchafu wa njano ukeni maswali na majibu

uchafu wa njano ukeni
uchafu wa njano

Kutokana na sababu kadhaa, kutokwa na uchafu wa njano ukeni yaweza kuwa salama au hatarishi. Zifuatazo ni njia za kutambua kama uchafu wako ni salama ama ni kiashiria cha ugonjwa.

Aina za uchafu wa njano ukeni

Kutambua kama uchafu wako ni salama au hatari, unatakiwa kufatilia na kuzingatia baadhi ya mambo. Kuna aina nyingi sana za uchafu wa ukeni, hivo unahitaji kufatilia rangi, mwonekano, uzito na wepesi na harufu ya uchafu ili kujua kama watakiwa umwone daktari.

Kama uchafu wako wa njano hauna harufu kwa kiasi kikubwa huhitaji kumwona daktari. Uchafu wenye harufu unaweza kuashiria mamabukizi flani. Na kama uchafu wako unanuka, tambua kwamba ile rangi ya njano ni kiashiria cha aina ya maambukizi husika.

Uchafu mwepesi wa njano usiokolea na ambao hauna harufu wala dalili zozote mbaya kama maumivu ya tumbo, maumivu kwenye uke au muwasho, hapo hakuna tatizo ni uchafu wa kawaida.

Njano iliyokolea na uchafu mzito, ukiwa unaambatana na harufu mbaya, huu ni uchafu usio kawaida na unaashiria maambukizi.

Je ni kawaida mwanamke kupata uchafu wa njano ukeni?

Katika baadhi ya mazingira ni kawaida kupata uchafu wa njano. Siku chache baada ya hedhi unaweza kuona ute wa njano kama cream au unaonata.

Utakapokarbia hedhi, uchafu waweza kuwa mweusi kutokana na vipande vya damu kujichanganya na uchafu wa ukeni.

Kadiri hedhi inavokaribia kuisha rangi ya damu inabadilika kutoka kuwa nyekundu na kuwa brown na baadae kuwa na unjano. Huu uchafu wa njano ni masalia ya hedhi ya mwisho iliyobaki kwenye kizazi.

Uchafu wa njano ukeni ni wa kawaida endapo haujaambatana na harufu mbaya, muwasho, maumivu chini ya kitovu, maumivu kwenye tendo na maumivu wakati wa kukojoa.

Kama uchafu wa njano unanuka na kuna muwasho nini chanzo??

1.Maambukizi ya fungus -yeast infection

Uke wako unatakiwa kuwa na uwiano sawa wa vimelea na utindikali pia. Pale inapotokea mazingira yakavurugika, bakteria na fungus huanza kukua kupita kiasi na kukufanya uumwe. Kufanya tendo la ndoa na watu wengi, kutumia antibiotic mara kwa mara, kuosha uke mpaka ndani na kuvurugika kwa homoni inaweza kuvuruga mazingira ya uke.

Fungus ukeni, ni ugonjwa unatokea sana kwa wanawake wengi. Ugonjwa unatokea pale vimelea wa fungus wanapokua kupita kiasi.

Dalili kubwa za fangas ukeni ni pamoja na

  • muwasho kwenye mashavu ya uke
  • kuvimba kwa mashavu ya uke
  • maumivu wakati wa tendo
  • maumivu na hali ya kuungua wakati wa kukojoa
  • uke kuuma na kuvimba
  • uchafu mweupe wa kuganda kama mtindi

2.Ugonjwa wa Trichomoniasis

Ni ugonjwa unaotibika na unaambukiwa kupitia zinaa. Watu wengi waliathiriwa na ugonjwa huu hawakujua kama wameshaambukiwa sababu dalili huwa zinachelewa kujionesha.

dalili za trichomoniasis ni pamoja na

uchafu wa njano au kijani wenye harufu mbaya
kuvimba kwa mashavu ya uke na uke wote
kuhisi haja ndogo mara kwa mara
maumivu wakati wa tendo la ndoa na
maumivu wakati wa kukojoa

Ugonjwa unatibika kupitia antibiotics, endapo utapimwa na kugundilika na ugonjwa hakikisha unampeleka na mpenzi wako kupimwa.

3.Kisonono na Chlamydia

Magonjwa haya yote yanaabukizwa kwa zinaa. Magonjwa haya yanatibika kupitia antibiotics endapo utaanza tiba mapema. Kama hautapata tiba mapema, yaweza kupelekea upate PID, mirija kuziba na maumivu makali ya nyonga kutokana na makovu kwenye kizazi.

