Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Kubeba Mimba Katika Umri Mkubwa

mimba katika umri mkubwa
mimba uzeeni

Ni umri gani tunasema umeshika mimba uzeeni?

Kuanzia miaka 35 tunasema ni umri mkubwa zaidi wa kushika mimba (advanced martenal age)

Kutokana na sababu mbalimbali, wanawake wanaweza kuamua kuchelewa sana kutafuta mtoto. Hii imekuwa tabia maarufu sana katika miaka ya hivi karibuni. Mabadiliko ya teknologia yamechangia sana. Mfano mtu anaweza kuamua kutunza mayai na mbegu kisha zikatumika hata baada ya miaka mi5 kushika mimba.

Pamoja na teknologia kukua, bado hatari ya kubeba mimba katika umri mkubwa ipo. Changamoto kama mimba kuharibika, kifafa cha mimba, kujifungua kwa upasuaji nk

Kwanini ni hatari kubeba mimba katika umri mkubwa?

Kadiri umri unavosogea, uwezekano wa kuugua magonjwa sugu unaongezeka. Magonjwa kama kisukari, presha ya kupanda na magonjwa ya tezi ya shingo. Hata kama afya yako iko njema kabla ya mimba, unapopata mimba italeta mabadliko ya kukuweka kwenye changamoto.

Wanawake wanaobeba mimba katika umri zaidi ya 35 wapo kwenye hatari ya

  • mimba kutunga nje ya kizazi
  • mimba kutoka mapema
  • kuchelewa kujifungua
  • matatizo ya kondo la nyuma
  • kisukari cha mimba
  • presha ya kupanda
  • kifafa cha mimba
  • kujifungua mapema kabla ya wakati
  • kupungukiwa damu
  • magonjwa ya moyo
  • kuziba mishipa ya damu
  • kuvuja damu nyingi baada ya kuzaa

Changamoto kwa mtoto

Kuna ongezekeno la hatari ya mamatizo ya hitilafu za vinasaba, pale mayai yanapozeeka. Mwanaume yeye anazalisha mbegu mpya kila siku, ila kwa mwanamke ni tofauti.

Mwanamke anazaliwa na mayai yote, hakuna mayai mapya yanayozalishwa tena, ila tu yanapevuka kila mwezi. Mayai haya yanavokaa miaka mingi yanazeeka na kuwa na hitilafu za kivinasaba.

Kwa mtu mzima, mzunguko wa damu kwenye via vya uzazi na kuelekea kwenye kondo la nyuma unapungua, na hivo kupelekea ukuaji hafifu wa mtoto tumboni.

Pia hatari ya kuumwa kwa mjamzito katika umri mkubwa inaongeeka, na kuathiri ukuaji wa mtoto, kupungua majimaji ya mtoto, na kujifungua njiti.

Maandalizi ya kubeba mimba katika umri mkubwa

Wataalamu wa uzazi wanashauri kuweka sawa uzito wako, kufanya mazoezi, kula vizuri na kupunguza stress ni muhimu pale unapotaka kubeba mimba katika miaka 35+

Muone daktari akufanyie vipimo hasa kwa magonjwa ya kisukari, tezi ya shingoni, na presha ya kupanda. Ni muhimu sana kupima magonjwa haya kabla hujashika mimba kwasababu yanaweza kuwepo bila dalili yoyote. Hakikisha unamweleza daktari anayekupima kwamba unajaribu kubeba mimba.

Je mama mtu mzima atapata changamoto gani kwenye kujifungua?

Mjamzito anapokaribia kujifungua, kondo la nyuma huanza kulegea. Hii inamaanisha mishipa ya damu inaanza kuzeeka, na usafirishaji wa chakula na hewa kuelekea kwenye mtoto unapungua. Lengo ni kumuandaa mtoto kuanza kujitegemea kula akitoka nje ya tumbo.

Kitendo hichi kinatokea mapema sana kwa wajawazito wa umri mkubwa. Yaani usafirishaji unapungua mapema kabla ya muda muafaka wa kujifungua. Ndiomaana katika umri huu, mimba ikifika tu wiki 39 na hujapata uchungu, unazalishwa kwa lazima ili kumuokoa mtoto.

Watu wazima wako kwenye uwezekano mkubwa wa kujifungua kwa upasuaji kwasababu wanakosa nguvu ya kusukuma mtoto. Na watoto wanaozaliwa na wazazi wazee, wanaweza kuwa mapigo ya moyo ya tofauti na hivo kujifungua kwa njia ya uke ikawa hatari kwao.

