Categories
Magonjwa ya viungo

Miguu kujaa maji, Chanzo, Ushauri na Tiba

miguu kujaa maji
mguu uliovimba

Nini maana ya miguu kujaa maji?

Kujaa maji kitaalamu edema, ni kitendo cha kuvimba kwa maneneo mbalimbali ya mwili. Unaweza kujaa maji kwenye miguu, enka, usoi na hata mikono. Yatokana na kukusanyika kwa majimaji yasiyohitajika eneo husika. Makala yetu itajikita zaidi kwenye miguu kujaa maji na nini kifanyike kutibu shida yako.

Miguu yako inavimba kwa sababu kubwa mbili

1.Maji kujikusanya(edema)

Hapa inatokea pale tishu au mishipa ya damu inaposhikiia maji mengi kuliko inavotakiwa. Kukaa mda mrefu wakati unafanya kazi, au ukiwa kwenye ndege, mabadiliko ya homoni wakati wa mimba hata kusimama mda mrefu yaweza kupelekea hali hii.

Mwili wako kumbuka umetengenezwa kwa maji asilimia 60. Sasa inapotokea hakuna uwiano mzuri wa amji, inapelekea kiwango fulani cha maji kuegemea eneo lingine zaidi.

2.Kututumka(inflammation)

Hii inatokea pale tishu za miguu zinapochokozwa na kitu kigeni na hivo kuvimba. Ni kawaida eneo la mwili kuvimba pale kunapotokea hitilafu. Endapo utavunjika mfupa eneo la maungio, ama kuna baridi yabisi, lazima eneo husika livimbe kukupa ishara kwamba kuna shida.

Magonjwa na changamoto zinapelekea miguu kujaa maji

1.Moyo kufeli

Hii inatokea pale moyo wako unapokuwa dhaifu katika kupump damu kwenda maeneo mbalimbali ya mwili. Dalili zingine za kufeli kwa moyo ni pamoja na

  • pumzi kukata na kushindwa kupumua vizuri
  • mwili kuchoka sana
  • kukohoa kupita kiasi

2.Matatizo kwenye mishipa ya damu

Matatizo makubwa mawili kwenye mishipa ya damu ambayo kitaalamu tunaiata Deep vein thrombosis(DVT) na thrombophlebits yanaweza kupelekea miguu kuvimba. Ukiwa na hizi changamoto maana yake kuna kipande cha damu kimegamda kwenye mshipa na hivo kuzuia usafirishaji.

Muone daktari mapema endapo utaona dalili

  • maumivu kwenye miguu na mguu kuwa laini
  • ngozi kuwa nyekundu au blue
  • ngozi yenye hali ya joto kuliko kawaida
  • maumivu baada ya kukaa au kusimama mda mrefu
  • ngozi kuwa kavu na inayobabuka na
  • malengelenge kwenye ngozi ya mguu

3.Magonjwa ya figo

Figo zinapopata hitilafu kwa mda mrefu, zinafeli kufanya kazi yake ya kuchuja maji. Na matokeo yake kiwango kikubwa cha maji kinahifadhiwa kwenye mwili badala ya kutolewa nje.

Maji yanayobaki yanaweza kujikusanya kwenye miguu na mikono. Ukiwa na tatizo kwenye figo na kisha maji yamejaa waweza pia kupata dalili zingine kama

  • mwili kuishiwa nguvu
  • kushindwa kupumua vizuri
  • kiu kupita kiasi
  • kichefuchefu
  • kuwashwa na kutoa damu

4.Mimba

Kwa wajawazito wengi, mimba inapofikia wiki 25, inakuwa ni mimba kubwa na inaleta mgandamizo kwenye mishipa yako ya damu. Mgandamizo huu unapunguza kiwango cha damu kinachosafiri na hivo kupelekea miguu na mikono kujaa maji.

Endapo una mimba na umeona dalili hizi hakikisha unaenda hospitali haraka, kwani siyo dalili njema. Dalili mbaya ni

  • kuvimba kupita kiasi hasa maeneo ya macho
  • maumivu ya kichwa kupita kiasi
  • macho kushindwa kuhimili mwanga na kushindwa kuona vizuri

Kama umepata dalili za miguu kuvimba, kukosa pumzi baada tu ya kujifungua, ongea na daktari kama unaweza kuwa na changamoto ya moyo. Atakupangia vipimo na utapata uhakika wa afya yako.

