Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Kisukari cha mimba na hatua za kupunguza Tatizo

kisukari cha mimba

Bilashaka umewahi kusikia kuhusu kisukari cha mimba. Kama una maswali zaidi kuhusu tatizo hili na unataka kujua nini cha kufanya kupunguza hatari basi makala hii ndio kila kitu kwako.

Nini maana ya kisukari ha mimba yani Gestational diabetes?

Okey hiki ni kisukari anachopata mjamzito pale ambapo kiwango cha sukari kwenye damu kinapanda sana , na mwili wako hauzalishi insulini ya kutosha kupunguza ile sukari.

Kuna makundi mawili ya kisukari ya mimba. Kundi la kwanza tuite class 1 hii inaweza kudhibitiwa kwa kurekebisha tu vyakula na mtindo wa maisha, na kundi la pili tuite class 2 hii itahitaji upate matibabu ya dawa hospitali.

Ukicha kile kisukari ha ukubwani ambacho wanaugua watu wengi, hiki kisukari cha mimba kinampata mtu pale tu akiwa mjamzito na kwa wanawake wengi wanapona baada ya kujiungua.
lakini tafiti inaonesha pia kwamba unakuwa kwenye hatarri ya kuugua kisukari cha ukubwani pale ukiwa na kisukari cha mimba.

Je nini kinapalekea mwanamke kuugua kisukari cha mimba?

Wakati a mimba, kondo yani placenta inaweza kuzalisha vichocheo ambavyo vinapeleka sukari kuwa nyingi kwenye damu na kupelekea kiasukari cha mimba. Baada ya mtoto kuzalishwa na kondo kutolewa sukari inarudi kawaida.

Dalili za kisukari cha mimba

Kisukari ha mimba gestational diabetes chaweza kupelekea dalili kama

  • mdomo kukauka
  • kukojoa mara kwa mara
  • kuhisi mwili kuchoka sana
  • kuhisi kiu kuliko kawaida

Je tatizo ni kubwa kiasi gani??

Japo kiwango cha wanawake wanaogundulika kuwa na kisukari cha mimba ni ndogo, karibu 10% ya wanawake duniani wanapata shida hii kwa mwaka.
Madaktari pia wanajua kwamba baadhi ya sababu zinachangia kuwa kwenye hatari zaidi kama

Umri: Tafiti zinasema wanawake wenye zaidi ya miaka 30 wanapata zaidi tatizo.
Uzito: Wenye uzito mkubwa na kitambi wapo kwenye hatari mara 3 ya kuugua.
Historia kwenye familia: Kama kwenye familia yako kuliwahi kutokea wagonjwa wenye kisukari cha mimba, basi na wewe utakuwa kwenye hatari ya kupata shida hii.

Je lini unatakiwa kupima kujua kama una kisukari cha mimba?

Kipimo kwa kiasi kikubwa kinafanyika kati ya wiki ya 24 mpaka 28 kwenye mimba. Wajawazito waliopo kwenye kundi hatarishi ama wenye historia ya tatizo wao hupimwa mapema zaidi kwenye miezi mi3 ya kwanza.

Je nini ufanye ikiwa utajikuta unaumwa yani +ve?

Kama utakutwa na kisukari, usipaniki. Daktari wako atakuwa nawe bega kwa bega kuhakikisha unapata matibabu na ushauri sahihi kwa tatizo lako. Kumbuka unaweza kupona kwa lishe na maoeiz tu ndani ya muda mfupi. Hakikisha unauliza maswali yote ukiwa na daktari ili upate ufafanuzi wa kina.

Utaelekezwa kufatilia sukari yako kila siku kwa kupima. Kama sukari yako haiwezi kutibika kwa lishe na mazoezi, hapo utaweza kuanzishiwa dawa ambao ni salama kwa ujauzito wako.

Yapi madhaar ya Kisukari cha mimba?

