Categories
Uncategorized

Kiwango cha mayai ya mwanamke

yai la mwanamke

Mwanamke ana mayai mangapi?

Natambua una kiu sana ya kutaka kufahamu idadi ya mayai uliyonayo, na kama bado una uwezo wa kushika mimba kulingana na umri wako wa sasa. Makala hii itajibu maswal yako mengi kuhusu mayai ya mwanamke na uzazi.

Je watoto wa kike wanazaliwa na mayai?

Jibu ni ndio, watoto wa kike huzalishwa na mayai yote wanayotakiwa kuwa nayo. Hakuna mayai mapya yatazalishwa tena kwenye maisha yako kama mwanamke.

Mayai mangapi mwanamke anazaliwa nayo?

Pale kichanga kinapokuwa bado tumboni mwa mama kinakuwa na mayai karibu millioni 6. Mayai haya yanakuwa hayajapevuka na huitwa oocytes. Mpaka kufikia kuzaliwa mayai yanapungua mpaka milioni 1 mpaka 2.

Kwanini mtoto mdogo hapati hedhi wakati tayari ana mayai?

Hili ni swali zuri sana, kwamba nini sasa kinazuia mtoto asianze hedhi wakati tayai ana mayai? Mzunguko wa hedhi husubiri mpaka kipindi cha kubalahe ama kuvunja ungo. Balehe huanza pale ubongo unapoanza kuzalisha homoni ya GnRH-Gonatrophin-releasing hormone.

GnRH inachochea tezi ya pitutary ambayo huzalisha homoni ya FSH-follicle stimulating hormone. FSH ndio inachochea sasa mayai kuanza kupevuka.

Hedhi huanza kama miaka miwili baada ya matiti kuota. Wanawake wengi huvunja ungo na kuanza hedhi wakiwa na miaka 12 mpaka 15. Wachache sana huvunja ungo mapema wakiwa na miaka 8.

Mwanamke ana mayai mangapi anapovunja ungo?

Pale mwanamke anapofikia balehe, anakuwa na idadi ya mayai laki 3 mpaka laki 4. je nini kimetokea kwenye mayai mengine? Hili ndio jibu sahihi:- ni kwamba mayai mengi karibu 10000 yanakufa kila mwezi kabla ya balehe, yaani hayafikii kwenye kupevuka.

Mayai mangapi yanakufa kila mwezi baada ya mwanamke kuvunja ungo?

habari njema ni kwamba idadi ya mayai uanayokufa kila mwezi inapungua sana baada ya kuvunja ungo. Tafiti zinasema kwamba mwanamke anapoteza mayai 1000 kila mwezi baada ya kuanza hedhi/kuvunja ungo. Hii ni kama kusema unapoteza asilimia 30 mpaka 35 ya mayai kila mwezi.

Kila mwezi ni yai moja tu linapevuka na kuwa tayari kwa mimba kutunga kwenye siku za hatari. Ni mara chache sana inatokea mayai mawili yakawa tayari kwa kurutubishwa. Hapo ndipo wanapatikana mapacha wasiofanana.

Mwanamke ana mayai mangapi kwenye miaka ya 30s?

Mwanamke anapofikia miaka 32 uwezo wake wa kushika mimba unapungua sana na unashuka zaidi anapofika 37. Kuanzia miaka 35 mpaka 37 mayai yanakuwa chini ya laki 1. Hii ni sawa na kusema mayai yamebaki asilimia 3 tu ya hifadhi yote.

Mayai mangapi yanabaki kwa mwanamke wa miaka 40?

Pengine uko na miaka 40 na bado una kiu ya kushika mimba. Sasa unawaza umebakiwa na mayai kiasi gani. Tafiti zinasema kwamba kikawaida mwanamke anapofika miaka 40, idadi ya mayai inapungua chini ya 18,000/=. japo chansi ya kushika mimba iko chini, haimaanishi kwamba huwezi kushika mimba, bado inawezekana kubeba ujauzito katika umri huu.

Nini kinatokea baada ya kukoma hedhi?