Bofya kusoma kuhusu: Kujifungua kwa upasuaji, ushauri na hatua za kuzingatia

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Hedhi salama

Hedhi Mara Mbili Katika Mwezi

hedhi mara mbili katika mwezi
kalenda ya hedhi

Mzunguko wa hedhi

Hedhi ya kawaida inachukua mzunguko wa siku siku 21 maka 35. Nikisema mzunguko namaanisha jumla ya siku kuanzia ulipopata hedhi mwezi mmoja, mpaka utakapopata hedhi tena katika mwezi unaofata. Makala hii itaongelea tatizo la kupata hedhi mara mbili katika mwezi na nini cha kufanya.

Japo siyo kawaida kupata mizunguko tofauti kila mwezi. Baadhi ya mizunguko yaweza kuwa mifupi au mirefu kuliko mingine, na hivo kupelekea upate hedhi mara mbili katika mwezi.

Tazama na dalili zingine

Katika nyakati nyingi kupata hedhi mara mbili ndani ya mwezi mmoja yaweza isiwe tatizo. Lakini kama inatokea kwa kujirudia ni muhimu kutazama na dalili zingine zinazoambatana. Endelea kusoma zaidi ili kujifunza kuhusu changamoto ya hedhi mara mbili katika mwezi

Hedhi mara mbili katika mwezi kwa mara ya kwanza

Watu wenye mzunguko mfupi mara nyingi sana wanapata hedhi mwanzoni na mwishoni mwa mwezi. Kwa mtu mwenye mzunguko wa kawaida wa siku 28 au zaidi, akipata hedhi mara mbili lazima ashituke.

Kumbuka hedhi isipotoka kwa wakati inaashiria changamoto ya kiafya. Ni ni rahisi sana kuchanganya hedhi na bleed ingine. Waweza kudhani ni hedhi kumbe unatokwa na damu tu kutokana na changamoto fulani.

Changamoto zinazoweza kupelekea bleed isiyo ya hedhi ni pamoja na

Mimba- mimba inapojishikiza kwenye ukuta wa kizazi yaweza kupelekea bleed. Ugonjwa wa zinaa: Magonjwa ya ngono yanaweza kupelekea upate bleed kidogo na kutokwa na uchafu usio wa kawaida ukeni.

Mimba kuharibika-Mimba inapoharbika inaambatana na maumivu makali na kutokwa na mabonge ya damu. Ni muhimu kwenda hospitali mapema ikiwa una mimba na umeanza kuona damu.

Mabadiliko ya uzito– Mazoezi kupita kiasi na mabadiliko makubwa ya uzito wa mwili yanaweza kupelekea hedhi mara mbili.

Uzazi wa mpango wa kisasa-Hedhi kuvurugika na kutoka mara mbili inatokea sana kwa wanaotumia njia za kisasa kuzuia mimba , mfano sindano, njiti na vidonge

Vimbe kwenye mlango wa kizazi na ukuta wa kizazi: Hizi ni vimbe ambazo siyo saratani kwenye kuta za mlango wa kizazi na kwenye ukuta wa kizazi, ambazo zaweza kupelekea upate hedhi zaidi ya mara moja.

Saratani ya mlango wa kizazi: kutokwa damu yaweza kuashiria uwepo wa saratani

Tofauti kati ya damu ya hedhi na bleed ya tatizo la via vya uzazi

Hizi dondoo zitakusaidia kujua kama damu unayopata ni hedhi ama siyo hedhi

Kama ni hedhi ya kawaida itakulazimu kubadili pedi au tampon kila baada ya masaa kadhaa. Na damu kawaida inakuwa nyekundu nzito au ya kungaa, brown au pink

Kama ni matone ya damu ambayo siyo hedhi, haitahitaji kubadili pedi au tamponi mara kwa mara, unaweza kutumia pedi moja tu kwa siku. Damu yake yaweza kuwa ya pick, brown na inakata mapema ndani ya siku moja au mbili

Chanzo kikubwa cha mzunguko mfupi na hedhi mara mbili katika mwezi

Nini kinapelekea hedhi mara mbili katika mwezi? inaweza kutokana na mzunguko mfupi ama changamoto ya kiafya inayopelekea bleed ukeni.

Baadhi ya mambo yanayopelekea hedhi mara mbili ni pamoja na

1.Kukaribia kukoma hedhi-Perimenopause

Perimenopause ni kipindi ambacho mwanamke anakarbia kukoma hedhi yake, wakati ambapo kunatokea mabadiliko makubwa ya homoni. Kipindi hichi waweza kupata hedhi mara mbili ndani ya mwezi mmoja. Perimenopasue inatofautiana kwa kila mwanamke.