Kisukari cha mimba chaweza kupekea matatizo kadhaa kama kuzaa mapema kabla ya mda, kujifungua mtoto mwenye uzito mkubwa zaidi kuliko kawaida na pia yaweza kuhitaji ujifungue kwa upasuaji. Hutakiwi kuogopa wanawake wengi wanapata hili tatio linaisha baada ya kuzaa na wanaendelea na maisha yao.

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Malezi ya Mtoto na Kunyonyesha

Chanzo cha Mama kukosa Maziwa baada ya Kujifungua na Tiba

mama kukosa maziwa baada ya kujifungua

Pale unapojifungua kuna vitu unatagemea na kutakiwa kuzingatia, kuanzia kwenye mikao ya kunyonyesha, kumlaza mtoto na usafi wa mtoto. Mama kukosa maziwa baada ya kujifungua ni mtihani mkubwa sana kwa mwanamke anapojifungua. Leo utasoma kwanini maziwa yanatoka kidogo na nini cha kufanya ili kuongeza maziwa.

Je utajuaje maziwa yanyotoka ni kidogo na hayatoshi kwa mtoto?

Kama unanyonyesha mtoto kwa chupa ni rahisi kujua kiwango gani anatumia kwa siku. Lakini kama unanyonyesha kikawaida ni ngumu kujua mtoto anameza kiwango gani cha maziwa, kwahivo unatakiwa kujua viashiria vingine vya mtoto kushiba.

Mama kukosa maziwa nyakati za usiku

Wamama wengi hawanyonyeshi usiku, hasa kwaavile wanakuwa wamechoka na wanahitaji kupumzisha miili yao. Kwahivo kiwango cha homoni ya prolatin kitashuka na kupelekea maziwa kuzalishwa kidogo hata nyakati zingine. Prolactin ni kichocheo ambacho kinachochea maziwa yazalishwe mengi ili mtoto anyonye vizuri. Pia maziwa ya usiku yanakuwa na kiwango kikubwa cha mafuta mazuri ambayo ni muhimu kwa ukuaji wa mtoto.

Mama kukosa maziwa baada ya kujifungua: Dalili za kuoenesha maziwa yapo ya kutosha

Tatizo hili la mama kukosa maziwa linawapata watu wachahe sana. Hapa chini ni dalili za kukuonesha maziwa ya mtoto yapo mengi na yanatosheleza

Uzito wa mtoto haupungui na kuongezeka. Ni kawaida kwa mtoto kupoteza asilimia 5 mpaka 7 ya uzito kwenye siku za mwanzoni. Lakini uzito unatakiwa kurudia hali ya kuzaliwa ndani ya siku 10 mpaka 14.

  1. Mashavu ya mtoto yanaonesha yametuna wakati ananyonya
  2. Mtoto kupata choo mara tatu kwa siku katika siku za mwanzo baada ya kujifungua
  3. Mtoto haoneshi dalili yoyote ya kuishiwa maji, dalili kama kulia sana, mkojo mwekundu, mdomo mkavu na macho kuingia ndani
  4. Endapo mtoto ni mtulivu wakati wa kunyonya na anaachia nyonyo yeye mwenyewe baada ya kushiba
  5. Matiti yanaonekana laini sana baada ya kunyonyesha. Kabla ya kunyonyesha maziwa yanakuwa yamejaa na yakipungua maziwa yanakuwa laini na kunywea
  6. Mtoto anaonekana kumeza wakati huo ananyonya

Nini kinapelekea mama kukosa maziwa baada ya kujifungua?

Kuna sababu nyingi kwanini umejifungua hivi karibuni na maziwa ni kidogo sana au hayatoki kabisa. Baadhi ya sababu ni hizi

  • Matumizi ya vidonge kupanga uzazi
  • Kushindwa kumuweka mtoto vizuri ili adake titi
  • Mabaki ya kondo la nyuma kwenye kizazi
  • Historia ya upasuaji kwenye matiti
  • Kuvusha damu nyingi wakati wa kujifungua
  • Matumizi ya baadhi ya dawa baada ya kujifungua mfano dawa za aleji
  • Kumwanzishia mtoto maziwa bandia mapema sana bila kukamua maziwa yako mwenyewe

Mama kukosa maziwa baaa ya kujiungua: Nini kifanyike ili kuongeza maziwa ya mama?