Pale unapokoma hedhi na mayai kuisha, mifuko ya mayai inakoma kuzalisha homoni ya estrogen. Na hivo utaanza kupata dalili za tofauti kama ukavu ukeni, uchovu, kukosa hamu ya tendo. Endapo ulizaliwa na mayai mengi, kuna chansi kubwa ukaweza kushika mimba na ukapata mtoto hata kwenye miaka ya 40s.

Hitimisho

Umri mzuri wa kubeba mimba na kuzaa ni miaka ya 20s. Hapo ndipo mwanamke anakuwa na mayai ya kutosha na chansi ya kushika mimba ni kubwa sana. Kama unatafuta mimba kwa muda mrefu bila mafanikio, inahitaji uonane na daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake. Wote wawili me na ke mfanyiwe vipimo kujua chanzo cha tatizo.

Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Unataka kusafisha kizazi na kuongeza uzalishaji mayai? bofya hapa upate dawa asili zenye ubora

Categories
Natural remedies

Hatua Tano za kusafisha meno kwa njia asili

kusafisha meno na kuwa na meno meupe
Kusafisha meno inachukua muda

Zaidi ya asilimia 18 ya watu hufisha meno yao wakati wa kupiga picha, wengi wakiogopa aibu ya kuonekana wan meno machafu. Kuwa na meno meupe ni jambo kubwa sana katika jamii yetu ya sasa. Leo nitakwelekeza hatua rahisi tano za kusafisha meno yako ukiwa nyumbani, bila kutumia dawa zenye kemikali.

Meno ya Kun’gaa ni kiashiria cha usafi

Meno yako ni kitu cha kwanza watu wanakiona wanapokutazama, ni kiashiria cha utimamu wa afya yako na chanzo chako cha kujiamini mbele za watu. Kuwa na meno ya rangi nyekundu au njano ni kiashiria kwamba hujali kabisa afya yako. Bilashaka unahitaji nawe kuwa na tabasamu mawanana mbele za watu bila kuogopa.

Baadhi ya watu, pamoja na kusafisha meno asubuhi, bado wanakuwa na utando kwenye meno. Hii ni kutokana na tabia kama za kunywa kahawa au chai na kuvuta sigara. Meno ya njano au kijivu yanaweza kuashiria tatizo kubwa zaidi la kiafya. Kusafisha meno pekee bado haitoshi kulinda afya ya kinywa, unahitaji na kurekebisha chakula unachokulana mtidno wako wa maisha.

Kwanini meno yanabadilika kuwa na wekundu ama njano?

Meno yanachafuka na kubadilika kuwa na wekundu , njano ama wakati mwingine kuwa na weusi, kwasababu ya kugandamana kwa uchafu. Pamoja na kwamba ni ngumu kwa meno kuwa na weupe ule ule miaka yote mpaka uzee, kuna sababu nyingi zinafanya meno kuchafuka na uanweza kuziepuka.

Sababu hizi ni kama

  • kunywa kahawa na chai nyeusi
  • kuvuta sigara
  • lishe mbovu ikiwemo vitu vya sukari, soda nk
  • tatizo la mdomo mkavu (mate husaidia kulinda meno)
  • kupumua kupitia mdomo na kuziba kwa njia za pua. Hali hii inapunguza kiwango cha mate mdomoni
  • matumizi ya antibitics kwa muda mrefu
  • matumizi makubwa ya vitu vyenye madini ya fluoride na
  • changamoto za kurithi

Njia asili za kusafisha meno yakawa na weupe

1.Brush meno baada ya kunywa ama kula

Njia nzuri ya kusafisha meno yako yawe meupe ni kupiga mswaki baada ya kumaliza kula ama kunywa. Japo siyo rahisi kufanya kila mara lakini inawezekana ukijizoesha. Inategemea pia na eneo ulilopo, aidha makazini ama shuleni, anza kwa kupiga mswaki kabla ya kulala. Fanya hilo zoezi kwa mwezi mmoja kila siku mpaka iwe ni tabia.

Acha kuvuta sigara, kunywa kahawa na soda kwa wingi, kula lishe nzuri ili kuepusha meno kuchafuka. Jiwekee tabia ya kunywa zaidi maji baada ya kula ama kunywa juisi yoyote, kusaidia kuepusha madhara ya kitu hicho kwenye meno.