Kuna wengine inachukua hata miaka 10 ndipo hedhi inakoma. Wakati wa kipindi hiki kuelekea kukoma, waweza kupata hedhi nzito sana, kuvusha miezi kadhaa bila hedhi, mzunguko kuwa mrefu , hedhi nyepesi sana. Menopause ndio kukoma hedhi kwenyewe. Mwanamke anakoma hedhi endapo atakosa hedhi kwa miezi 12 mfululizo.

2.Fibroids

Hizi ni vimbe zinazotokea kwenye kizazi. Ni vimbe zisizo saratani, na zaweza kuleta hedhi nzito, au ukavusha kabisa hedhi. Dalili zingine za fibroids ni pamoja na

  • kupata mkojo mara kwa mara
  • kuhisi uzito eneo la nyonga
  • maumivu chini ya mgongo
  • maumivu wakati wa tendo

Daktari atagundua kama una fibroids kwa kukufanyia kipimo cha utrasound.

3.Magonjwa ya tezi ya shingoni

Tezi huu huitwa thyroid, inakaa shingoni na ina umbo kama la kipepeo. Kazi ya tezi hii ni kuzalisha homoni ambazo zinaratibu mpangilio wa hedhi yako. Dalili za kwamba kuna tatizo kwenye tezi ya shingo ni pamoja na

  • kuhisi baridi mda wote
  • kuongezeka uzito
  • tumbo kujaa
  • kupungua mapigo ya moyo
  • kutoka na damu nyingi ya hedhi

Kwa upande mwingine ikiwa tezi yako inafanya kazi kupita kiasi utaanza kupata dalili hizi

  • kuhisi joto mda wote
  • macho kuvimba
  • moyo kwenda mbio sana
  • kukosa usingizi
  • kuharisha na
  • macho kuvimba

Hakikisha unaenda hospital, endapo utaanza kupata dalili hizi za tezi ya shingo.

Madhara zaidi ya kupata hedhi mara mbili

Watu wanaotoka kwenye familia zenye historia ya kuugua vimbe kwenye kizazi na kukoma hedhi mapema , wapo kwenye hatari zaidi ya kupata hili tatizo la hedhi mara mbili katika mwezi. Moja ya changamoto utakayopata kutokana na kupata hedhi mara mbili ni kupungukiwa damu. Dalili hizi zinaonesha kwamba umepungukiwa na damu.

  • mwili kuchoka sana
  • kizunguzungu
  • mapigo ya moyo kubadilika
  • kukosa pumzi
  • kuumwa sana kichwa

Je kuna umuhimu wa dawa kutibu hedhi mara mbili?

Hedhi mara mbili siyo tatizo ikiwa mzunguko wako ni mfupi. Japo ni muhimu sana kumuona daktari endapo kama utapata dalili hizi hapa chini

  • hedhi mara mbili kwa miezi mi2 au mi3 mfululizo
  • maumivu wakati wa tendo
  • hedhi nzito ya mabonge
  • damu ya kuganda
  • maumivu chini ya kitovu hasa kama maumivu hayaishi
  • maumivu makali kwenye hedhi
  • kupata matone ya damu katikati ya mzunguko ambayo yanajirudia mwezi unaofata

Kwa binti mdogo hakuna tatizo

Matibabu ya tatizo hili ya kupata hedhi mara mbili katika mwezi mmoja, yanategemea na chanzo cha tatizo. Watu wenye mzunguko mfupi au wanaopata hili tatizo kwenye miaka ya mwanzo ya kubalehe, hawahitaji tiba tatizo laweza kuisha lenyewe.

Tiba inalenga Chanzo cha Tatizo

Daktari anaweza kupendekeza akupe dawa za kurekebisha homoni zile za kupanga uzazi. Kama tayari unatumia dawa za kisasa za uzazi wa mpango, na unahisi ndio chanzo cha tatizo, mjulishe daktari ili akubadilishie njia ingine.

Kwa tatizo la tezi ya shingo: daktari anaweza kupendekeza vipimo zaidi na kukupa dawa kwa tatizo hili

Kama unakarbia kukoma hedhi: kuna dawa za hormone utapewa kupunguza ukali wa tatizo

Kwa vimbe yani fibroids: daktari anaweza kukupa dawa, ama akapendekeza upasuaji, kulingana na ukubwa wa tatizo.

Kubadili mtindo wako wa maisha pia utasaidia kurekebisha homoni zako, mfano kama una uzito mkubwa na kitambi, anza kufanya mazoezi na kupunguza vyakula vya sukari.