Kunyonyesha kuna faida nyingi sana kwa mtoto na kwa mama. Kwa bahati nzuri kuna njia nyingi za kusaidia kuongeza maziwa ya mama ili mtoto anyonye zaidi.

  1. Nyonyesha au kamua maziwa mara kwa mara kadiri uwezavyo. kunyonya mara kwa mara kunashtua homoni ya hivo kuchochea zaidi uzalishaji wa maziwa. Hakikisha unanyonyeha mara 8 mpaka 12 kwa siku. Na kama maziwa yatakuwa kengi zaidi basi yakamue na yatunze ili utumie baadae
  2. Usimpe mtoto formula wala maziwa ya ng’ombe katika miezi 6 ya mwanzo. Tafiti zinaonesha mama anapunguza uzalishaji maziwa pale akianza kulisha mtoto chakula
  3. Badili titi unalompa mtoto kila unapotaka kunyonyesha, usikomae na titi moja pekee, tumia yote ili kuhakikisha maziwa yanaisha kwenye titi na hivo kuhochea mengine kuzalishwa
  4. Hakikisha unakunywa maji mengi na usiwe na kiu, pia upate muda wa kupumzika. Mwili wako unahitaji sana majimaji na lishe nzuri ukiwa unanyonyesha. Kula vyakula mbalimbali na, juisi na maji ili mtoto apate maziwa ya kutosha.
  5. Mpe mtoto nyonyo mda wote akiwa na njaa. Muweke mtoto karibu na titi utajua anataka kunyonya au kashiba
  6. Usilalie tumbo na matiti. Kugandamiza matiti inapunguza uzalishaji maziwa

Kwa ushauri na Tiba asili Tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Afya ya uke

Uchafu wa kunata ukeni

uchafu wa kunata ukeni

Uchafu ukeni upo wa aina nyingi sana, kuna uchafu mzuri na uchafu mwngine unaashiria kuna changamoto ya kiafya. Uhafu mwingi unaotoka unakuwa ukeni ili kukulinda dhidi ya maambukizi mengi. Topic ya leo tutajifunza zaidi kuhusu uchafu wa kunata ukeni na nini cha kufanya.

Ni kwaida kupata kiwango cha uchafu kiasi cha kujiko kimoja kila siku, na wingi wa uhafu utategemea upo siku ipi kwenye mzunguko wako.

Pamoja na kukulinda dhidi ya maambukii, uchafu wawea kuashiria endapo unaugua tatizo flani na kama inahitaji kwenda hospital haraka.

Je ni kawaida kutokwa uchafu wa kunata ukeni?

Uhafu wa ukeni unatofautiana mwonekano, wningi na uzito kulingana na mabadiliko ya homoni kwenye mzunguko wako. Uteute unaotoka ukiwa period siyo sawa na ule unaotoka siku za hatari.

Hebu tusome kwa undani nini kinatokea kwenye kila hatua/phase ya mzunguko.

Mzunguko wako unagawanyika katoka hatua/phase mbili; Tunaziita follicula phase na luteal phase. Katikati ya hivi vipindi viwili ndio kuna kipindi cha yai lililokomaa kutolewa yani ovulation.

Mabadiliko ya homoni na uchafu wa kunata ukeni

Vipindi hivi vyote vinaratibiwa na mabadiliko ya homoni ama vichocheo, homoni kama etrogen na progesterone. Estrogen inasaidia kujena ukuta na kuandaa kubeba mimba na pia inaathiri namna ya uchafu unaotoka.

Kama uchafu unatoka wa kunata basi kwa kiasi kikubwa yaweza isiwe tatizo. Lakini usiishie kwa kuangalia mwonekano tu wa uchafu, tazama na dalili zingine kama unahisi muwasho, haurufu mbaya, kutokwa damu na maumivu.