5.Baridi yabisi na magonjwa mengine ya joints

Magonjwa haya yamegawanyika: Nitayaelezea kila moja na dalili zake

Gout

Gout ni ugonjwa unaosababishwa na kuongezeka kwa uric acid kwenye damu. Acid hii inapojikusanya maeneo ya maungio huleta maumivu makali sana na kupelekea eneo hilo kuvimba. Utajiona kama una gout endapo unaamka asbhi, dole gumba la mguuni lina maumivu makali kama sindano inachoma.

Osteoarthritis

Hii ni aina ya baridi yabisi ambapo mgonjwa anapata maumivu na kuvimba kutokana na kuchoka kwa maungio. Hii inawapat zaidi wazee

Rheumatoid arthritis

Ugonjwa huu ni aina ya baridi yabisi ambapo kinga ya mwili inapambana na tishu za mwili. Ugonjwa unaweza kumtokea mtu wa umri wowote.

Majeraha

Kama mfupa umevunjika, au enka kuteguka, inaweza kupelekea eneo hilo kuvimba. hii ni namna ya kawaida kabisa ya mwili kuvimba kutokana na shambulizi. Kitendo cha kuvimba ni ishara kwamba mwili unapambana kulitibu eneo husika.

Cellulitis

Haya ni maambukizi ya bakteria kwenye eneo la ndani la ngozi. Dalili zingine za cellulitis ukiacha kuvimba ni pamoja na

  • homa
  • maumivu ya ngozi
  • eneo la ngozi kutengeneza dimple yani mbonyeo
  • ngozi kuwa laini sana kupita kiasi
  • wekundu kwenye ngozi unaoongezeka kila siku

Nini cha kufanya endapo miguu yangu imevimba?

Unaweza kujaribu huduma hizi za kwanza wakati ukijiandaa kwenda hospitali

  1. Punguza vyakula vyenye chunvi
  2. Weka ratiba ya kufanya mazoezi mepesi kila siku
  3. Usikae mda mrefu bila kusimama na kutembea
  4. Kama una uzito mkubwa na kitambi, lenga kurekebisha uzito wako kwanza

Lakini kwasbaabu kuvimba kwa miguu kunaweza kuashiria tatizo kubwa la kiafya, usipuuze dalili zake. Hakikisha unaenda hospitali mapema kupimwa kujua shida iko wapi.

Bofya kusoma kuhusu: Miguu kuwaka moto

Categories
Magonjwa ya viungo

Miguu kuwaka moto

miguu kuwaka moto
ganzi mguuni

Nini maana ya miguu kuwaka moto?

Miguu kuwaka moto ni tatizo kubwa sana kwa sasa. Maumivu haya yanaweza kuwa ya mda mfupi au yakakaa mda mrefu bila kuisha. Miguu yako itahisi hali ya kuungua na kufa ganzi. Maumivu huwa makali sana hasa nyakati za usiku.

Matibabu ya changamoto ya miguu kuwaka moto yanategemea na chazo cha tatizo lako. Endelea kusoma zaidi makala hii ili ujue chanzo cha tatizo lako na tiba sahihi inayokufaa.

Sababu 10 zinazokufanya upate tatizo la miguu kuwaka moto

1.Miguu kuwaka moto kwasababu ya kisukari-Diabetic Neuropathy

Kisukari kinapokusumbua kwa mda mrefu kinapelekea mishipa midogo ya fahamu kuathirika. Mishipa inapoathirika inakwamisha pia usafirishaji wa taarifa ndani ya mwili.

Taarifa zisiposafirishwa vyema inapelekea changamoto kwenye kuhisi matukio ya ndani na nje ya mwili. Pia kisukari kinaharibu mishipa ya damu ambayo inabeba hewa safi ya oksijeni ndani ya mwili.

Mishipa ya fahamu inaweza kuathiriwa maeneo mbalimbali ya mwili. Na athari hii inaongeza endapo una

  • uzito mkubwa na kitambi
  • presha ya kupanda imeongezeka
  • unavuta sigara
  • kunywa pombe

Aina za ganzi ya kisukari

Athari za mishipa ya fahamu kitaalamu tunaita neuropathy, lakini kuna aina za neuropathy. Aina kubwa ambayo inawatokea zaidi wagonjwa kisukari ni peripherial neuropathy.