Tumia Evecare Kurekebisha hedhi yako ndani ya mwezi mmoja

evecare

Evecare ni dawa asili na imetengenezwa nchini India kupitia mimea ua Ashoka, Asaparagus na lodh tree. Kwa miaka zaidi ya mitano ambayo tumekuwa tukihudumia wagonjwa wetu wa matatizo ya hedhi na homoni, tumepokea shuhuda lukuki.

Dawa itakusaidia kurekebisha homoni na mzunguko wa hedhi ili uanze kupata hedhi vizuri. Evecare inakuwa na vidonge 30, unameza vidonge viwili kila siku kwa muda wa wiki mbili.

Gharama ni Tsh 75,0000/=. Kabla ya kukupa dawa, daktari atakusikiliza kwanza na kujua chanzo cha tatizo lako.

angalizo

Kuna wimbi kubwa la wajasiliamali mitandaoni wanauza vidonge fake vya evecare, tena wanauza kwa bei rahisi sana. Watu hao siyo madaktari wala siyo wataalamu wa afya na wanauza bidhaa feki ambazo ni hatari wa afya yako. Wengi wao hawana hata ofisi, ukipata madhara unakosa pa kuuliza. Kuwa makini na watu hao, wamejaa sana insta na fb

Ukiwa na maswali na uhitaji wa tiba Tuandikie whatsapp kwa namba 0678626254. Tupo Dar- Mwembechai

Bofya kusoma: Njia salama za kupunguza maumivu kipindi cha hedhi

Categories
Magonjwa ya Kuambukiza

Tetekuwanga

tetekuwanga
tetekuwanga

Nini maana ya Tetekuwanga?

Tetekuwanga ni ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza. Ugonjwa unasababishwa na kirusi anayeitwa varicella-zoster. Watu wengi wanaugua tetekuwanga wakiwa wadogo, endapo hawakupata chanjo.

Mtoto anayeugua tetekuwanga anaweza kumwambukiza mtoto mwingine kwa urahisi sana. Kwa sasa tatizo siyo kubwa ukilinganisha na zamani kwani watoto sasa wanaweza kuachanjwa ili wasipate tetekuwanga.

Huwezi kuugua tetekuwanga mara mbili

Ukishaugua tetekuwanga huwezi tena kuugua maisha yako yote hata kama ukigusana na mgonjwa. Kama hujachanja unaweza kuugua tetekuwanga katika umri wowote ule.

Watu wazima wanaougua tetekuwanga wanakua wadhaifu sana na ugonjwa ukawapelekesha mno ukilinganisha na watoto. Ni bora kuugua tetekuwanga ukiwa mtoto kuliko kuugua ukubwani, au upate chanjo kabisa ili uisugue.

Tetekuwanga inaambukizwaje?

Unaweza kupata tetekuwanga kwa

  • kugusana na mgonwa mwenye tatizo
  • kuvuta hewa ya mgonjwa watetekuwanga au majimaji ya kooni na mafua
  • kugusa majimaji ya mgonjwa kwenye pua zako, mdomo na macho

Je kuna uhusiano gani kati ya tetekuwanga na mkanda wa jeshi?

Ukishaugua tetekuwanga, wale virusi wanabaki mwilini lakini hawasababishi tena tetekuwanga. Lakini siku virusi hawa wakiibuka wataleta ugonjwa mwingine unaoitwa mkanda wa jeshi ama shingles. Kwahivo mkanda wa jeshi hauambukizwi bali ni virusi wako wa tetekuwanga ulougua zamani ndo wanakuletea ugonjwa mpya.

Kumbuka watu wenye mkanda wa jeshi hawawezi kumuambukiza mtu mkdanda wa jeshi, basi wanaweza kumpa tetekuwanga, endapo huyo mtu hakuwahi kuugua tetekuwanga. Mkanda wa jeshi nao huisha wenyewe ndani ya week .

Dalili za tetekuwanga

Dalili za tetekuwanga hazijifichagi, ni rahisi sana kumtambua mgonjwa wa tetekuwanga. Dalili hizi ni kama

  • Homa
  • Kuhisi uchovu
  • kichwa kuuma
  • Maumivu ya tumbo
  • Malengelenge kwenye ngozi yanayowasha na kutoa maji
  • Makovu baada ya lengelenge kutoboka
  • Ngozi yenye madoadoa

Vipimo kugundua uwepo wa tetekuwanga

Kwa kutumia tu macho, muhudumu wa afya anaweza kugundua kwamba unaumwa tetekuwanga.