Kama uchafu unatoka ukeni ni wa kunata, ni mweupe na hauna rangi na hakuna haufu mbaya au dalili zingine mbaya mwilini. Basi hapo ujue uko salama kabisa

Je kwanini napata uchafu wa kunata ukeni

Uchafu wa kunata maa nwingi unaanza kutoka baada tu ya kumaliza hedhi na baada ya ovulation. Uchafu unavokuwa wa kunata zaidi ndvyo inakuwa ngumu kwa mbegu kuogelea na kurutubisha yai.

Uchafu huu wa kunata ni tofautia kabisa na uchafu uanovutika kama yai ambao unataoka kwenye ovulation. Uteute huu unakuwa laini na kuvutika ili kufanya mbegu kuogelea vizuri kwenda kurutubisha yai.

Vipi kuhusu uteute unaotoka ukiwa na hisia za mapenzi

Mwanamke ukiamshwa na hisia za mapenzi zikapanda, utahisi unyevunyevu ukeni na ute wa kuteleza. Huu ni ute alama ili usipate maumivu kwenye tendo wakati wa msuguano. Ute huu unaweza kunata kadiri unavoendelea na tendo.

Uteute karibia na siku ya hedhi

Unapokarbia kuanza hedhi utaanza kuona uteute wa jkunata ukeni, sawa na unapomalizia hedhi. Kipini hiki waweza kupata uchafu wa pink, brown au mwekundu ambao ni kawaida kabisa.

Uchafu unaoashiria maambukizi

Japo uchafu wa kunata ukeni siyo ishu kubwa sana, ni muhimu kutazama pia dalili zingine ili uone kama hauna maambukizi. Tazama kama uchafu unaambatana na dalili zingine kama

  • maumivu ukeni na muwasho
  • uchafu wa kijani
  • uchafu mwingi sana katoka siku
  • Uchafu wa kama maziwa mtindi au usaha
  • maumivu wakati wa kukojoa au kwenye tendo
  • maumivu chini ya kitovu
  • harufu mbaya ukeni kama shombo la samaki

Lini unatakiwa kumwona daktari?

Mwone daktari mapema ukiona daklili mbaya hapo juu. Utapata vipimo na kuanza toba mapema, maana magonjwa kama ya zinaa siyo ya kuhelewa kupata tiba.

Hitimisho kuhusu uchafu wa kunata ukeni

Mhanganyiko wa uhafu ukeni, bakteria wazuri na uteute unasaidia kulinda uke wako na kufanya uwe mlaini

Uchafu mzuri ukeni unatofautiana kwa wingi na uzito kulingana na upo siku ya ngapi kwenye mzunguko wako

Hisia za mapenzi, Ujauzito , hedhi na pia maambukizi vyote hivi vinaathiri mwonekano na wingi wa ucchafu unaotoka

Kama una hofu juu ya uhafu wako unaooka ukeni, basi tizama kama una unatoa harufu, ni mwingi kupita kiasi, upo kama maziwa mtindi, wa kijani na una dalili zingine za muwasho na malengelenge. Hapo unatakiwa kumwona daktari mapema.

Kwa ushauri na Tiba asili tuandikie kwa namba 0678626254

Categories
Siku za hatari

Je kubana miguu baada ya tendo kunasaidia kushika mimba mapema?

kubana miguu baada ya tendo

Kwa mwanamke unapojaribu kushika mimba,unakuwa na shauku ya kujaribu mbinu mbalimbali ili jambo lako ilitimie mapema. Wengi wanasema kubana miguu baada ya tendo yaweza kusaidia, hili tutaona kwenye makala ya leo kama ni kweli ama siyo.

Wanawake wanaamini kwamba kubana miguu baada ya kutiwa mbegu ni mbinu ya kuanya ashike mimba mapema. Baada ya tendo mwanamke ananyoosha miguu juu na kuibana huku akiegemeza kwenye kitanda au ukuta kwa dakika kadhaa.

Kubana miguu baada ya tendo na nguvu ya uvutano(gavity)

Dhana hii inabebwa na imani kwamba nguvu ya uvutano ya dunia yani gravity inarahisisha mbeu kuogelea na kwenda kurutibisha yai mapema.

