Categories
Hedhi salama Siku za hatari

Kumeza P2, Maswali na Majibu

vidonge vya p2
vidonge vya p2 kuzuia mimba

Nini Kinatokea P2 isipofanya kazi?

P2 ni vidonge vya kumeza kwa dharula tu ili kuzuia mimba isiyotarajiwa endapo hukutumia kinga. Lakini unaweza kuwa unajiuliza je kuna uhakika gani kama p2 zinakusaidia kuzuia mimba? Uwezo wake ni asilimia ngapi? Na vipi kama haitafanya kazi nini kitatokea?

Hapa chini kuna majibu ya maswali yako yote kuhusu p2 kutoka kwa watalamu na wabobezi wa afya ya uzazi. Tusome zaidi.

Je unaweza kushika mimba hata baada ya kumeza p2?

P2 ama morning after pill au plan B, ni dawa zilizopo kwenye kundi la levonorgestrel. Ambazo kazi yake ni kuzuia usishike mimba baada ya tendo endapo umesahau kinga, au kondomu imepasuka au ulifanya tendo ukiwa umelewa.

Dawa zinafanya kazi kwa kuzuia yai kutolewa kwenye ovary wakati wa ovulation, na hivo kuzuia mbegu na yai zisikutane kufanye kiumbe.

Muda sahihi wa kumeza p2 ni upi?

Kumbuka mbegu inapoingia kwenye uke inachukua saa 12 mpaka 48 kwenda kurutubisha yai. Na dawa inafanya kazi vizuri endapo utameza ndani ya masaa 12 baada ya kufanya tendo. Ukimeza ndani ya masaa 24 chansi ya kuzuia mimba ni asilimia 95 na zaidi.

Ukimeza kuanzia masaa 48 mpaka 72, yani siku 2 mpaka 3 baada ya kufanya tendo, chansi ya kuzuia mimba inapunguza mpaka asilimia 61 pekee. Kumbe sasa uwezekano wa kushika mimba hata kama ulimeza p2 unaongezeka kadiri unavochelewa kumeza kidonge.

Dalili gani nitapata baada ya kumeza p2?

Baada ya kumeza p2 tegemea kupata dalili ama side effects kama

  • kichefuchefu
  • maumivu ya tumbo
  • kichwa kuuma
  • kizunguzungu na
  • kutapika

Kama utatapika ndani ya masaa mawili bada ya kumeza dawa, unatakiwa umeze tena kidonge kingine ama utumie njia ingine ya kuzuia mimba kama condom.

Je uzito mkubwa na kitambi ni kikwazo cha p2 kufanya kazi?

Jibu ni ndio, tafiti zinaonesha kwamba wanawake wenye uzito mkubwa na kitambi wapo kwenye hatari ya kushika mimba hata kama wametumia p2 vizuri. Inashauri kama wewe ni mnene tumia kitanzi cha copper kama njia ya kisasa kuzuia mimba.

Dawa Zinapelekea P2 isifanye Kazi

Ni muhimu pia kujua kwamba baadhi ya dawa zinaweza kuathiri utendaji wa P2. Dawa kama za fungus, HIV, dawa za kifafa na baadhi ya antibiotic,. Sasa unapoenda dukani kununua P2, hakikisha unamweleza muhudumu hali yako ya kiafya na dawa unazotumia kwa muda huo.

Je p2 zinafanya kazi kwenye ovulation?

Dawa za p2 zinafanya kazi vizuri kabla ya ovulation, yani kabla yai halijatolewa. Hii ni kwasababu inazuia kabisa yai kutolewa kwenye ovari na hivo kuzuia urutubishaji.

Lakini hata kama yai limeshatolewa, kidonge kinazuia mbegu kulifikia yai, kwa kufanya ute wa ukeni uwe mzito sana kiasi mbegu zinashindwa kuogelea.

Kama pengine umechelewa kumeza kidonge, na tayari yai limerutubishwa, basi kidonge kinazuia kiumbe kujishikiza kwenye ukuta wa kizazi na hivo mimba haitakuwepo.

Je kuna madhara kwa mjamzito kumeza P2?

Ni muhimu pia kujua kwamba, endapo umemeza kidonge bahati mbaya bila kujua kumbe kuna mimba, haitakuwa na madhara. Kiumbe kitaendelea kukua pasipo shida.