Peripherial maana yake ni maeneo ya pembezoni, hivo ni athari ya mishipa ya fahamu iliyo kwenye viungo vya pembezoni mwa mwili. kama vidole vya miguuni na mikononi.

Dalili zingine za hii peripherial neuropathy ni pamoja na

  • kuhisi mguu na mikono kufa gani
  • kuhisi kama umevaa kitu cha kubana mfano wa sox
  • maumivu makali ya haraka na kupotea
  • kutokwa jasho jingi kupita kiasi na
  • miguu na mikono kukosa nguvu

Ni muhimu sana kumwona daktari endapo umegundua una dalili za ganzi ya kisukari. Kwenye kutibu tatizo lako utatakiwa kurekebisha kwanza kisukari ili mishipa isiendelee kuathirika zaidi.

2.Matumizi ya pombe

Watu wanaokunywa sana pombe wapo kwenye hatari ya kuathirika mishipa ya fahamu, na hii kitaalamu inaitwa alcoholic neuropathy. Aina hii ya ganzi inaweza kusababisha maumivu kwenye unyayo na miguu kukosa nguvu.

Tiba kwa ganzi ya aina hii kuacha kwanza pombe na kubadili lishe yako kwa kula mlo kamili. Endapo utaacha pombe itapunguza athari zaidi na pia kuondoa zile dalili mbaya.

3.Upungufu wa lishe.

Upungufu wa Vitamin B kwenye lishe yako kunaweza kupelekea upate tatizo la miguu kuwaka moto.
Kupungukiwa damu pia inatokana na upungufu wa vitamin B.

Dalili zingine za kwamba una upungufu wa damu na kupelekea ganzi ni pamoja na kukosa nguvu, uchovu, kushindwa kupumua vizuri na kizunguzungu

4.tatizo kwenye tezi ya shingo-thyroid

Kuna changamoto mbili za tezi ya shingoni. Ni aidha tezi inafanya kazi chini ya kiwango- hypothyrpoidsm au inafanya kazi kupita kiasi-hypethyrodism. Tezi inapofanya kazi chini ya kiwango, yaweza kupelekea mishipa ya fahamu kuathirika na hivi kukufanya miguu yako iwake moto.

5.Magonjwa ya kuambukiza

Mishipa ya fahamu inaweza kuathiriwa kutokana na magonjwa mbalimbali ya kuambukiwa, na hivo kukufanya upate ganzi kwenye miguu. Magonjwa haya ni pampja na

Kama unahisi una magonjwa haya ya kuambukiza, ongea na daktari ili aweze kukupima.

6.Fungus ya Miguu-athletes foot

Hii ni aina ya fungus ya miguu inayoambukizwa kwa kasi sana, na inaathiri unyayo, mikono na kucha pia. Ugonjwa huu pia huitwa tinea pedis.

Dalili kubwa ya fungus kwenye miguu mi kuwasha kwenye unyayo na dali zingine ni pamoja na

  • malengelenge kwenye unyayo
  • ngozi kunyonyoka katikati ya vidole na kwenye unyayo
  • ngozi kuwa kavu pembeni ya mguu na kwenye unyayo
  • kucha kugeuka rangi kuwa yeusi na nene sana kuliko mwanzo

7.Magonjwa ya figo

Kazi ya figo ni kuchuja mkojo na kutoa taka kupitia njia ya mkjo na jasho. Kama figo hazifanyi kazi vizuri, inapelekea sumu kujikusanya kwenye mfumo wako. Sumu zinapojikusanya zaweza kupelekea ganzi kwenye na miguu kuwaka moto.

Karibu asilimia kumi ya watu wenye magonjwa ya figo wanapata hili tatizo la kuvimba miguu kunakoambatana na kuwaka moto.

Wagonjwa wa figo waliopo kwenye huduma ya kusafisha damu yani dialysis, wanapta hii changamoto ya miguu kuwaka moto. Hii ni kwasababu wanakuwa na upungufu mkubwa wa virutubishi mwilini. Tiba ya kusafisha damu-dialysis inaondoa vitami B1 kwenye damu.