Ni ahisi sana kuamini jambo hili, lakini tumewauliza wataalamu wa afya na kupitia tafiti mmbalimbali, na hapa chini tutasoma ukweli kuhusu dhana hii tuone uhalisia wake.

Je urutubishaji unaanyikaje? na Je kubana miguu baada ya tendo kunasaidia?

Kabla ya kujua kama kubana miguu baada ya tendo inasaidia kuhika mimba, tuone kwanza urutubishaji unatokeaje.
Kuna njia mbili ambapo urutubishaji unaweza kufanyika, moja ni kwa kuingiliana mwanamke na mwanaume bila kina na mbili ni kwa mwanamke kupandikizwa mbegu hospitali kwa kutumia vifaa maalumu.

Kupandikizwa yani atifirtial insemination kunafanykika na mtaalamu wa afya aliyebobea. Mbegu za mwanaume zinakusanywa kwa uangaliffu na kutunzwa, kisha mwanamke ataandaliwa na kupandikiziwa mbegu kwenye siku zake za hatari

Kubana miguu baada ya tendo ni imani tu isiyo na ukweli

Kama wataalamu wanavosema hakuna ukweli wowote kwamba eti kubana miguu inasaidia mbeu kuogelea, pia hata kulala chali kwa mda siyo suluhisho la mbegu kufika kwenye yai. Kuna baadhi ya mambo mengine unaweza kuanya kuongeza hansi yako ya kushika mimba ikiwemo kuanya tendo kwenye siku za hatari.

Utajuaje siku za hatari?

Njia zifuatazo zitakusaidia kujua siku ya ovulation/siku za hatari

1.Kwa miezi 8 mpaka 12 rekodi siku ambayo unaanza hedhi na uhesabu siku zote za kila mzunguko. Siku ya kwanza ni ile unayoanza hedhi katika mwezi husika na hesabu mpaka siku unayoanza hedhi katika mwezi mwingine hapo mzunguko mmoja utakuwa umekamilika.

2.Rekodi mzunguko mfupi na mzunguko mrefu zaidi katika ufuatiliaji wako

3.Kupata siku yako ya kwanza ya hatari chukua namba ya mzunguko mfupi zaidi toa 18, mfano mzunguko wako mfupi ni siku 27-18 inabaki 9.

4.Kupata siku yako ya mwisho ya hatari kwenye mzunguko, chukua siku za mznguko wakko mrefu toa 11. Mfano mzunguko wako mrefu ilikuwa siku 30-11 inabaki 19.
5.Katika mahesabu hapo juu ni kwamba siku kati ya mzunguko mfupi na mrefu ndizo siku zako za hatari, kwa maaana ya kuanzia siku ya 9 na 19 ndizo siku zako za hatari. Kama unataka usishike mimba basi usifanye ngono siku ya 9 ya hedhi mpaka siku ya 19.

Kubana miguu baada ya tendo kunasaidia kushika mimba haraka? Lini unatakiwa kumwona daktari?

Kitu cha muhimu sana unatafuta mimba ni kutazama ushauri wa daktari na vipimo endapo unatafuta mimba kwa zaidi ya miezi 12 bila mafanikio.
Kama unajaribu mimba a una historia ya changamoto kama hedhi kuvurugika, magonjwa ya zinaa, kutoa mimba nyingi, kuugua vimbe kama fibroids nk unatakiwa kumwona specialist wa wanawake mapema.

Mwanaume pia inahitajika apime mbegu (semen analysis) maana yawezekana shida ikawa ipo kwake na siyo kwa mwanamke.

Kwa ushauri na tiba asili tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Namna ya Kuhesabu umri wa mimba na Siku ya kujifungua

umri wa mimba

Nawezaje kujua umri wa mimba? Mpaka sasa umeshapima kwa UPT na umejua una mimba. Bilashaka una furaha sana maana sasa unakaribia kuitwa mama. Lakini pengine una kiu ya kujua mimba yako iliingia lini au ina umri gani. Pengine una wapenzi wawili na wote umekutana nao katika muda usiozidi wiki moja, sasa unawaza mimba hii ya nani?.