Maelezo ya Mwisho Kuhusu P2

Meza p2 kwa emergency tu na siyo kila siku. P2 ziapelekea hedhi kuvurugika na homoni kuvurugika. Tumia kwa tahadhari na usizoee kuzimeza kila siku.

Endapo unatafuta njia ya kupanga uzazi ya mda mrefu, tafadhali tembelea hospitali uonane na muhudumu akupe maelekezo.

Kwa ushauri zaidi na tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Soma hapa ikiwa hedhi yako Imevurugika na unataka kuiweka sawa.

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Hedhi salama

Maumivu ya Tumbo la Chango

tumbo la chango

tumbo la chango

Chango ni kitu gani hasa?

Tumbo la chango au mchango, wengi husema wakimaanisha maumivu makali ya tumbo kipindi cha hedhi. Kitalamu maumivu haya huitwa dysmenorrhea, ikimaanisha maumivu kutokana na kujikaza kwa ukuta wa kizazi ili ubomoke na kutoa damu kipindi upo kwenye hedhi.

Aina za tumbo la chango

Kuna aina kuu mbili za maumivu haya ya hedhi ama mchango, ambayo ni primary dysmenorrhea na secondary dysmenorrhea.

Primary Dysmenorrhea (Tumbo la Chango la kawaida)

Chango hili la uzazi ni yale maumivu ya kawaida yanayokupata kila mwezi kwenye hedhi na hayatokani na ugonjwa wowote. Maumivu haya huanza siku moja ama mbili kabla hujapata hedhi yako. Waweza kuhisi maumivu kwenye nyonga, kiuno na tumbo pia.

Pia chango la namna hii huchukua masaa 12 mpaka 73 yani siku 3 kuisha, na inaambatana na dalili zingine kama kichefuchefu na kutapika na hata kuharisha. Chango la namna hii huwa linapungua kadiri unazozeeka ama pale utakapozaa.

Secondary Dysmenorrhea (Tumbo la Chango lisilo Kawaida)

Chango lako linaposababishwa la ugonjwa fulani kwenye via vya uzazi. Chango hili huanza mapema zaidi kwenye mzunguko hata wiki kabla na inachukua mda mrefu sana kuisha. Mara nyingi chango hili halina dlaili za kuchefuchefu, kutapika kukosa nguvu na kuharisha.

Nini kinapelekea upate maumivu makali sana kwenye hedhi?

Maumivu hutokea pale kemikali inayoitwa prostaglandin inapofanya ukuta wa kizazi kujikaza. Ukuta wa kizazi ambapo mtoto hujishikiza na kukua,umetengenezwa kwa misuli, na unajikaza kwenye hedhi ili kubomoka kutoa damu isiyohitajika.

Ukuta unapojikaza sana, unaleta mgandamizo kwenye mishipa ya karibu ya damu, na hivo kupunguza kiwango na hewa safi ya oksijen kwenda kwenye misuli. Na misuli inapokosa hewa ndipo unapata maumivu makali.

Chango la uzazi kutokana na ugonjwa

Chango hili laweza kutokea kwa kusababishwa na ugonjwa fulani, changamoto hizi ni pamoja na

  1. Endometriosis: Changamoto ambapo kuta za kizazi zinakua na kwenda nje ya kizazi. Tishu hizi nyakati za hedhi zitapelekea maumivu makali na kuvimba.
  2. Adenomysis: Hili ni tatizo ambapo kuta za kizazi zinakua kuelekea kwenue misuli ya kizazi. Tatizo hili kaweza kupelekea kizazi kutanuka na hivo kuletea bleed nyingi yenye maumvu
  3. PID: Haya ni maambukizi ya bakteria kwenye njia ya uzazi. PID yaweza kuleta maumivu makali chini ya kitovu, kwenye tendo na maumivu nyakati za hedhi yani chango.
  4. Fibroids: Hizi ni vimbe ambazo siyo za saratani ndani au nje ya kizazi, zinazopelekea chango kali sana
  5. Cervical stenosis: Hiki ni kitendo cha mlango wa kizazi kusinyaa na hivo kuzuia damu kutoka kwa kasi nzuri hivo kuleta maumivu ya chango kwenye hedhi.

Vipimo: Utajuaje kama Chango lako la kawaida au ni hatarishi?