Kufeli kwa figo oia kunasababisha dalili hizi

  • kuvimba miguu
  • muwasho
  • kichwa kuuma
  • maumivu
  • joint kuwa ngumu na kujaa maji
  • kuhisi ganzi na viungo kukosa nguvu

8.Peripherial artery disease

Artery ni mishipa inayosafirisha damu yenye hewa safi ya oksijeni mwilini. Kwahivo kama damu isipofika eneo fulani la mwili, inapelekea ganzi na hali ganzi na kuwaka moto maeneo ya miguu na vidole vya mikono.

9.Matibabu ya Chemotherapy

Tiba hii inahusisha matumizi ya dawa zenye nguvu sana ili kuharbu seli za saratani. Chemotherapy ina madhara kiasi kwenye mwili, ikiwamo kuleta matokeo mabaya kama

10.Kukaa kwenye mazingira yenye sumu

Unapofanya kazi maeneo yenye kemikali nyingi, mfano viwandani au kwenye mionzi yaweza kukupelekea uathirike mishipa ya faham na hivo kupelekea miguu kuwaka moto. Pia dawa baadhi mfano za ukimwi na kifafa zaweza kupelekea athari kwenye mishipaya fahamu.

Tiba ya nyumbani itakayokupa nafuu kwa miguu kuwaka moto

  1. Chovya miguu yako kwenye maji baridi au kwenye barafu kwa dakika chache kisha utoe
  2. Chovya miguu yako kwenye maji yenye chunvi au apple cider vinegar. Kama una kisukari muulize kwanza daktari wako kama njia hii ni sahihi
  3. Tumia chai ya manjano. Manjano ya kiambata cha curcumin ambacho kinapunguza maumivu kwenye neva
  4. Fanya masaji kwenye mguu ili kurahishisha usafirishaji wa damu.
Categories
Afya ya Meno na Kinywa

Ulimi Kuchubuka

ulimi kuchubuka
ulimi

Ulimi wako ni umetengenezwa kwa msuli wa tofauti sana na kipeke sana na umejishika kwenye mfupa eneo moja tu la mwishoni. Ngozi yake imejaa testa za ladha.Mwisho wa makala hii utakuwa umejua chanzo cha ulimi kuchubuka na hatua 7 za kutibu tatizo.

Kazi kubwa za ulimi ukiwa ni

  • kusaidia utafunaji wa chakula na kukizungusha chakula kwenye mdomo
  • kuonja chunvu, tamu na kitu kichungu
  • kutamka maneno vizuri na sauti

Ulimi kuchubuka yaweza kusababishwa na vitu vifuatavyo

1.Majeraha kwenye ulimi

Endapo ngozi ya ulimi ilipata majeraha, kinga ya mwili inaanza kupambana ili kutoa zile seli ziliokufa. Kitendo hichi kinaweza kupelekea ulimi wao kuchubuka.

Kuna njia nyingi zaweza kupelekea ukapata mejeraha kwenye ulimi wako, njia hizi ni pamoja na

  • kunywa kitu cha moto sana mfano chai
  • kunywa au kula kitu chenye tundikali kwa wingi mfano vinegar, malimau nk
  • kula au kunywa vyakula vichachu mfano pilipili
  • kujin’gata ulimi nyakati za kuongea au kula, ama umepata ajali ya kujigongesha

2.Fungus ya ulimi-oral thrush

Fungus ya ulimi inasababishwa na vimelea wa candida. Dalili kubwa ya ulimi wako kuwa na fungus ni utando mweupe na pia kuchubuka ngozi

3.Vidonda vya mdomo-canker sores

Vidonda vya mdomo vinaleta maumvu sana kwenye ulimi. Na vidonda hivi tunaweza kuvigawanya katika makundi matatu

Minor. Hivi ni vidonda vidongo vya ukubwa wa ml 2 mpaka 8, na huwa vinapona vyenyewe.

Major: hivi ni vikubwa na vinafikia cm 1, vikipona vinaacha alama

Herpetiform: hivi bi vidonda vingi vinajikusanya pamoja na kufanya kidonda kikubwa.