Lengo la makala hii ni kukwelekeza jinsi gani unaweza kuhesabu na ukajua umri wa mimba,bila hata kwenda hospitali.

Namna ya kuhesabu umri wa mimba

Kwanza muhimu ujue tafsiri ya hivi vifupi kwa maana vitatumika sana.
LMP yaani last menstural period, ikimaanisha siku ya kwanza kuanza hedhi yako ya mwisho kabla hujashika mimba na EDD-Estimated delivery date, yaani makadirio ya siku yako ya kujifungua.

Watoa huduma yani manesi na madaktari huwa wanapima umri wa mimba kwa kucheki kwanza lini ulipata hedhi yako ya mwisho. Kama mzunguko wako ni ule wa kawaida yani siku 28 maana yake siku ya hatari ni ya 14, kwahivo hapo mimba ilitungwa week mbili baada ya LMP. Sasa kwenye kuhesabu umri wa mimba hizi week mbili huwa zinaongezwa.

Kumbuka kwamba haya ni makadirio na siyo umri sahihi wa mimba. Kupima siku ya kujifungua, ongeza siku 280 ambazo ni wiki 40 kwenye siku yako ya kwanza kuanza hedhi ya mwisho, endapo una mzunguko wa siku 28.

Nitajuaje ni lini siku nilishika mimba?

Kitaalamu tunaita conception date- ni siku ambapo mimba ilitungwa. Kwasababu mbegu zinaweza kukaa kwenye kizazi mpaka siku 6, urutubishaji unaweza kutokea siku yoyote katika hizo siku 6 baada ya tendo. Mimba kutungwa kunategemea na yai limepevuka na kutolewa lini. Kama yai lipo tayari limeshatolewa na mbegu zimeingia, basi ndani ya masaa 24 mimba inatungwa.

Siku ya kujifungua

Mwanzoni utakuwa na hamu ya kujua umri wa mimba, ila kadiri miezi inavosogea sasa utakuwa na kiu ya kujua lini utajifungua? Muhimu fahamu tu kwamba unaweza kupata uchungu kabla a baada ya siku ya makadirio. Pengine daktari amekufatilia na ameona unahitaji kufanyiwa upasuaji, au kuchomwa sindano ya uchungu mapema. Vyote hivi vinachangia mabadaliko ya siku ya makadirio.

Kipimo cha utrasound kugundua umri wa mimba

Utrasound ni kipimo kinachotumia mawimbi ya sauti kupata picha za ndani ya mwili. Kujua ukubwa wa mimba na hata jinsia, watoa huduma wanaweza kutumia kipimo hiki cha utrasound. Pia utrasound inaweza kugundua kama mtoto ana changamoto za kiafya kama kushindwa kukua vizuri.

Vipi kama nilipandikiza kwa IVF, najuaje umri wa mimba?

Kwanza muhimu kujua IVF ni nini. IVF ni kifupi cha invitro fertilization, ni njia ya kupandikiza mimba ambapo mbegu na yai zinarutubishwa nje ya mwili, kisha kiume kinapandikizwa kwenye kizazi ili kikue.

Kwavile mimba hujapata kiasili, hata naman ya kufanya madadirio ya umri wa mtoto ni tofauti.

  • Kama yai fresh limetumika, utajumlisha siku 266 kutoka kwenye siku yai limetolewa kwenye kizazi chako kwa ajili ya urutubishaji
  • kama yai lilitunzwa kwa siku 3 basi jumlisha siku 263 kutoka kwenye siku ya upandikizaji
  • Kama mayai yalitunzwa kwa siku 5, basi utajumlisha siku 261 kwenye siku ya upandikizaji.

Namna ya kuhesabu siku ya kujifungua

Kujua siku ya makadirio yaako, muhudumu anaangalia siku ya mwisho kuanza hedhi na pia utrasound yako ya kwanza. Kisha watajumlisha siku 280 yani wiki 40 kwenye LMP. Baada ya hapo wnalinganisha na makadirio kwenye utrasound na kutoa siku ya kujifungua.