Kama chango lako linachukua zaidi ya siku 3, hakikisha unaenda hospitali kufanyiwa vipimo. Kumbuka aina zote za chango zinaweza kutibiwa hospital na hata kwa tiba asili. Muhimu kwanza ni kujua nini kipo nyuma ya chango lako.

Kwanza kabisa daktari atakwambia ujieleze dalili zote unazopata kwenye hedhi pamoja na mzunguko wako ukoje. Pili daktari atakufanyia vipimo ndani ya via vya uzazi(pelvic exam) ambapo ataingiza kifaa ukeni kucheki kama kuna hali yoyote isiyo ya kawaida kwenye uke, mlango wa kizazi na kizazi chenyewe.

Daktari anaweza pia kuchukua kiwango cha majimaji kwenye uke na kupeleka maabara kwa ajili ya vipimo zaidi.

Nini kinatokea kama kuna ugonjwa?

Kama daktari atahisi pengine kutokana na dalili zako una chango la ugonjwa, hapo utafanyiwa utrasound. Na ikionekana kuna shida, daktari atajikita zaidi kukutibu tatizo husika.

Nini cha Kufanya ili Kupunguza Maumivu ya Chango kwa Muda

Kuna njia nyingi ambazo husaidia kupunguza maumivu ya hedhi ambazo unaweza kutumia ukiwa nyumbani kwako kabla ya kwenda hospitali. Kama maumivu ni makali sana unaweza:-

  • Kumeza dawa za kukata maumivu kama ibuprofen kwa ahueni ya haraka. Angalizo: dawa za maumivu isiwe ni nia ya kutumika kila mara kwani madhara yake ni makubwa kiafya, dawa hizi zitumike kwa uangalifu.
  • Tumia maji ya uvuguvugu kukandakanda mahali pa tumbo la chini
  • Epuka kuvuta sigara na kunywa pombe kipindi cha hedhi
  • Usitumie vinywaji na vyakula vyenye caffeine mfano majani ya chai na kahawa
  • Fanya masaji kwenye upande wa chini wa mgongo na sehemu ya tumbo la chini.
  • Pata muda mwingi wa kupumzika
  • Weka ratiba ya kufanya mazoezi mara kwa mara: Tafiti zinasema wanawake wanaofanya mazoezi hupunguza maumivu ya hedhi kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na wasiofanya mazoezi.

Lini natakiwa Kumwona Daktari?

Chango linapokuwa kali sana linapelekea baadhi ya wanawake washindwe kufanya kazi zao na kushindwa kwenda darasani. Huhitaji kabisa kuvumilia mateso ya namna hii, unahitaji kuishi vizuri na kufurahia maisha. Kama maumivu hayavumiliki hakikisha unaenda hospital haraka.

Jua mzunguko wako

Ni muhimu sana kujua mzunguko wako, pia ujue maumivu huwa yanaanza siku ngapi kabla ya hedhi. Kama chango linaambatana na dalili zingine mfano maumivu makali ya kichwa, bleed nzito sana na nyingi, nenda hospitali.

Je Tumbo la Chango Linapelekea Ugumba?

Kama tulivoona kwamba chango siyo ugonjwa bali ni dalili za maumivu makali ya tumbo la hedhi. Sasa kama unapata chango la kwanza (primary amenorrhea) hapo hakuna kikwazo cha kushika mimba. Lakini kama chango lako ni ile aina ya pili yani secondary amenorrhea, hapo lazima kuwe na kikwazo kushika mimba mapema.

nini ufanye kama umetafuta mimba mda mrefu bila mafanikio?

Endapo wewe na mme wako mmetafuta mimba kwa zaidi ya mwaka mmoja, nendeni hospitali wote wawili kupimwa kujua chanzo cha tatizo. Mwanamke utapima mirija, kizazi na homoni na mwanaume atapimwa mbegu kuona kama zina hitilafu.

Unahitaji ushauri na tiba? Tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Uncategorized

Maumivu ya kichwa baada ya tendo

maumivu ya kichwa

Japo inatokea kwa watu wachache sana, unaweza kupata maumivu ya kichwa baada ya kufanya tendo hasa baada ya kufika kileleni. Maumivu haya yanaweza kuisha ndani ya dakika chache ama yakaendelea kwa zaidi ya masaa mawili.