matibabu na huduma kwa mgonjwa wa tetekuwanga

Nawezaje kumsaidia mwanangu anayeumwa tetekuwanga?
Hakikisha mtoto anapata mda mwingi wa kupumzika na kunywa maji ya kutosha. tetekuwanga huwa inapona yenyewe ndani ya week 1 au mbili. Kumsaidia mtoto na muwasho unaweza kufanya haya

  • weka nguo yenye majimaji baridi kwenye lengelenge
  • hakikisha mwanao yupo eneo lenye ubaridi
  • ongea na mwanao asitoboea lengelenge kama mtoto mdogo sana mkate kucha ili ajijikune
  • unaweza kumpaka lotion maalumu au ukampa dawa zenye kiamabata cha antihistimine- nunua pharmacy
  • mwogeshe mwanao kwa maji baridi mara kwa mara. Mfute mtoto kwa taulo kama unakanda mwili, usifute kwa kusugua.

Usimpe mtoto dawa za asprin. Hizi zinaweza kumletea mtoto shida hasa mwenye homa. Kama huna uhakika dawa ipi ya kumpa mwanao, nenda pharmacy jieleze utapewa dawa sahihi.

Je kuna madhara zaidi yanaweza kutokea kwa mtoto mwenye tetekuwanga?

Changamoto kubwa zinazoweza kujitokeza kutokana na tetekuwanga ni pamoja na

  • bakteria kushambulia ngozi, damu na tishu laini
  • Nimonia- yani mapafu kujaa maji
  • mwili kupungukiwa maji kupita kiasi
  • ini kuathirika
  • damu kuganda

Nani anaweza kuugua zaidi na kulemewa na tetekuwanga?

Watu wenye afya njema, wanapougua tetekuwanga, huwa haiwapelekeshi sana. Japo wa watoto wadogo sana kuugua tetekuwanga inaweza kuwaletea shida zaidi, pia wenye mimba, wenye kinga dhaifu . Wagonjwa wa Ukimwi, saratani na wanapata tiba ya mionzi wanalemewa sana na tetekuwanga

Je tetekuwanga yaweza kuua mtu?

Ni mara chache sana tetekuwanga ikahatarisha maisha ya mtu. Watu wengi hupona mapema ndani ya wiki mbili baada ya kuugua. Japo wapo watu waliowahi kufa kwasababu ya tetekuwanga.

Je mwanangu anaweza kupata chanjo ya tetekuwanga?

Jibu ni ndio kuna chanjo ya tetekuwanga, ongea na mtoa huduma hospital atakupa maelekezo.

Je watu wazima wanaweza kuugua tetekuwanga?

Mtoto akishaugua tetekuwanga, mwili wake unapambana na virusi hao na kutengeneza kinga ya kudumu. Kinga hii inakaa mwilini miaka yote ya uhai wako, na itapambana na virusi wageni wataakaoingia siku zijazo.

Ni lini unatakiwa kumwona daktari?

Nenda hospital haraka endapo mtoto wako anapata dalili za

  • ana malengelenge kwe nye macho
  • kuumwa sana kichwa
    • ana malengelenge makubwa yanayotoa usaha
    • anashindwa kupumua vizuri

    Bofya kusoma kuhusu: kwanini unaugua kaswende sugu

    Categories
    Afya ya mwanamke na uzazi

    Dalili Mbaya Kwa Mjamzito

    dalili mbaya kwa mjamzito
    mjamzito

    Kipindi cha ujauzito kinaambatana na mabadiliko mengi sana ya mwili, pamoja na mabadiliko ya kimaisha pia kwenye kujiandaa kumpokea mwanafamilia mpya. Ni kipindi pia ambacho waweza kuwa na hofu sana kuhusu mimba yako, na utakuwa mwangalifu sana. Hapa chini ni maelezo a kina juu ya dalili mbaya kwa mjamzito na hatua za kuchukua mapema.

    Mabadiliko mengi ambayo utayaona mwilini mwako, jua kwamba ni kawaida na ni lazima uyapitie. Dalili nyingi mfano kuumwa nyonga, tumbo kuunguruma, kukosa choo, kizunguzungu nk zinakuja na kupotea.

    Je dalili mbaya zinaisha mapema?

    Baadhi ya dalili waweza kukaa nazo mpaka siku unajifungua, na kuna zingine zinakuja na kupotea. Hapo ndipo yatakiwa kuwa makini kwa kila dalili unazopata. Kuna dalili zingine hatari ambazo haitakiwi upitishe hata siku 1 bila kwenda hospital, endapo utaziona.