4.Mabaka kwenye ulimi -geographic tongue

Mabaka haya yanaweza kuwa na rangi tofauti na ngozi ya kawaida ya ulimi. Mabaka haya mengi hayaumi na ni ya kawaida hata siyo saratani. Yanaweza kubabuka na kuisha yenyewe.

Lini unatakiwa kumwona Daktari

Unatakiwa kumwona daktari endapo unapata dalili mbaya zaidi, na vidonda vinazidi kukua kila siku bila kuonesha nafuu. Pia watakiwa kwenda hospitali haraka endapo unapata

  • homa kali
  • unashindwa kunywa maji vizuri au kula
  • ulimi unapata vidonda mara kwa mara
  • maumivu ya ulimi yasiyoisha hata kwa dawa za kununua dukani
  • unanuka mdomo kupita kiasi
  • ulimi unavimba na unashindwa kupumua vizuri

Huduma ya kwanza kwa tatizo la ulimi kuchubuka

  1. Usitumie vyakula na vinywaj vya moto sana
  2. Uache kunywa pombe na kuvuta sigara
  3. Safisha meno yako mara kwa mara na hakikisha kinywa chako ni kisafi
  4. Epuka kula vyakula vilivyokaangwa kwenye mafuta, vichachu na vyenye tindikali kwa wingi
  5. Nunua supliment ya vitamin C na B-complex pharmacy utumie
  6. Weka maji ya vuguvugu na chunvi kiasi, kisha yazungushe mdomoni na uteme
  7. Weka kipande cha barafu kwenye kwenye kidonda kupunguza maumivu.

Bofya kusoma kuhusu: Fungus mdomoni

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Kubeba Mimba Katika Umri Mkubwa

mimba katika umri mkubwa
mimba uzeeni

Ni umri gani tunasema umeshika mimba uzeeni?

Kuanzia miaka 35 tunasema ni umri mkubwa zaidi wa kushika mimba (advanced martenal age)

Kutokana na sababu mbalimbali, wanawake wanaweza kuamua kuchelewa sana kutafuta mtoto. Hii imekuwa tabia maarufu sana katika miaka ya hivi karibuni. Mabadiliko ya teknologia yamechangia sana. Mfano mtu anaweza kuamua kutunza mayai na mbegu kisha zikatumika hata baada ya miaka mi5 kushika mimba.

Pamoja na teknologia kukua, bado hatari ya kubeba mimba katika umri mkubwa ipo. Changamoto kama mimba kuharibika, kifafa cha mimba, kujifungua kwa upasuaji nk

Kwanini ni hatari kubeba mimba katika umri mkubwa?

Kadiri umri unavosogea, uwezekano wa kuugua magonjwa sugu unaongezeka. Magonjwa kama kisukari, presha ya kupanda na magonjwa ya tezi ya shingo. Hata kama afya yako iko njema kabla ya mimba, unapopata mimba italeta mabadliko ya kukuweka kwenye changamoto.

Wanawake wanaobeba mimba katika umri zaidi ya 35 wapo kwenye hatari ya

  • mimba kutunga nje ya kizazi
  • mimba kutoka mapema
  • kuchelewa kujifungua
  • matatizo ya kondo la nyuma
  • kisukari cha mimba
  • presha ya kupanda
  • kifafa cha mimba
  • kujifungua mapema kabla ya wakati
  • kupungukiwa damu
  • magonjwa ya moyo
  • kuziba mishipa ya damu
  • kuvuja damu nyingi baada ya kuzaa

Changamoto kwa mtoto

Kuna ongezekeno la hatari ya mamatizo ya hitilafu za vinasaba, pale mayai yanapozeeka. Mwanaume yeye anazalisha mbegu mpya kila siku, ila kwa mwanamke ni tofauti.

Mwanamke anazaliwa na mayai yote, hakuna mayai mapya yanayozalishwa tena, ila tu yanapevuka kila mwezi. Mayai haya yanavokaa miaka mingi yanazeeka na kuwa na hitilafu za kivinasaba.

Kwa mtu mzima, mzunguko wa damu kwenye via vya uzazi na kuelekea kwenye kondo la nyuma unapungua, na hivo kupelekea ukuaji hafifu wa mtoto tumboni.