Je maumivu ya kichwa baada ya tendo yakoje?

Maumivu haya (orgasim headache)yanaweza kuanza taratibu kwenye shingo na kichwa kadiri unapopandwa na hisia na kuongezeka kadiri msisimko watendo unavoongezeka. Au maumivu yanaweza kuja kwa haraka na makali sana kwenye eneo la mbele kuzunguka macho, pindi tu ukifika kileleni.

Karibu asilimia 75 ya watu wanaopata maumivu ya kichwa, wanasema yanatokea pande zote za kicha kulia na kushoto.

Je nini chanzo cha tatizo?

Madakatari wanafikiri kwamba maumivu ya kichwa ni kutokana na mishipa midogo ya damu kuvimba (vascular headache). Pale mtu akifika kileleni.

Pale mtu anapofika kileleni, presha ya damu hupanda juu kwa kasi. Kupanda huku kwa presha kunapelekea mishipa midogo ya damu ya kichwa kutanuka haraka na hivo kupelekea maumivu ya kichwa.

Vihatarishi vinavyopelekea maumivu ya kichwa kwenye tendo

Kila mtu anaweza kupata maumivu ya kichwa baada au wakati wa tendo. lakini tafiti zinasema kwamba chansi ya wanaume kupatwa na tatizo ni zaidi ya mara 4 kwa wanawake.

Pia watu walio kwenye umri wa kuanzia miaka 40 na kuendelea wapo kwenye hatari zaidi ya kukutwa na tatizo ukilinganisha na vijana wadogo.

Watu wenye historia ya kuumwa kichwa mara kwa mara kutokana na mwanga mkali au kikohozi pia wanaweza kuumwa kichwa kwenye tendo.

Je maumivu yanaisha kwa muda gani

Kwa kiasi kikubwa maumivu ya kichwa kwenye tendo huisha yenyewe ndani ya dakika chache. Baadhi ya watu hupatwa na maumivu haya mara moja na wengine hupatwa mfululizo katika week au mwezi.

Kama maumivu yatendelea zaidi ya lisaa na yanajirudia mara kwa mara, unatakiwa ummwone daktari. Matibabu ni pamoja na dawa za maumivu kama ibuprofen na dawa za kupunguza presha (beta blockers)

Maumivu ya kichwa baada ya tendo inaweza kuashiria uwepo wa changamoto kubwa ya kiafya. Kwa mazingira hayo unatakiwa kutibu chanzo cha tatizo kwanza.

Lini Unatakiwa Kumwona Daktari?

Siyo kila maumivu ya kichwa kwenye tendo ni ya kawaida. Daktari atakusaidia kujua kama tatizo ni la kawaida ama kuna chanzo kingine cha tatizo. Baadhi ya changamoto zinazoweza kupelelekea upate maumivu ya kichwa kwenye tendo ni pamoja na

  • Maambukizi ya bakteria, fungus au virusi
  • Magonjwa ya moyo
  • Kulegea kwa mshipa wa damu kwenye ubungo
  • Kupungua kwa njia ya mshipa wa damu safi kwenye ubongo
  • Kuvuja kwa damu ndani ya kichwa
  • Kiharusi
  • Matumizi ya baadhi ya dawa kama za kupanga uzazi

Maumivu yasiyo ya kawaida kwa kiasi kikubwa yanaambatana na dalili zingine kama

  • kichefuchefu
  • kutapika
  • shingo kukakamaa na
  • kupoteza fahamu

Watu wanaopata hizi dalili wanatakiwa kupelekwa hospitali haraka

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Hedhi ya kuteleza kama mlenda

hedhi ya kuteleza

Kama hujawahi kupata hedhi ya kuteleza mithili ya mlenda, inaweza kukuchanganya sana akili siku ya kwanza.

Kwa mwanamke kuwa na mzunguko mzuri wa hedhi ni jambo la kujivunia na linaloleta heshima sana. Mzunguko wa hedhi unaweza kutoa picha kamili nini kinaendelea kwenye mwili wa mwanamke. Kama mfuko wa mimba unapata mzunguko mzuri wa damu, homoni zako zinbalansi, au kama mayai yanatolewa kwenye ovari

Makala hii itaongelea kwa kina juu ya hedhi ipi ni salama na ipi siyo salama. karibu tujifunze.