    Dalili za Kawaida Ambazo siyo hatarishi

    Dalili nyingi kati ya hizi siyo hatari, na haitakiwi kupata hofu sana. Japo unaruhusiwa kumpigia daktari wako na kumuuliza ili upate uhakika zaidi. Dalili nyingi ya hizi zinajitokeza mimba ikiwa changa, na zingine baadae

    • kutapika
    • kutokwa na uchafu mwingi ukeni
    • kichwa kuuma
    • uchofu na kizunguzungu
    • maumivu yanayokuja kwa haraka na kupotea
    • kupungua uzito
    • kuhisi joto kali
    • kushindwa kuvuta hewa vizuri
    • mawazo, na kupata hofu ana kushindwa kufanya kazi zako vizuri

    Dalili mbaya kwa mjamzito.

    Dalili hizi zinatokea mda wowote wa ujauzito. Japo mimba inapokuwa changa zaidi ndipo hatari ya mimba kuharibika inakuwa kubwa, ila watakiwa kuwa makini kipindi chote.

    Dalili hatarishi ni pamoja na

    1.Kuvuja damu

    Kitendo cha kutokwa damu/bleed ukiwa na mimba siyo ishara nzuri hata kidogo, ni kiashiria kwamba kuna tatizo. ikiwa unatokwa damu nzito, na una maumivu makali ya tumbo upande wa kushoto au kulia na unajihisi kuishiwa nguvu, hii inaweza kuashiria mimba imetunga nje ya kizazi.

    Mimba ikitunga nje ya kiazi haiwezi kukua, inatakiwa kuondolewa ma[pema kwa upasuaji. Mimba hiozi huitwa ecopic, endapo haitaondolewa mapema, mgonjwa anaweza kupoteza maisha.

    Kama damu zinatoka nzito, tumbo linauma kuzunguka kitovu, hii inaashiria mimba imeharbika, na hii inatokea zaidi mimba ikiwa chini ya wiki 12. Sisemi kwamba mimba kubwa kubwa haziharbiki, hapana. Ni kwamba mimba nyingi zinaharbika zikiwa changa.

    2.Kutapika na kichefuchefu kupita kiasi

    Kwa mjamzito ni kawaida kupata kichefuchefu, lakini kama tatizo ni kubwa inaweza kuashiria shida kubwa ya kiafya. Kama unashindwa mpaka kula au kunywa chochote, hapo utaishiwa maji. Na kuishiwa maji inaweza kuhatarisha ujauzito wako.

    Kama unahisi kizunguzungu kinakutesa sana, ongea na daktari atakupa dawa ya kupunguza makali yake.

    3.Mtoto kuacha kucheza

    Mtoto kupunguza kucheza inaweza kuashiria kachoka, hii ni kawaida isikupe hofu. ila kama hachezi kabisa kwa siku nzima, hapo kuna shida kubwa.

    Sasa ili kugundua tatizo, inashauriwa ukiona mtoto hachezi mda mefu, jaribu unywe kitu cha baridi. Kisha lala kwa ubavu, na fatilia kama mtoto ataanza kucheza.

    Mpigie daktari, ama nenda hospital haraka endapo utagundua mtoto ameacha kucheza. Daktari atafanya vipimo kuona kama kuna hatari yoyote.

    4.Kupata uchungu mapema mimba ya miezi 7

    Kupata uchungu na mimba haijatimiza umri wa kujifungua, ni dalili mbaya. Kama tumbo linavuta na kuachia na hii hali itokee mara chache na kuisha hilo ni kawaida. Kwani hata ukifika kileleni baada ya tendo, lazima utahisi tumbo kuvuta.

    Lakini endapo tumbo linavuta na kuachia, kisha baada ya dakika 10 linaanza tena kuvuta na kuachia, hiyo ni ishara ya kuelekea kuzaa njiti. Mpigie daktari mapema endapo utaona hali hii.

    5.Chupa kupasuka mapema ni dalili mbaya kwa mjamzito

    Tunaposema chupa, tunamaanisha ule mfuko unaobeba mtoto. Mfuko huu unakuwa na maji yanayomlinda mtoto asiumie. Mfuko unapasuka pale mama akianza uchungu na yupo tayari kujifungua. Endapo mfuko utapasuka mapema na mtoto akaendelea kubaki tumboni, mtoto atakosa hewa na kupoteza uhai.

    Maji haya ni tofauti na mkojo, kwani hayaishi mapema yakianza kuvuja. Kwahivo tazama ukiona dalili ya kuvuja maji ukeni, tena maji mengi, nenda hospitali haraka.