2.Coconut oil pulling

Coconut oil pulling ni mja ya njia murua kabisa ya kusafisha bakteria wabaya mdomoni mwako na kukuacha na harufu nzuri ya kinywa sikuzote na meno meupe. Ni njia salama na ya asili isiyohitaji matumizi ya kemikali mbaya wala dawa ambazo zina madhara makubwa.

Nimekuwa nikishauri mamia ya watu na wamefanikiwa kuondoa adha hii ya kunuka mdomo na meno machafu kupitia coconut oili pulling. Wewe pia unaweza kuwa mmoja wa mashuhuda wetu kama tu utazingatia kwa makini step za kufuata.

Coconut oil pulling kama jina lake lilivyo ni kitendo cha kuvuta uchafu na bacteria ka vile sabuni inavyonyonya uchafu kwenye nguo wakati wa kufua nguo. Lakini kwenye upande wa kinywa unanyonya bacteria na uchafu kwenye meno kwa kutumia mafuta ya kupikia ya nazi.

Hatua za kusafisha meno kwa mafuta ya nazi

  1. Hakikisha unafanya oil pulling asubuhi unapoamka kabla ya kula na kunywa kitu chochote
  2. Chukua kijiko kimoja au viwili vya mafuta ya kupikia ya nazi kisha weka mdomoni, anza kuzungusha ulimi na kuyasambaza mdomo wote taratibu kwa dakika 10 mpaka 20
  3. Baada ya muda huu tema uchafu wote bila kumeza hata kidogo kisha safisha mdomo na maji, unaweza kutumia maji yenye chumvi ili kuondoa mafuta yote.
  4. Hakikisha usiteme kwenye sink tema nje ili kuzuia kuziba kwa mafuta kwenye sinki
  5. Brush meno yako kama kawaida
  6. Rudia kitendo hiki mara 3 mpaka 5 kwa week kupata matokeo mazuri

3.Apple cider vinegar

Pamoja na faida zake kwenye mapishi na kupunguza uzito, apple cider vinegar ni nzuri sana katika kutoa uchafu sugu uliogandamana kwenye meno yako. Apple vinegar inafaa sana kwa uchafu uliosababishwa na kahawa na sumu ya nicotine kwa uvutaji sigara.

Nini siri iliyopo kwenye apple cider vinegar?

ina viambata hai vya acetic acid, potasium, magnesium na viambata cvya kuchakata chakula (enzymes)ambazo zinaua bakteria wabaya pia hapohapo inachochea ukuaji wa bakteria wazuri kwenye mfumo wa chakula.

Hakikisha unatumia apple vinegar kw amuda mrefu kupata matokeo. Siyo njia ya kukuletea matokeo haraka, jipe walau mwezi mmoja kwa meno yako kuanza kun’gaa.

Matumizi: Chovya kiasi kidogo cha apple vinegar kwa kidole, kisha pakaa kwneye meno yako una usugue kwa dakika moja taratibu. Baada ya hapo brush meno yako kawaida kwa dawa uuliyozea kuitumia.

Angalizo; Vinegar ina utindikali hivo sugua meno taratibu sana unapotumia vinegar.

4.Tumia maganda ya limau au chungwa

Kama ilivyo kwa apple cider vinegar, maganda ya matunda haya yana kemikali ambazo husaisidia kuondoa uchafu kwene meno na kukuacha na tabasabu zuri. Matumizi: chukua ganda la limau au chungwa, sugua meno yako machafu kwa dakika moja, kisha osha kwa maji na upige mswaki kikawaida.

5.Mkaa

Mkaa husaidia kunasa vimelea wabaya na kufyonza sumu kwenye meno yako. Kufanya meno kuwa meupe kwa kutumia mkaa, chonya mswaki wako kwenye maji kisha pakaa unga kidogo wa mkaa na ubrush meno yako. Safisha zaidi kwenye meno machafu.

Baada ya hapo utasafisha meno yako kwa dawa ya meno. fanya zoezi hili mara tatu tu kwa wiki, sitisha zoezi kama utaisikia vibaya au kama una pumu.