Hedhi ya kuteleza kama mlenda.

Kwa kiasi kikubwa kupata hedhi ya mlenda ni kutokana na damu iliyoganda kwenye ukuta wa kizazi inetolewa nje. Endapo unapata mabonge madogo madogo ya damu ujue ni jambo la kawaida kabisa.

Kumbuka kwamba unapoanza hedhi ndio mwanzo wa mzunguko wako. Ni kipindi ambacho ukuta wa kizazi unabomoka kwasababu yai halikurtubishwa. Hedhi ni mchanganyiko wa damu ya ukuta wa mji wa mimba, maji maji ya ukeni na yai lisilorutubishwa.

Kumbuka pia kwamba siku ya kwanza ya hedhi inaweza kutoka nyingi na nzito kuliko siku zingine.

Hedhi kidogo inayoambatana na maumivu makali ya tumbo

Kama unapata hedhi nyepesi, nyekundu inaweza kuashiria kwamba mzunguko wa damu kwenye mfuko wa mimba ni mdogo. Unaweza kupunguza hali hii kwa kufanya masaji kwenye eneo la tumbo ukitumia mafuta ya mnyonyo, ama kitambaa kilicholowekwa kwenye maji ya moto.

Hedhi ya vipande vipande vya damu

Kadiri hedhi inavoendelea, unaweza kuanza kupata hedhi kama ya damu iliyoganwanyika vipande. Hii ni kawaida na inatokana na kuganda kwa damu kwenye ukuta wa kizazi. Hii ni kawaida kabisa na isikupe hofu. Damu hizi za kuganda zinaweza kuwa nyekundu sana, nyekundu mpauko au brown.

Hedhi nzito yenye weusi ama brown

Hii inaonesha kwamba kuna masalia ya damu ya zamani kwa hedhi iliyopita. Kubaki kwa damu husababishwa na flow ya polepole sana na mzunguko mdogo wa damu ndani ya mfuko wa mimba. Unaweza kurekebisha tatizo hili kwa kuhakikisha unakunywa maji ya kutosha, kufanya masaji eneo la tumbo na pia unaweza kujaribu uterus cleansing package yetu.

Hedhi nyepesi ya majimaji

Pale unapoelekea kumaliza hedhi yako, unaweza kupata damu nyepesi sana na nyembamba. Damu hii inaweza kuwa nyeusi pia kutokana na mwingiliano wa hewa ya oksijen na damu.

Kama hedhi inatoka ni damu mbichi na nyekundu ya kung’aa. inaonesha inatoka moja kwa moja kwenye kizazi. Na inaweza kuashiria jeraha kwenye kizazi au pengine mimba kuharibika.

Nenda hospitali mapema endapo utaona damu mbichi na nyepesi ikitoka kwenye kizazi, hasa kama umepitisha hedhi kwa siku kadha,maana yake kuna uwezekano kulikuwa na mimba.Pia kama unatoa mabonge ya damu mfululizo na ni makubwa, hakikisha unaenda hospitali.

Je hedhi ya mabonge inaashiria nini??

Kutokwa na mapande ya damu kwenye hedhi mfululizo ni kitu hatari na inaashiria changamoto fulani ya kiafya. Hedhi nzito kisha inachukua zaidi ya siku 5 inaweza kuashiria dalili za

  • Vimbe kwenye kizazi (fibroids)
  • Kutanuka kwa kizazi (adenomysis)
  • Vimbe kwenye mayai (PCOS)
  • Saratani kwenye kizazi
  • Changamoto ya tezi ya shingoni (thyroid condition)
  • Majeraha kutokana na kitanzi
  • Upungufu wa vitamin K

Lini unatakiwa kumwona daktari?

Endapo unapata dalili ambazo hujazoea kweye hedhi yako, pamoja na dalili zinazokunyima uhuru, unatakuwa kumwona daktari dalili hizi ni pamoja na

  • Kukosa nguvu na kuishiwa pumzi kwenye hedhi-hii yaweza kuashiria upungufu wa damu
  • Maumivu na kutokwa damu kwenye sex
  • Mabonge ya damu makubwa
  • Kutumia zaidi ya pedi mja kwa lisaa
  • Hedhi ya maji maji ya kung’aa au kijivu
  • Kupata hedhi nyingi zaidi ya siku 7

    Kwa maoni na ushauri tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254.