Ndiomaana ni muhimu sana kupima magonjwa ya zinaa mara kwa mara, hasa kama una wapenzi wengi au kama umekutana bila kinga na mpenzi mpya.

Dalili kubwa za chlamydia na kisonono ni pamoja na

  • kuongezeka kwa kiwango cha uchafu ukeni
  • maumivu wakati wa kukojoa na kwenye tendo
  • kutokwa na bleed katikati ya mzunguko
  • maumivu makali ya nyonga

4.PID

Pid ni kifupi cha pelvic inlafammatory disease. Ni athari kwenye via vya uzazi kwa mwanamke, na inatokea pale magonjwa kama chlamydia na kisonono yasipotibiwa vizuri na kuisha mpaka kusambaa kwenye mirija, na mayai. Aina nyingi za maambukizi ya bakteria zaweza kupelekea uugue PID.

Endapo PID haitatibiwa vizuri yaweza kupelekea changamoto kama mimba kutunga nje ya kizazi, mimba kuharibika na maumivu makali ya nyonga.

Dalili za PID ni pamoja na

  • uchafu wa njano au kijani ukeni wenye harufu mbaya
  • hedhi kuvurugika
  • maumivu wakati wa tendo
  • maumivu wakati wa kukojoa
  • kutokwa damu wakati na baada ya tendo
  • kuhisi homa na kichefuchefu

Uchafu wa njano wakati wa ujauzito

Mimba inakuja na mabadiliko mengi sana kutokana na kuongezeka kwa baadhi ya homoni. Wajawazito wengi wanashuhudia ongezeko la uchafu unaotoka ukeni kutokana na kuongezeka kwa homoni za estrogen na progesterone.

Kama unapata uchafu mweupe , mwembamba usio na harufu mbaya hiyo ni kawaida. Kitaalamu uchafu unaitwa leukorrhea.

Kama utaona uchafu wa kijani au njano wenye harufu mbaya, hiyo yaweza kuashiria maambukizi. Wajawazito wanaugua sana fungus ukeni. Unatakiwa kwenda hospital mapema upate vipimo na dawa.

Endapo hujatibiwa fungus au magonjwa ya zinaa, inaweza kuhatarisha afya ya mtoto wakati anazaliwa. Maana mtoto anaweza kupata maambukizi.

Mwisho kabisa

Kama wewe ni mwanamke, ujue kwamba lazima utakutana na changamoto nyingi kwenye uke wako hasa wala la uchafu ukeni. Ni muhimu sana kujielimisha na kujua uchafu upi ni hatari na upi ni salama ili umwone daktari mapema.

Kwa ushauri na tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Tendo la ndoa

Maumivu ukeni wakati wa tendo

maumivu ukeni wakati wa tendo

Tendo la ndoa ni moja na tukio tamu na la kufurahisha sana katika maisha ya mwandamu. Tendo linaimarisha ukaribu na upendo baina ya mke na mume. Pamoja na hayo ,watu wengi wanapata maumivu makali wakati wa tendo na hawafurahii kabisa. Kuna mambo mengi yanapelekea maumivu ukeni wakati wa tendo. Soma zaidi kujua nini cha kufanya kuondoa tatizo.

Maumivu kwenye tendo la ndoa ni kitu gani hasa?

Kitaalamu huitwa dyspareunia ni neno linalomaanisha maumivu ya via vya uzazi wakati wa tendo au baada ya tendo. Tatizo hili linawapata karibu asilimia 75 ya wanawake wote duniani.

Maumivu kwenye tendo yanaweza kuvuruga mahusiano, kukufanya ujihisi mpweke na huna thamani na kukosa kujiamini mbele ya mpenzi wako. Baadhi ya wanawake huamua kutojihusisha tena na tendo la ndoa baada ya kupata maumivu.

Pamoja na kwamba tatizo linatibika kwa kiasi kikubwa, watu wengi ni waoga sana kuelezea changamoto hii kwa kuogopa aibu ama kudharaulika.

Dalili za maumivu kwenye tendo

  • maumivu ya haraka
  • hali ya kuungua ukeni
  • kukosa hamu ya tendo
  • kushindwa kufika kileleni
  • maumivu ya tumbo

Je haya maumivu yanatokea ukeni tu?

Maumivu kwenye tendo yanatofautiana kwa kila mtu. Baadhi ya wanawake wanahisi maumivu wakati uume unaingia, na wengine wanapata maumivu wakiguswa tu kwenye via vya uzazi. Baadhi wanapata maumivu ya tendo baada ya kukoma hedhi.