Hatari ya kutumia njia za kisasa kusafisha meno

Tafiti zinaonesha kwamba kusafisha eno kupitia njia za kisasa zinaharibu na kufanya meno kuwa dhaifu. Dawa nyingi za kusafisha meno zinazouzwa famasi zina kemikali mbaya za carbamide peroxide. Kemikali hii huzalisha urea ambayo hupelekea meno kuoza na kubomoka. Kemikali hizi pia hufanya meno kuwa dhaifu na kushindwa kun’gata vitu vigumu.

Tumia njia hizi endapo tu njia asili nilizoeleza pale juu hazijakupa matokeo katika kipindi cha mwezi mmoja. Kumbuka tu kwamba njia nzuri ya kusafisha meno na kinywa chako ni kwa kula lishe bora. Kusafisha meno vizuri kila siku asubuhi na jioni, kuepuka vyakula hatarishi kama vya sukari na kuacha sigara.

Categories
Urembo wa ngozi

Njia Asili za Kuondoa Michirizi kwenye ngozi

kuondoa michirizi kwenye ngozi
michirizi kwenye ngozi

Wanawake wengi kwa sasa wanatafuta njia gani salama za kuondoa michirizi kwenye ngozi. Michirizi na mikunjokunjo kwenye ngozi ya mapaja, tumbo na kwenye mikono ni tatizo linalowatesa zaidi wanawake. Kwani wengi wanahangaika ili kuondokana na tatizo hili bila mafanikio. Pamoja na kutumia vipodozi na cream mbalimbali bado tatizo halijaisha.

Tatizo linapelekea wadada kuona aibu, kushindwa kujiachia na kutovaa nguo wanazozitaka kwa kuogopa mikunjokunjo kuonekana.  Makala yangu ya leo itaangalia tatizo kwa upana wake na kukupa mpangilio wa lishe na ushauri wa kina. Pamoja na njia za asili za kutibu tatizo lako ili ufurahie urembo wako wa mwili, karibu.

Michirizi au cellulite ni kitu gani?

Cellulite ni mwonekano wa mikunjokunjo na mistari kwenye ngozi ya mwili. Mistari hii hutokea zaidi kwenye eneo la tumbo, chini ya mikono, kwenye mapaja na matako. Michirizi hutokea zaidi kadiri umri unavoenda. Baadhi ya vitu vinavyoletekeza mikunjokunjo kwenye ngozi ni pamoja na kuvurugika kwa homoni, pamoja na kutokufanya mazoezi.

Wanawake wanapata zaidi Michirizi kuliko Wanaume

Tatizo hili huwatokea zaidi wanawake kuliko wanaume ambapo kutokana na unene. Unene kupita kiasi hupelekea leya ya ndani yenye mafuta (fat globules) kuwa na msuguano na tishu za ngozi na hivo kupelekea mikunjokunjo na michirizi kwenye ngozi.

Tafiti zinasema kwamba asilimia 80 ya wanawake wana tatizo hili la cellulite. Ambapo wengi wanalipata kadiri wanavozeeka kwa ngozi kupungua uwezo wa kuvutika na kusababisha nyama kuanguka na kuleta mikunjokunjo.

Kuwa na michirizi siyo tatizo kubwa kiafya ndio maana wengi huliacha kama lilivyo bila kushughulika nalo. Lakini kama wewe ni mwanamke unayependa urembo na unapenda kujiachia maeneo kama beach na sehemu za wazi basi hiki kitakuwa kikwazo sana. Maana utaogopa kuonekana na watu kwamba ngozi yako ina kasoro ndio maana nimeandika makala hii ikusaidie.

Nini kinasababisha Michirizi Kwenye Ngozi

Mazingira hatarishi na sababu zinazochangia upate mikunjokunjo na michirizi kwenye ngozi ni pamoja na

  • lishe mbovu
  • mwili kubakiza maji tumboni (fluid retention ambapo wakati mwingie hupelekea tumbo kujaa gesi)
  • damu kutozunguka vizuri
  • udhaifu wa tishu zenye collagen na kuepelekea kujikunja kiurahisi
  • mabadiliko ya homoni
  • mwili kukosa mazoezi na kutoshugulika
  • msongo wa mawazo kupita kiasi ambao hupunguza uzalishaji wa collagen: collagen ni kiungo kilichosheni protini ambacho kinatengeneza shape na tishu za ngozi, hivo kufanya ngozi ya mtu kuonekana bado changa.
  • historia ya magonjwa mfano magonjwa ya autoimmune, kisukari, watu wanaovuta sigara na wenye alegi/mzio.