    Categories
    Uzazi wa Mpango

    Njia asili za kupanga Uzazi

    ufatiliaji wa mzunguko-kushika mimba
    kupanga uzazi kupitia kalenda

    Kwanini tunasema hizi ni njia asili-natural contracepives? Ni kwa sababu hazibadili mpangilio wa homoni au vichocheo kwenye mwili. Badala yake njia hizi zinamwongoza mke na mume kutofanya ngono wakati yai limepevuka.

    Yani lengo ni kutoruhusu mbegu ikalifikia yai lililokomaa kurutubishwa. Ni muhimu sana kufatilia kwa ukaribu viashiria vyote vya yai kupevuka.

    Kikawaida yai hutolewa kila baada ya siku 14 kabla ya hedhi ijayo. Hapo kwenye siku 14 toa siku mbili nyuma au ongeza siku mbili mbele. Lakini kwasababu yai linaweza kuishi mpaka siku 3 au 4 baada ya kutolewa na mbegu inaweza kuishi siku mbili mpaka tano, kufanya mahesabu vizuri inabidi uzingatie kwa week na siyo kwa siku.

    Njia asili za kupanga uzazi zinafanya kazi kwa asilimia mpaka 98, lakini zinataka ufatiliaji wa kila siku na kujicontrol hisia zako.

    Njia ya kwanza ni calender

    Hii inawafaa zaidi wenye mzunguko mzuri. Ni topic ndefu inayohitaji kusoma taratibu na kuelewa. Ni zoezi ambalo laweza kuchukua miezi miwili mpaka mia4 kulifatilia na kulizoea, kwani yatakiwa kurekodi na kufatilia matukio na mabadiliko yote ya mwili wako.

    Hatua kwa hatua za kufatilia kalenda

    1. Kwa miezi 8 mpaka 12, rekodi siku ambayo unaanza hedhi na uhesabu siku zote za kila mzunguko. Siku ya kwanza ni ile unayoanza hedhi katika mwezi husika na hesabu mpaka siku unayoanza hedhi katika mwezi mwingine hapo mzunguko mmoja utakuwa umekamilika
    2. Rekodi mzunguko mfupi na mzunguko mrefu zaidi katika ufuatiliaji wako. Kupata siku yako ya kwanza ya hatari, chukua namba ya mzunguko mfupi zaidi toa 18, mfano mzunguko wako mfupi ni siku 27-18 inabaki 9.
    3. Kupata siku yako ya mwisho ya hatari kwenye mzunguko, chukua siku za mznguko wako mrefu toa 11. Mfano mzunguko wako mrefu ilikuwa siku 30-11 inabaki 19.Katika mahesabu hapo juu ni kwamba siku kati ya mzunguko mfupi na mrefu ndizo siku zako za hatari, kwa maaana ya kuanzia siku ya 9 mpaka siku ya 19 ndizo siku zako za hatari.
    4. Kama unataka usishike mimba basi usifanye ngono siku ya 9 ya hedhi mpaka siku ya 19, au utumie condomu.

    Kufatilia joto la mwili-Basalm metabolic rate.

    Joto la mwanamke hushuka masaa 12 mpaka 24 kuelekea mda wa ovulation, baada ya hapo joto huongezeka tena baada ya ovulation. Tukisema ovulation maana yake muda wa yai kutolewa kwenye kikonyo chake na kuwa tayari kw aurutubishaji. Mabadiliko haya ya joto ni madogo sana chini ya nyuzi moja.

    Kupima joto hili tumia kipimajoto maalumu kinachopatikana famasi, na upime kila siku asubuhi kabla ya kuamka. Kutumia joto la mwili kama njia ya kujua siku za hatari, mwanamke anatakiwa asifanye ngono kwenye siku ambazo joto linashuka. Utasubiri masaa 48 mpaka 72 baada ya joto kupanda ndipo ufanye tendo.

    Kufatilia ute wa uzazi.

    ute wa mimba

    Njia hii ya ute inataka kufatilia mabadiliko ya uteute kwenye uke katika siku tofauti za mzunguko wako. Mwanamke atazalisha ute mwingi laini, unaovutika kama yai kwenye siku za hatari. Sasa wewe kama mwanamke unatakiwa ujifunze kufatilia na kutofautisha ute huo kwa kutumia vidole viwili. Ingiza ukeni taratibu kisha fanya kama unavuta kuona kama unavutika. Kama hutaki kushika mimba basi usifanye kabisa tendo kwa siku 3 mpaka 4 tangu uone huo ute ute wa kuvutika.

