Categories
Hedhi salama Menopause

Kukoma hedhi mapema

kukoma hedhi

Kukoma hedhi kitaalamu menopause ni kipindi katika ukuaji wa mawanamke ambapo damu ya kila mwezi inakata kutoka. Jambo hili hutokea hasa miaka ya 40 au wengine mpaka 50. Ni kipindi ambacho kinaambatana na mabadiliko mengine makubwa ya mwili ikiwemo kupungua hamu ya tendo, mashavu ya uke kusinyaa na mifupa kuwa dhaifu.

Kukoma hedhi mapema zaidi

Kwa wanawake wengi kukoma hedhi hata siyo jambo la kuliwazia mpaka pale utakapofikia miaka 40s au 50s. Japo mmoja kati ya wanawake 100 anaweza kukoma hedhi mapema zaidi akiwa na miaka 20s au 30s, kuliko ilivozoeleka.

Menopause inapoanza mapema zaidi kabla hujafikisha miaka 40, tunaita primary ovarian insufficiency au primary ovarian failure.

Kundi gani la wanawake wanaweza kukoma hedhi mapema zaidi?

Wakati unaanza kukoma hedhi, mifuko ya mayai yani ovary zinapunguza uzalishaji wa homoni za estrogen. Kukoma hedhi siyo kipindi kifupi, ni mlolongo wa miaka inaweza kuchukua hata miaka 5 au 10 kukoma kabisa hedhi. Utaanza kwa kukosa hedhi miezi mi3 mpaka 6 kisha baadae unakoma mwaka mzima.

Hichi kipindi cha kukosa hedhi ndicho chaweza kudumu mpaka miak 5 au 10 kabla hujakoma moja kwa moja.

Sababu nyingi zinaweza kupelekea mwanamke akome hedhi mapema kabla ya mda wake. Sababu hizi ni pamoja na

Dalili za kukoma hedhi mapema

Wanawake waliokoma hedhi mapema wanapata dalili za

Kumbuka siyo kawaida kwa mwanamke aliye kwenye umri wa kuzaa kupata dalili hizi, hivo hakikisha unamwona daktari mapema apate kupima homoni zako”

Daktari atahitaji kupima kiwango cha homoni ya estrogen na FSH kujiridhisha kama kweli umekoma hedhi.

Ushauri gani wa kuzingatia na Lishe ukiwa kwenye menopause?

Vyakula vya kutumia mara kwa mara ukishakoma hedhi

Unapojaribu kuekebiusha homoni zako zilizovurugika na kupunguza madhara ya menopause, lishe yako inatakiwa kujumuisha madini ya kutosha na mafuta mazuri. Unapokula lishe hii kwa wingi itakusaidia kuweka sawa homoni na pia kukupunguzia mafuta mabaya mwilini.

Weka akili kwamba kadri unavozeeka utahitaji kupunguza kiwango cha mlo wako kwasababu kasi ya shuguli za mwili inapungua na umri. Ni muhimu sana kujizuia vyakula vilivyosindikwa na kupendelea kula chakula safi. Vyakula vitakavyokusaidia ni pamoja na

1.Vyakula vyenye madini ya calcium kwa wingi

Mifupa kudhoofika ni moja na changamoto inayotokea baada ya kukoma hedhi. Japo mwanzoni huwezi kuona lakini madhara yake yanaweza kuonekana miaka ya baadae.

Mwili wako unajenga mifupa kuanzia ukiwa mdogo mpaka kufikia miaka 30. Baada ya hapo unaanza kupoteza mifupa. Kwa mwanamke kutokana na kupungua kwa homoni ya estrogen, kasi ya kumomonyoka mifupa inakuwa kubwa zaidi baada ya kukoma hedhi.

Ndiomaana tunashauri upendelee kula kwa wingi vyakula vyenye madini ya Calcium kama

  • maziwa
  • yogurt
  • mboga za majani za kijani kilichokolea na
  • dagaa
  • mboga zingine jamii ya kabeji kama broccoli, cauliflower na asparagus

2.Vyakula vyenye fiber/kambakamba kwa wingi

Vyakula vyenye kambakamba ni muhimu sana kwa afya ya moyo na mfumo wa chakula, pamoja na kuweka sawa uzito wako. Baadhi ya tafiti zinasema ulaji wa vyakula vya kamba kwa wingi unasaidia pia uzalishaji wa homoni ya estrogen. Homoni ambayo inapungua sana kwa walikoma hedhi.

Vyanzo vizuri vya kambakamba ni pamoja na karanga, parachichi, mbegu, maharage, nafaka, mbogamboga na matunda.

3.Mafuta yenye omega 3

Omega 3 ni kiambata kinachopatikana kwenye samaki na mbegu za maboga. Kiambata hiki kinasaidia kuimarisha moyo , kumarisha ngozi na kuzuia mwili kututumka . Mafuta haya yanapatikana zaidi kwenye samaki aina ya saladini na salmon. Tafiti zinasema kwamba kutumia omega 3 mara kwa mara kunasaidia uzalishaji wa homoni na kuzuia makali ya menopause.