Sasa umejifunza jinsi sababu za kimaisha zinavoharibu mwonekano wa ngozi yako na tayari umejua chanzo cha tatizo lako kuwa ni kwenye lishe. Ni wazi sasa kwamba dawa na cream za kupata kwenye ngozi au mikanda ya kuvaa ili upunguze michirizi siyo suluhisho salama na la kudumu. Bali unatakiwa kubadili mtindo wa maisha  kwenye lishe na kuweka ratiba ya mazoezi.

Tiba Asili ili Kuondoa Michirizi na Mikunjokunjo kwenye Ngozi Yako

Hizi ni njia zangu 5 zitakazokusaidia kuondoa shida ya michirizi.
Angalizo: Kama wewe unataka njia za haraka haraka basi hutazipata hapa. Maana ninaelekeza namna ya kubadili mtindo wa maisha ili uepuke tatizo miaka yote, na itachukua muda kupata matokeo.

1.Kula Lishe Bora

Kama tulivosoma pale juu kuna uhusiano mkubwa kati ya uzito mkubwa na kitambi na kupata mikunjokunjo. Hivo punguza vyakula vya wanga na sukari na kula zaidi vyakula vya mafuta kama nyama, parachichi, nazi na mafuta ya nazi, samaki nk. Weka ratiba ya kupunguza unene wako uliopitiliza kwa kufanya mazoezi na kushugulisha mwili wako.

2.Tumia Collagen ya Kutosha

Kama tulivojifunza mwanzoni ni kwamba tishu za ngozi zimetengenezwa kwa protini za collagen. Kwahiyo kama ngozi yako ipo imara basi utapunguza uwezekano wakupata mikunjokunjo. Collagen ni protini inayopatikana kwa wingi kwenye ngozi na husaidia kuvutika na kufanya ngozi kuwa hai na laini.

Chanzo kizuri cha Collagen ni kunywa supu ya mifupa (bone broth) . Supu ya mifupa ina amino acid kwa wingi ambazo hutengeneza collagen. Collagen iliyopo kwenye Supu ya mifupa  husaidia kuimarisha tishu za ngozi na kuondoa tatizo la cellulite.

3.Tumia virutubisho

Virutubisho vya kuondoa mikunjokunjo kwenye ngozi na michirizi (anti-cellulite suppliments): Unaweza kufika ofsini kwetu ukatumia virutubisho kama royal gel na sipiriluna vikakusaidia kupambana na tatizo lako bila kikwazo.

4.Fanya mazoezi kila mara

Mazoezi ni njia nzuri sana pale unapotaka kupunguza uzito. Tumeona pale juu athari za uzito mkubwa na kitambi kwenye kupata mikunjokunjo, pamoja na kula lishe nzuri ni muhimu sasa uweke ratiba ya kufanya mazoezi walau mara tatu kwa week.

5.Tumia mafuta asili ya nazi kwenye kutibu ngozi yako.

Unaweza kutumia mafuta halisi ya nazi kwa kupaka kwenye ngozi yako baada ya kuoga. Kumbuka cream za madukani zinaweza kuwa ghali na hatari kwa afya yako kwa maana zina kemikali na metali nzito ambazo ni sumu kwa afya ya ngozi.

Maelezo ya Mwisho pale Unapopambana na michirizi+mikunjokunjo

  • Cellulite ni mwonekano wa mikunjokunjo kwenye ngozi na hii ni kutokana na kusuguana kwa tabaka la mafuta na tishu za ngozi
  • Sababu zinazopelekea upate mikunjokunjo kwenye ngozi ni pamoja na uzito mkubwa, lishe mbaya, kubakiza maji ama mwili kukosa kabisa maji, matatizo kwenye usafirishaji mwilini na udhaifu wa tishu zenye collagen kwenye ngozi
  • Kupunguza uzito, kula vyakula asili vyenye kambakamba na kufanya mazoezi ,  husaidia kupunguza sana tatizo la cellulite.