    Ovulation Kits

    kipimo cha kufatilia ovulation

    Mwanamke anaweza kutumia vifaa malumu vya kufatilia yai kupevuka. Vifaa hivi vina mfanano na kipimo cha mimba cha mkojo ya UPT. Vipimo hivi vinaangalia kiwango cha homoni ya lutenizing(LH) kwenye mkojo. Homoni ya lutenizing inaongezeka masaa 20 mpaka 48 kabla ya ovulation. Vifaa vya kupima vinapatikana kwenye famasi, unaweza kununua package yako ukaweka ndani.

    Utaanza kupima siku mbili mpaka tatu kabla ya siku ambazo unafikiri yai linakarbia kutolewa. Kipimo hichi kama ilivyo kwa kile cha UPT, kinapima mkojo na kunyesha rangi nyekundu. Kama yai limeshatolewa mistari mwili iliyokolea itatokea, na kama bado mstari utakuwa mmoja mwekundu. Kama ovulation imekaribia basi mstari utakuwa umepauka.

    Vipimo hivi kwa kiasi kikubwa hutumika kufatilia yai kupevuka ili mwanamke aweze kushiriki apate mimba, lakini unaweza kuvitumia pia kupanga uzazi ili usishike mimba mapema wakati hujatarajia.

    Withdraw method (kuchomoa uume kabla mbegu hazijatoka)

    Withdraw inahitaji mwanaume kutoa uume haraka kabla mbegu hazijatoka wakati wa tendo. Changamoto ya njia hii ni kwamba wanawaume wachache wanaweza kujizuia na wakatoa uume nje kwasababu ya hisia kali na utamu wa kufika kileleni. Lakini pia mbegu kidogo zinaweza kutoka wakati mwanaume anakarbia kilele na zikasababisha mimba. Njia hii ina ufanisi wa asilimia 75 mpaka 80 katika kuzuia mimba.

    Lactational infertility.

    Njia hii inamaanisha kwamba unapokuwa unanyonyesha mayai yanakuwa hayapevuki kwahivo mimba haitaingia. Wanawake wanaonyonyesha, mayai huanza tena kupevuka week 10 mpaka 12 baada ya kujifungua. Katika miezi sita ya kwanza ambapo mtoto ananyonya pasipo kula chakula kingine, njia hii inakuwa na ufanisi zaidi.

    Mtoto yatakiwa anyonye walau kila baada ya masaa ma4 na usipitishe zaidi ya masaa sita bila kumnyonyesha mtoto. Hakikisha unatumia njia hii miezi 6 tu ya mwanzo baada ya kujifungua. Faida zake ni kwamba huhitaji kutumia kinga yoyote wala njia yoyote ya kemikali ili kuzuia mimba,badala yake ni kunyonyesha tu ipasavyo.

    Njia hii siyo ya uhakika kutumika pasipo kuzingatia njia zingine hasa baada ya miezi 6 kuisha na mtoto kuanza kula. Mwanamke anayenyonysha anaweza kushika mimba pale mtoto akipunguziwa ratiba ya kunyonya kwa siku.

    Kuosha uke na kukojoa baada tu ya tendo

    Njia hii inahitaji mwanamke kila anapomaliza tendo kwenda haraka washroom na kuchuchumaa kisha kunawa na kutoa mbegu na uchafu wote ukeni. Wanawake wengi pia husimama haraka na kukojoa ili mbegu zitoke nje kabla ya kulifikia yai. Njia hizi hazina uhakika hivo hakikisha unatumia na njia ingine kuzuia mimba.

    Kutofanya kabisa tendo

    Hapa mwanamke na mwanaume wanaweza kuamua kutokutana kabisa ili kuepuka mimba. Hii ndio njia pekee yenye uhakika wa asilimia mia kukukinga usishike mimba ambayo hujatarajia. Badala yake kila mmoja anaweza kufanya punyeto ili kujiridhisha.

    Unahitaji maoni na Ushauri? Tuandikie kwa Whatsapp namba 0678626254. Usipige simu namba ni ya whatsapp tu