Pia hatari ya kuumwa kwa mjamzito katika umri mkubwa inaongeeka, na kuathiri ukuaji wa mtoto, kupungua majimaji ya mtoto, na kujifungua njiti.

Maandalizi ya kubeba mimba katika umri mkubwa

Wataalamu wa uzazi wanashauri kuweka sawa uzito wako, kufanya mazoezi, kula vizuri na kupunguza stress ni muhimu pale unapotaka kubeba mimba katika miaka 35+

Muone daktari akufanyie vipimo hasa kwa magonjwa ya kisukari, tezi ya shingoni, na presha ya kupanda. Ni muhimu sana kupima magonjwa haya kabla hujashika mimba kwasababu yanaweza kuwepo bila dalili yoyote. Hakikisha unamweleza daktari anayekupima kwamba unajaribu kubeba mimba.

Je mama mtu mzima atapata changamoto gani kwenye kujifungua?

Mjamzito anapokaribia kujifungua, kondo la nyuma huanza kulegea. Hii inamaanisha mishipa ya damu inaanza kuzeeka, na usafirishaji wa chakula na hewa kuelekea kwenye mtoto unapungua. Lengo ni kumuandaa mtoto kuanza kujitegemea kula akitoka nje ya tumbo.

Kitendo hichi kinatokea mapema sana kwa wajawazito wa umri mkubwa. Yaani usafirishaji unapungua mapema kabla ya muda muafaka wa kujifungua. Ndiomaana katika umri huu, mimba ikifika tu wiki 39 na hujapata uchungu, unazalishwa kwa lazima ili kumuokoa mtoto.

Watu wazima wako kwenye uwezekano mkubwa wa kujifungua kwa upasuaji kwasababu wanakosa nguvu ya kusukuma mtoto. Na watoto wanaozaliwa na wazazi wazee, wanaweza kuwa mapigo ya moyo ya tofauti na hivo kujifungua kwa njia ya uke ikawa hatari kwao.

Bofya kusoma kuhusu: Kujifungua kwa upasuaji, ushauri na hatua za kuzingatia

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Hedhi salama

Hedhi Mara Mbili Katika Mwezi

hedhi mara mbili katika mwezi
kalenda ya hedhi

Mzunguko wa hedhi

Hedhi ya kawaida inachukua mzunguko wa siku siku 21 maka 35. Nikisema mzunguko namaanisha jumla ya siku kuanzia ulipopata hedhi mwezi mmoja, mpaka utakapopata hedhi tena katika mwezi unaofata. Makala hii itaongelea tatizo la kupata hedhi mara mbili katika mwezi na nini cha kufanya.

Japo siyo kawaida kupata mizunguko tofauti kila mwezi. Baadhi ya mizunguko yaweza kuwa mifupi au mirefu kuliko mingine, na hivo kupelekea upate hedhi mara mbili katika mwezi.

Tazama na dalili zingine

Katika nyakati nyingi kupata hedhi mara mbili ndani ya mwezi mmoja yaweza isiwe tatizo. Lakini kama inatokea kwa kujirudia ni muhimu kutazama na dalili zingine zinazoambatana. Endelea kusoma zaidi ili kujifunza kuhusu changamoto ya hedhi mara mbili katika mwezi

Hedhi mara mbili katika mwezi kwa mara ya kwanza

Watu wenye mzunguko mfupi mara nyingi sana wanapata hedhi mwanzoni na mwishoni mwa mwezi. Kwa mtu mwenye mzunguko wa kawaida wa siku 28 au zaidi, akipata hedhi mara mbili lazima ashituke.

Kumbuka hedhi isipotoka kwa wakati inaashiria changamoto ya kiafya. Ni ni rahisi sana kuchanganya hedhi na bleed ingine. Waweza kudhani ni hedhi kumbe unatokwa na damu tu kutokana na changamoto fulani.

Changamoto zinazoweza kupelekea bleed isiyo ya hedhi ni pamoja na

Mimba- mimba inapojishikiza kwenye ukuta wa kizazi yaweza kupelekea bleed. Ugonjwa wa zinaa: Magonjwa ya ngono yanaweza kupelekea upate bleed kidogo na kutokwa na uchafu usio wa kawaida ukeni.