Mafuta ya lavender yanasaidia kuondoa michirizi

lavender oil

Mafuta ya lavender au mrujuani ni moja ya mafuta yanayotumika zaidi kwenye kundi la (essential oil) lakini faida zake ziligunduliwa kwa zaidi ya miaka 2500 iliyopita katika kutibu magonjwa na matatizo ya ngozi.

Matumizi ya mafuta ya lavenda kwa kupakaa kwenye ngozi huzuia na kuondoa chunusi na matatizo mengine ya ngozi kama madoa, michirizi, mikunjokunjo na pia kupunguza kasi ya kuzeeka kwa ngozi.

Mafuta ya levender yamekuwa adimu sana kutokana na uwezo wake mkubwa kupambana na matatizo ya ngozi. Fika ofsini hapa Magomeni Mwembechai upate mafuta haya ambayo ni original na asili. Gharama ya mafuta ni sh 40,000/=

Tuandikie whatsapp kwa namba 0678626254 kupata tiba ya tatizo lako

Soma makala inayofuata kuhusu: Kubana tumbo baada ya kujifungua

Categories
Natural remedies

Faida 8 za kunywa Green Tea

green tea
green tea

Green tea inasemekana kwamba ni moja ya kinywaji chenye afya sana duniani, na kinachopendwa zaidi.

Chai hii imejaa viondoa sumu vingi sana ambavyo vitakusaidia kuimarisha afya ya ubongo, kupunguza mafuta mabaya mwilini, kukulinga dhidi ya saratani na kupunguza hatari ya kuugua magonjwa ya moyo. Hapa chini ni maelezo ya nane za kunywa green tea.

1.Green tea ina viambata hai muhimu kwa ajili ya afya yako

Green tea ni zaidi tu ya chai kama ulivozoea. Ina viambata vya polyphenols, ambavyo vitakusaidia kupunguza mpambano(inflammation) kwenye mwili na pia kupambana na saratani.

Pia green tea ina viambata vya epigallocatechin-3-gallate(EDCCG). Viamabata hai hivi husaidia kuzuia madhara ya sumu mwilini na kulinda seli za mwili dhidi ya sumu.

2.Kuimarisha afya ya ubongo

Green tea inafanya kazi nzuri katika kukuweka kuwa mchangamfu na kuimarisha uwezo wa ubongo. Kiambata kikubwa ambacho kinaboost ubongo ni caffeine.

Usiogope kwamba ina caffeine nyingi kama kahawa hapana. Green ina kiwango kidogo tu cha caffeine ambacho kitachochea uzaishaji wa kemikali za dopamine na norepinephrine ambazo hufanya ubongo wako upige kazi zaidi.

Pia green tea inachochea ufanyaji kazi wa kemikali ya GABA. GABA ni ant-anxiety yaani inazuia msongo wa mawazo na hivo kukufanya ujisikie vizuri.

3.Kuondoa mafuta mabaya mwilini

Licha ya kuwa kiburudisho kizuri, green tea inachochea uwezo wa mwili kuunguza mafuta mabaya na hivo kupunguza uzito na nyama uzembe. Green tea inachochea shughuli za mwili na kupelekea mafuta kuunguzwa kuwa nishati.

4.Kupunguza hatari ya kuugua baadhi ya aina za saratani

Saratani husababishwa kukua kupita kiasi kwa seli za mwili. Ni moja ya ugonjwa unaaongoza kwa kusababisha vifo vingi sana duniani.

Tafiti zinasema kwamba seli zinapoathiriwa na sumu hupelekea seli hizi kuvimba na kuanzia kukua kupita kiasi. Viambata amana antioxidants zilizopo kwenye green tea husaidia kuzuia madhara ya sumu ambazo hupelekea saratani.

Tafiti zimebaini kwamba viondoa sumu vya kwenye green tea husaidia kupunguza hatari ya kupata aina hizi za saratani

Ili upate faida zaidi za green tea, epuka kuchanganya na maziwa. Baadhi ya tafiti zinasema kwamba unapochanganya na maziwa inapunguza ufyonzaji wa viondoa sumu.