Maumivu yanaweza kutokea

  • ndani ya ukeni
  • kwenye mashavu ya ukeni
  • chini ya mgongo
  • ndani ya kizazi
  • kwenye nyonga
  • tumboni chini ya kitovu na
  • kwenye ukuta unaotenganisha uke na mkundu

Baadhi ya wanawake wanapata maumivu baada tu ya kumaliza tendo, na wengine wakati wa kukojoa.

Nini kinapelekea maumivu kwenye tendo?

Baadhi ya sababu kubwa zinazopelekea mwanamke kupata maumivu ni pamoja na

1.Ukavu ukeni

Hii ni sababu kubwa zaidi ya maumivu kwenye tendo kutokana na kukosekana na ute ukeni na hivo msuguano kuwa mkubwa. Ukavu ukeni inatokea zaidi baada ya kukoma hedhi. Mabadiliko ya homoni yanapelekea kupungua kwa uzalishaji wa ute kwenye uke baada ya kukoma hedhi.

Sababu zingine zinazopelekea ukavu ukeni ni pamoja na kutumia njia za kisasa kupanga uzazi, kunyonyesha, stress na mwanamke kutoandaliwa vya kutosha.

2.Maambukizi

Maambukizi aina tofauti yanaweza kupelekea maumivu kwenye tendo. Maambukizi haya ni pamoja na

  • maambukizi ya bakteria ya ni bacterial vaginosis
  • fungus ukeni: dalili zake ikiwa ni pamoja na kutokwa uchafu unaoganda mzito, muwasho
  • kisonono
  • UTI kali
  • PID na
  • Chlaydia

Pia magonjwa mengine kwenye kizazi yanaweza kupelekea maumivu kwenye tendo. Magonjwa haya ni pamoja na

  • Endometriosis- yani ukuta wa ndani wa kizazi kuvimba
  • vaginismus: hii ni hali ya uke kugoma kuruhusu kitu chochote kuingia
  • Fibroids: Vimbe kwenye ukuta wa kizazi
  • Ovarian cyst: Vimbe kwenye mayai
  • Bartholin abscess: hizi ni vimbe kweye tezi za uke
  • Cervicitis: yani maambukizi kwenye mlango wa kizazi na kupelekea kuvimba kwake

Kumbuka magonjwa haya ni ngumu kwako kuyagundua ukiwa nyumbani. Ni mpaka kwenda hospitali, na kufanyiwa vipimo ndipo daktari atakwmabie endapo una uvimbe nk

Nini cha kufanya kuondoa maumivu?

Tiba ya tatizo inategemea na chanzo chake. Unapojiskia vibaya, hatua ya kwanza ni kwenda hospital na kuonana na daktari ili akusaidie kugundua chanzo cha tatizo.
Daktari atakuuliza baadhi ya maswali kujua historia ya tatizo, na aatapendekeza vipimo vya kufanyiwa.

Baada ya vipimo ndipo utapewa dawa sahihi ili uanze tena kufurahia tendo la ndoa.

Mawasiliano baina ya wapenzi

Mawasiliano ni nguzo muhimu sana kwenye mahusiano, itasaidia wapenzi kujuana kuhusu changamoto zao. Mpenzi wako ataweza kukuvumilia wakati unaendelea na tiba. Kumbuka kuendelea kufanya tendo wakati unapata maumivu ni mbaya, kwani itakuathiri kisaikolojia na kukfanya uchukue tendo la ndoa.

Kama chanzo cha tatizo ni ukavu ukeni, ni muhimu sana mtumie muda mwingi kwenye kuandaana.

Weka kwenye akili kwamba kutumia vilainishi vya kuganda kulainisha uke, yaweza kuleta madhara kwenye tishui laini za uke. Ni vizuri kutumia vilainishi vye maji maji pamoja na condom.

Kama maumivu unapata siku kadhaa tu, basi jaribu kubadili style ya kufanya mapenzi. Ongea na mwenzi wako akuingilie taratibu bila nguvu nyingi.

Lini unatakiwa kumwona daktari?

Muone daktari haraka endapo tatizo linajitokeza mara kwa mara, na maumivu yanazidi kila unapojaribu kufanya tendo. Pia kama unajihisi unaugua magonjwa kama fungus, unatokwa uchafu usio kawaida ana unapata maumivu ya tumbo muone daktari haraka.

Kwa ushauri na Tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254