Mimba kuharibika-Mimba inapoharbika inaambatana na maumivu makali na kutokwa na mabonge ya damu. Ni muhimu kwenda hospitali mapema ikiwa una mimba na umeanza kuona damu.

Mabadiliko ya uzito– Mazoezi kupita kiasi na mabadiliko makubwa ya uzito wa mwili yanaweza kupelekea hedhi mara mbili.

Uzazi wa mpango wa kisasa-Hedhi kuvurugika na kutoka mara mbili inatokea sana kwa wanaotumia njia za kisasa kuzuia mimba , mfano sindano, njiti na vidonge

Vimbe kwenye mlango wa kizazi na ukuta wa kizazi: Hizi ni vimbe ambazo siyo saratani kwenye kuta za mlango wa kizazi na kwenye ukuta wa kizazi, ambazo zaweza kupelekea upate hedhi zaidi ya mara moja.

Saratani ya mlango wa kizazi: kutokwa damu yaweza kuashiria uwepo wa saratani

Tofauti kati ya damu ya hedhi na bleed ya tatizo la via vya uzazi

Hizi dondoo zitakusaidia kujua kama damu unayopata ni hedhi ama siyo hedhi

Kama ni hedhi ya kawaida itakulazimu kubadili pedi au tampon kila baada ya masaa kadhaa. Na damu kawaida inakuwa nyekundu nzito au ya kungaa, brown au pink

Kama ni matone ya damu ambayo siyo hedhi, haitahitaji kubadili pedi au tamponi mara kwa mara, unaweza kutumia pedi moja tu kwa siku. Damu yake yaweza kuwa ya pick, brown na inakata mapema ndani ya siku moja au mbili

Chanzo kikubwa cha mzunguko mfupi na hedhi mara mbili katika mwezi

Nini kinapelekea hedhi mara mbili katika mwezi? inaweza kutokana na mzunguko mfupi ama changamoto ya kiafya inayopelekea bleed ukeni.

Baadhi ya mambo yanayopelekea hedhi mara mbili ni pamoja na

1.Kukaribia kukoma hedhi-Perimenopause

Perimenopause ni kipindi ambacho mwanamke anakarbia kukoma hedhi yake, wakati ambapo kunatokea mabadiliko makubwa ya homoni. Kipindi hichi waweza kupata hedhi mara mbili ndani ya mwezi mmoja. Perimenopasue inatofautiana kwa kila mwanamke.

Kuna wengine inachukua hata miaka 10 ndipo hedhi inakoma. Wakati wa kipindi hiki kuelekea kukoma, waweza kupata hedhi nzito sana, kuvusha miezi kadhaa bila hedhi, mzunguko kuwa mrefu , hedhi nyepesi sana. Menopause ndio kukoma hedhi kwenyewe. Mwanamke anakoma hedhi endapo atakosa hedhi kwa miezi 12 mfululizo.

2.Fibroids

Hizi ni vimbe zinazotokea kwenye kizazi. Ni vimbe zisizo saratani, na zaweza kuleta hedhi nzito, au ukavusha kabisa hedhi. Dalili zingine za fibroids ni pamoja na

  • kupata mkojo mara kwa mara
  • kuhisi uzito eneo la nyonga
  • maumivu chini ya mgongo
  • maumivu wakati wa tendo

Daktari atagundua kama una fibroids kwa kukufanyia kipimo cha utrasound.

3.Magonjwa ya tezi ya shingoni

Tezi huu huitwa thyroid, inakaa shingoni na ina umbo kama la kipepeo. Kazi ya tezi hii ni kuzalisha homoni ambazo zinaratibu mpangilio wa hedhi yako. Dalili za kwamba kuna tatizo kwenye tezi ya shingo ni pamoja na

  • kuhisi baridi mda wote
  • kuongezeka uzito
  • tumbo kujaa
  • kupungua mapigo ya moyo
  • kutoka na damu nyingi ya hedhi

Kwa upande mwingine ikiwa tezi yako inafanya kazi kupita kiasi utaanza kupata dalili hizi

  • kuhisi joto mda wote
  • macho kuvimba
  • moyo kwenda mbio sana
  • kukosa usingizi
  • kuharisha na
  • macho kuvimba

Hakikisha unaenda hospital, endapo utaanza kupata dalili hizi za tezi ya shingo.