5.Kulinda ubongo dhidi ya magonjwa ya uzee

Pamoja na kuimarisha ufanyaji kazi wa ubongo, green tea inasaidia kupunguza ubongo kuzeeka. Magonjwa makubwa yanayowakumba wazee kutokana na ubongo kuzeeka ni pamoja na Alzheimer na Parkinson. Magonjwa haya hupelekea ubongo kupungua uwezo wa kumbukumbu na pia kupunguza uwezo wa kufikiri.

6.Green tea itakusaidia kutibu harufu mbaya mdomoni.

Streptococcus mutans ni bakteria wanaopatikana sana kwenye mdomo. Bakteria hawa husababisha uchafu kuganda kinywani na kupelekea harufu mbaya na meno kuoza.

Kiamabata hai cha catechins kilichopo kwenye green tea kinasadia kudhibiti ukuaji wa bakteria hawa na hivo upunguza athari yake kwenye kinywa ikiwemo kuondoa harufu mbaya.

7.Green tea yaweza kukukinga na Kisukari cha Ukubwani.

Kisukari cha ukubwani ama type 2 diabetes ni aina ya kisukari inayompata mtu kuanzia miaka 20 kwenda juu. Aina hii husababishwa na mwili kushindwa kutumia insulini inayomwagwa kwenye damu ili kushusha sukari. Au mwili kutozalisha kiwango kinachotakiwa cha insulini.

Tafiti zinasema kwamba green tea husaidia kuongeza mwitikio wa mwili kwenye insulini na hivo kuzuia sukari kupanda kupita kiasi kwenye damu.

8.Green tea yaweza kuzuia magonjwa ya moyo

Magonjwa ya mfumo wa damu ikiwemo ikiwemo magonjwa ya moyo na stroke, ni moja ya chanzo kikubwa acha vifo duniani kote.

Tafiti zinasema kwmaba green tea yanweza kupunguza hatari ya kuugua magonjwa haya, kwa kupunguza mafuta mabaya mwili (bad cholesterol).

Green tea pia inaongeza viondoa sumu kwenye damu, na hivo kulinda mishipa ya damu dhidi ya athari ya mafuta mabaya(LDL). Mafuta haya mabaya huweza kusababisha damu kuganda na hivo kuzuia usambazaji wa hew aya oxygen mwilini.

Unahitaji Green kutibu changamoto zako? Agiza kutoka kwetu green tea zenye ubora mkubwa kwa Tsh 50,000/=

Hapa chini ni picha na maelezo mafupi kwa kila green tea zetu. Kumbuka hizi ni zaidi ya chai, ni tiba kwa magonjwa yako ya kiafya. Chagua unayohitaji kisha fika ofsini kuchukua. Ikiwa upo mkoani tutakutumia. Kila chai tiba ni tsh 50,000/=

Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu

Bofya kusoma makala inayofuata: Chanzo cha fangasi mdomoni+tiba

Categories
Fangasi

Fangasi Mdomoni

fangasi mdomoni
fangasi mdomoni

Fangasi mdomoni kwa kitaalamu oral thrish au oral candidiasis ni maambukizi ya fangasi aina ya candida kwenye kuta laini za mdomo.

Kwa watu wengi wenye fangasi ya mdomo haileti changamoto kubwa sana na wanaweza kuishi na wagonjwa na maisha yakaendelea. Japo kwa watu wenye kinga dhaifu fangasi wa mdomoni huleta athari sana na dalili mbaya zaidi.

Habari njema ni kwamba wagonjwa wengi wanapona vizuri kabisa wakipatiwa tiba kwa fangasi za mdomoni. Japo wagonjwa wengi huugua tena katika kipindi cha muda mfupi baada ya kupona hasa kama chanzo cha fangasi kwa upande ni uvutaji wa sigara. Katika makala hii tutakwelekeza chanzo cha fangasi mdomoni, dalili zake pamoja na tiba.

Dalili za fangasi mdomoni

Kwa watu wazima dalili kuu ya fangasi mdomoni ni utando mweupe mzito kwenye ulimi. Endapo utando huu ukikwanguliwa mgonjwa anaweza kutokwa na damu. Baada ya muda utando huu unaweza kubadilika na kuwa malengelenge ya rangi nyekundu.