    6.Maumivu makali yasiyoisha kwenye kichwa, tumbo na kushindwa kuona vizuri

    Hizi dalili zinaweza kuashiri kupanda kwa presha kitaalamu (preeclampsia) . Hili ni tatizo baya na linaweza kupelekea kifafa cha mimba. Tatizo linaambatana na dalili za presha kupanda na protini nyingi kwenye mkojo, hasa inatokea baada ya week 20 za ujauzito. Hakikisha unaenda hospital haraka endapo unahisi dalili hizo.

    Nawezaje kujizuia nisipate dalili mbaya kwa ujauzito wangu?

    Ukweli ni kwamba ni vigumu sana kujizuia asilimia zote kupata dalili mbaya kwenye ujauzito. Lakini kuna vitu vichache unaweza kufanya kupunguza hatari ya mimba kuharibika kabla ya muda wake.

    Hudhuria clinic zote na upate dawa za kuongeza damu mapema kabisa. Unapoenda clinic daktari atachukua historia yako na kukwambia endapo upo kwenye kundi hatarishi. Utapewa ushauri wa kina kuhusu lishe na afya ya akili pamoja na afya ya tendo la ndoa.

    Bofya kusoma kuhusu kifafa cha mimba

    Categories
    Nguvu za Kiume Tendo la ndoa

    Viagra,Matumizi, Faida na Madhara

    viagra
    viagra

    Naamini umekuwa ukisikia hili neno kwa muda mrefu sana, pasipo kujua undani wa dawa hii ya viagra. Leo nitakweleza kwa undani kuhusu viagra, ikiwemo matumizi, upatikanaji, madhara yake ya mda mrefu na kitu gani waweza kutumia kama mbadala wa viagra.

    Viagra ni kutu gani?

    Endapo unawahi kufika kileleni ama unashindwa kusimamisha uume vizuri wakati wa tendo la ndoa. Ukienda hospitali, daktari anaweza kukuandikia utumie viagra. Hii ni dawa daktari anakwandikia kusaidia nguvu za kiume.

    Viagra inakuja katika mfumo wa vidonge na hutakiwi kutumia mpaka uandikiwe na daktari, na utatumia kabla ya tendo siyo kila siku.

    Viagra inafanyaje kazi?

    Uume unasimama pale protini inayoitwa cyclic guanosine monophosphate(cGMP) inapotolewa kwenye damu, na kupelekea mzunguko mkubwa wa damu kuelekea kwenye uume. Mzunguko wa damu ukiwa mkubwa kuelekea kwenye uume hapo utaweza kudindisha vizuri na kupiga show mda mrefu bila kuchoka.

    Je inachukua mda gani kwa Viagra kufanya kazi?

    Viagra inaleta matokeo haraka sana baada tu ya kumeza dozi yako. Viagra inafanya kazi ndani ya lisaa. Kwa watu wachache inaweza kuanza kazi ndani ya nusu saa tu baada ya kumeza, na wengine mpaka baada ya masaa ma4.

    Je vipi kama Viagra haitafanya kazi?

    Endapo viagra haitafanya kazi, hakikisha unamjulisha daktari aliyekuhudumia. Daktari anaweza kupendekeza utumie dozi kubwa zaidi ya dawa, kisha ataendelea kukufatilia kama dozi hiyo kubwa imefanya kazi.

    Je Nguvu a Viagra inaisha Ndani Ya Muda Gani?

    Viagra inafanya kazi vizuri ndani ya masaa kadhaa baada ya kumeza. Kwa watu wengi dawa inafanya kazi ndani ya lisaa tu na kwa tu wachache dawa itaendelea kukupa nguvu mpaka masaa ma4. Kadiri mda unavosogea nguvu ya viagra inapungua na baadae kuisha. Hapo utahitaji kumeza tena ikiwa unataka kushiriki.

    Kwahivo ieleweke hii siyo tiba ya tatizo lako. Ni booster tu ya mda mfupi ili ufurahie tendo, kisha utarudi kule kule.

    Je Vigra inatumika Kwa Wanawake?

    Pengine unajiuliza je mwanamke naye anatumia kuimarisha nguvu za kike? Dawa hii imethibitishwa kutumika kwa wanaume tu kwenye tatizo la uume kutosimama imara.

    Je Kuna Matokeo/madhara Gani Kutumia Viagra?

    Kama ilivo kwa dawa zingine zote, Viagra yaweza kuwa na madhara madogo na hata makubwa pia. Hapa chini ni list ya madhara yanayoweza kujitokeza. Kumbuka madhara haya yanatofautiana na umri wa mtu. Magonjwa mengine aliyonayo na pia dawa anazotumia kwa sasa.