Madhara zaidi ya kupata hedhi mara mbili

Watu wanaotoka kwenye familia zenye historia ya kuugua vimbe kwenye kizazi na kukoma hedhi mapema , wapo kwenye hatari zaidi ya kupata hili tatizo la hedhi mara mbili katika mwezi. Moja ya changamoto utakayopata kutokana na kupata hedhi mara mbili ni kupungukiwa damu. Dalili hizi zinaonesha kwamba umepungukiwa na damu.

  • mwili kuchoka sana
  • kizunguzungu
  • mapigo ya moyo kubadilika
  • kukosa pumzi
  • kuumwa sana kichwa

Je kuna umuhimu wa dawa kutibu hedhi mara mbili?

Hedhi mara mbili siyo tatizo ikiwa mzunguko wako ni mfupi. Japo ni muhimu sana kumuona daktari endapo kama utapata dalili hizi hapa chini

  • hedhi mara mbili kwa miezi mi2 au mi3 mfululizo
  • maumivu wakati wa tendo
  • hedhi nzito ya mabonge
  • damu ya kuganda
  • maumivu chini ya kitovu hasa kama maumivu hayaishi
  • maumivu makali kwenye hedhi
  • kupata matone ya damu katikati ya mzunguko ambayo yanajirudia mwezi unaofata

Kwa binti mdogo hakuna tatizo

Matibabu ya tatizo hili ya kupata hedhi mara mbili katika mwezi mmoja, yanategemea na chanzo cha tatizo. Watu wenye mzunguko mfupi au wanaopata hili tatizo kwenye miaka ya mwanzo ya kubalehe, hawahitaji tiba tatizo laweza kuisha lenyewe.

Tiba inalenga Chanzo cha Tatizo

Daktari anaweza kupendekeza akupe dawa za kurekebisha homoni zile za kupanga uzazi. Kama tayari unatumia dawa za kisasa za uzazi wa mpango, na unahisi ndio chanzo cha tatizo, mjulishe daktari ili akubadilishie njia ingine.

Kwa tatizo la tezi ya shingo: daktari anaweza kupendekeza vipimo zaidi na kukupa dawa kwa tatizo hili

Kama unakarbia kukoma hedhi: kuna dawa za hormone utapewa kupunguza ukali wa tatizo

Kwa vimbe yani fibroids: daktari anaweza kukupa dawa, ama akapendekeza upasuaji, kulingana na ukubwa wa tatizo.

Kubadili mtindo wako wa maisha pia utasaidia kurekebisha homoni zako, mfano kama una uzito mkubwa na kitambi, anza kufanya mazoezi na kupunguza vyakula vya sukari.

Tumia Evecare Kurekebisha hedhi yako ndani ya mwezi mmoja

evecare

Evecare ni dawa asili na imetengenezwa nchini India kupitia mimea ua Ashoka, Asaparagus na lodh tree. Kwa miaka zaidi ya mitano ambayo tumekuwa tukihudumia wagonjwa wetu wa matatizo ya hedhi na homoni, tumepokea shuhuda lukuki.

Dawa itakusaidia kurekebisha homoni na mzunguko wa hedhi ili uanze kupata hedhi vizuri. Evecare inakuwa na vidonge 30, unameza vidonge viwili kila siku kwa muda wa wiki mbili.

Gharama ni Tsh 75,0000/=. Kabla ya kukupa dawa, daktari atakusikiliza kwanza na kujua chanzo cha tatizo lako.

angalizo

Kuna wimbi kubwa la wajasiliamali mitandaoni wanauza vidonge fake vya evecare, tena wanauza kwa bei rahisi sana. Watu hao siyo madaktari wala siyo wataalamu wa afya na wanauza bidhaa feki ambazo ni hatari wa afya yako. Wengi wao hawana hata ofisi, ukipata madhara unakosa pa kuuliza. Kuwa makini na watu hao, wamejaa sana insta na fb

Ukiwa na maswali na uhitaji wa tiba Tuandikie whatsapp kwa namba 0678626254. Tupo Dar- Mwembechai

Bofya kusoma: Njia salama za kupunguza maumivu kipindi cha hedhi