Chanzo cha fangasi mdomoni

Fahamu kwamba fangasi aina ya candida wapo maeneo mengi sana ya mwili. Kama kwenye mdomo, ukeni, mkunduni, kwenye ngozi, na tumboni pia. Katika hali ya kawaida ya mwili, fangasi hawa hawana madhara kabisa.

Pale kinga ya mwili inaposhuka ndipo fangasi hawa wanapata muda wa kumea na kushambulia mwili. Kuvurugika kwa mazingira ya mdomo kutokana na kutumia dawa zingine ni chanzo pia cha fangasi hawa wa candida kukua na kuleta madhara.

Mazingira yanayongeza hatari ya kupata fangasi mdomoni.

Kwa watu wazima mambo yafuatayo yanakuweka kwenye hatari zaidi ya kupata fangasi ya mdomoni kiurahisi.

Watu wanaotumia meno bandia(dentures) ili kuziba jino lililon’golewa-hatari ni kubwa endapo meno bandia haya hayataondolewa wakati wa kulala ama yasipofitishwa vizuri.

Antibiotics– matumizi ya dawa za kuuma vimelea wa bakteria maarufu kama antibitics kwa muda mrefu yanakuweka kwenye hatari zaidi ya kuugua fangasi mdomoni. Kwani dawa hizi huua mpaka bakteria wazuri waliopo mdomoni ambao ni kinga dhidi ya fangasi wabaya.

Matumizi ya mothwash kwa muda mrefu

Watu wanaotumia mouthwash kwa muda mrefu ili kutibu harufu mbaya mdomoni wako kwenye hatari zaidi ya kupata fangasi mdomoni, kwasababu mouthwash zinaua na bakteria wazuri.

Matumizi ya dawa za homoni(Steroid medication) kama zile za kusisimua misuli.

Kinga kushuka– watu wenye kinga dhaifu wanaugua sana fangasi mdomoni, kinga dhaifu inaruhusu fangasi kukushambulia kiurahisi.

Kuugua kisukari

Wagonjwa wa kisukari huwa na kinga dhaifu sana na hivo kushambuliwa haraka na fangasi wa mdomoni.

Mdomo mkavu-watu wenye mate kidogo kitaalamu(xerostomia) wako kwenye hatari zaidi ya kuugua fangasi mdomoni.

Lishe- ukosefu wa madini na vitamini muhimu mwili kutokana na lishe mbovu hupelekea kinga kushuka na hivo kuruhusu mwili kushambuliwa kiurahisi na fangasi mdomoni. Lishe yenye upungufu wa madini chuma, vitamin B12 na folic acid ni chanzo cha kuugua fangasi.

Kuvuta sigara- wavutaji wa sigara kupita kiasi wanapelekea kuvurugika kwa mazingira ya mdomo na hivo kuugua fangasi haraka.

Uchunguzi wa daktari hospitali ili kugundua Fangasi mdomoni

Kwa kiasi kikubwa uchunguzi wa fangasi mdomoni hufanyika kwa daktari kutazama kinywani mwako na kukuuliza baadhi ya maswali. Daktari anaweza kuchukua baadhi ya sample ya utando wako mdomoni na kuepeleka maabara kwa ajili ya vipimo. Kama daktari atagundua chanzo cha tatizo lako basi atakupatia tiba kulingana na chanzo husika.

Tiba Kupitia Vidonge vya Propolis

Ni vidonge asili viliyotengenezwa kupitia bidhaa adimu ya propolis ili kutibu mambukizi sugu ya fangasi mwilini. Dozi moja inatumika kwa wiki mbili, unameza kila siku vidonge viwili asubuhi na jioni. Huhitaji kufanya utafiti ni dawa ipi nzuri, tayari tumeshafanya hivo kwa zaidi ya miaka mitano sasa na kukuletea dawa hii iliyothibitishwa.

Baada ya kutumia propolis tegemea haya ndani ya wiki mbili

  • Fangasi yako kupona kabisa
  • Dalili zote mbaya mbaya muwasho na maumivu kuisha
  • Kinga ya mwili kuimarika na fangasi kutojirudia

Gharama ni Tsh 90,000/=, Tupo Magomeni Dar. Chati nasi kwa whatsapp no- 0678626254 kuanza tiba

Bofya kusoma makala inayofuata: Fahamu kina na urefu wa uke