    Dalili/matokeo Ya Mda Mfupi

    Dalili mbaya au matokeo yanaweza kujitokeza baada ya kumeza viagra ni pamoja na

    • kichwa kuuma
    • makamasi kwenye koo
    • maumivu chini ya mgongo na misuli
    • kizunguzungu
    • kiungulia na
    • mabadiliko kweneye kuona

    Madhara Makubwa ya Viagra

    Madhara makubwa yanaweza kujitokeza ukimeza viagra, ila usiogope, hayajitokezi mara kwa mara. ikiwa umepata matokeo haya, mweleze daktari mapema. Matokeo haya ni pamoja na

    • kushindwa kuona
    • kupata aleji
    • presha kushuka sana
    • kupata shambulizi la moyo
    • kupungua uwezo wa kusikia na pia
    • kuumia sana wakati wa kukojoa mbegu
    • uume kukosa nguvu kabisa kwenye tendo hasa ukitumia viagra kwa mda mrefu

    Jinsi ya Kutumia Viagra

    Kwasababu dawa unaandikiwa hospitali, ni lazima daktari, ni lazima akwandikie matumizi ya dawa. Muhimu sana kufatilia maelekezo uliopewa na daktari wako. Viagra zinapatikana wa nguvu za ujazo tofauti, yani mg 25, mg 50 na mg 100.

    Muda gani unatakiwa kumeza viagra

    Viagra inatakiwa kumezwa pale tu inapohitajika, yani lisaa limoja kabla ya kwenda kufanya ngono. Haitakiwi kumezwa mara kwa mara. Hutakiwi kabisa kumeza viagra zaidi ya mara moja kwa siku.

    Maswali yanayoulizwa mara kwa mara kuhusu viagra

    1.Je viagra inaongeza hamu ya tendo la ndoa?

    Jibu ni hapana, viagra haiongezi hamu ya tendo. Unatakuwa uwe na msisimko tayari wa kuifanya tendo ili viagra ifanye kazi . Kazi ya viagra ni kuongeza msukumo wa damu kuelekea kwenye uume ili usimame vizuri kwenye tendo.

    2.Je viagra inazuia kumwaga mbegu? au kukufanya umwage mbegu mara nyingi zaidi?

    inawezekana kabisa viagra kubadili mfumo wa utoaji mbegu kama ilivokuwa mwanzo/ mabadiliko haya ni pamoja na

    • kukuzuia kumwaga mbegu
    • kufanya umwage mbegu mara nyingi zaidi

    Kama unapata changamoto baada ya kutumia viagra, ongea na daktari aliyekuhudumia.

    3.Je Viagra inafanya uume uendelee kusimama hata baada ya kumwaga mbegu?

    Ndio, viagra yaweza kukufanya uendelee kusimamisha hata baada ya kumwaga mbegu. Lakini endapo uume utasimama zaidi ya masaa ma4 muone daktari haraka. Hii inaweza kuwa hali ya hatari inayohitaji usaidizi wa haraka, maana itaharibu uume wako.

    4.Je Viagra inaongeza ukubwa wa uume wako?

    Hapana, ni ngumu sana viagra kuongeza ukubwa wa uume wako kuliko kawaida. Uume utavimba tu wakati una hisia za tendo, ukimaliza tendo uume unarudi kawaida. Viagra itafanya tu uume usimame na uwe imara kuliko kawaida ila siyo kuongeza maumbile.

    Makundi ya watu wasiotakiwa kutumia Viagra

    Viagra yaweza isikufae endapo una matatizo baadhi ya kiafya. Ongea na daktari vizuri na mweleze historia yako yote kabla hujaanza kumeza viagra. Magonjwa ama changamoto hizo ni pamoja na

    • magonjwaya moyo, stroke ama umefanyiwa upasuaji wa moyo ndani ya miezi 6
    • uume wako una maumbile yasiyo kawaida , mfano umejikunja sana, ama unapata mjeraha mara kwa mara.
    • Magonjwa ya damu kama sickle cell
    • magonjwa ya moyo
    • una presha ya kushuka
    • una changamoto za kutokwa damu mfano puani na kwingine kwenye matundu
    • vidonda vya tumbo: Hakikisha unamweleza daktari ikiwa unaumwa vidonda tumbo
    • magonjwa ya figo na ini: kama figo na ini zina hitilafu, kumeza dawa yaweza kuongeza sumu mwilini na kuleta shida zaidi.

    Viagra Na Pombe

    Kunywa viagra na huku unaendelea na pombe yaweza kuleta shida ya kupungua zaidi kwa presha ya damu. Kama wewe ni mnywaji wa pombe hakikisha unamjulisha daktari kuhusu hilo mapema.

    Bofya kusoma kuhusu; Kwanini unawahi kufika kileleni na kushindwa kurudia tendo