4.Vyakula vya mafuta mazuri

Ni kweli kwamba vyakula vya mafuta havipandishi sukari kwenye damu ukilinganisha na vyakula vya sukari na wanga. Ndiomaana hata wenye uzito mkubwa na kitambi na wenye kisukari tunawashauri wale zaidi vyakula vya mafuta.

Pia vyakula hivi vinapunguza mpambano ndani ya mwili. Mafuta ndio yanayounda homoni zako mwilini. Hakikisha unapata mafuta mwali ambayo hayajachakachuliwa wala kuongezwa kemikali mbaya. Mafuta haya ni yale ya nazi, olive, vyakula kama nazi, parachichi, karanga ,ufuta na mbegu za maboga.

Categories
Afya ya uke Aina za Uchafu Ukeni

Uchafu wa njano ukeni maswali na majibu

uchafu wa njano ukeni
uchafu wa njano

Kutokana na sababu kadhaa, kutokwa na uchafu wa njano ukeni yaweza kuwa salama au hatarishi. Zifuatazo ni njia za kutambua kama uchafu wako ni salama ama ni kiashiria cha ugonjwa.

Aina za uchafu wa njano ukeni

Kutambua kama uchafu wako ni salama au hatari, unatakiwa kufatilia na kuzingatia baadhi ya mambo. Kuna aina nyingi sana za uchafu wa ukeni, hivo unahitajo kufatilia rangi, mwonekano, uzito na wepesi na harufu ya uchafu ili kujua kama watakiwa umwone daktari.

Kama uchafu wako wa njano hauna harufu kwa kiasi kikubwa huhitaji kumwona daktari. Uchafu wenye harufu unaweza kuashiria mamabukizi flani. Na kama uchafu wako unanuka, tambua kwamba ile rangi ya njano ni kiashiria cha aina ya maambukizi husika.

Uchafu mwepesi wa njano usiokolea na ambao hauna harufu wala dalili zozote mbaya kama maumivu ya tumbo, maumivu kwenye uke au muwasho, hapo hakuna tatizo ni uchafu wa kawaida.

Njano iliyokolea na uchafu mzito, ukiwa unaambatana na harufu mbaya, huu ni uchafu usio kawaida na unaashiria maambukizi.

Je ni kawaida mwanamke kupata uchafu wa njano ukeni?

Katika baadhi ya mazingira ni kawaida kupata uchafu wa njano. Siku chache baada ya hedhi unaweza kuona ute wa njano kama cream au unaonata.

Utakapokarbia hedhi, uchafu waweza kuwa mweusi kutokana na vipande vya damu kujichanganya na uchafu wa ukeni.

Kadiri hedhi inavokaribia kuisha rangi ya damu inabadilika kutoka kuwa nyekundu na kuwa brown na baadae kuwa na unjano. Huu uchafu wa njano ni masalia ya hedhi ya mwisho iliyobaki kwenye kizazi.

Uchafu wa njano ukeni ni wa kawaida endapo haujaambatana na harufu mbaya, muwasho, maumivu chini ya kitovu, maumivu kwenye tendo na maumivu wakati wa kukojoa.

Kama uchafu wa njano unanuka na kuna muwasho nini chanzo??

1.Maambukizi ya fungus -yeast infection

Uke wako unatakiwa kuwa na uwiano sawa wa vimelea na utindikali pia. Pale inapotokea mazingira yakavurugika, bakteria na fungus huanza kukua kupita kiasi na kukufanya uumwe. Kufanya tendo la ndoa na watu wengi, kutumia antibiotic mara kwa mara, kuosha uke mpaka ndani na kuvurugika kwa homoni inaweza kuvuruga mazingira ya uke.

Fungus ukeni, ni ugonjwa unatokea sana kwa wanawake wengi. Ugonjwa unatokea pale vimelea wa fungus wanapokua kupita kiasi.

Dalili kubwa za fangas ukeni ni pamoja na

  • muwasho kwenye mashavu ya uke
  • kuvimba kwa mashavu ya uke
  • maumivu wakati wa tendo
  • maumivu na hali ya kuungua wakati wa kukojoa
  • uke kuuma na kuvimba
  • uchafu mweupe wa kuganda kama mtindi

2.Ugonjwa wa Trichomoniasis

Ni ugonjwa unaotibika na unaambukiwa kupitia zinaa. Watu wengi waliathiriwa na ugonjwa huu hawakujua kama wameshaambukiwa sababu dalili huwa zinachelewa kujionesha.

dalili za trichomoniasis ni pamoja na

uchafu wa njano au kijani wenye harufu mbaya
kuvimba kwa mashavu ya uke na uke wote
kuhisi haja ndogo mara kwa mara
maumivu wakati wa tendo la ndoa na
maumivu wakati wa kukojoa

Ugonjwa unatibika kupitia antibiotics, endapo utapimwa na kugundilika na ugonjwa hakikisha unampeleka na mpenzi wako kupimwa.

3.Kisonono na Chlamydia

Magonjwa haya yote yanaabukizwa kwa zinaa. Magonjwa haya yanatibika kupitia antibiotics endapo utaanza tiba mapema. Kama hautapata tiba mapema, yaweza kupelekea upate PID, mirija kuziba na maumivu makali ya nyonga kutokana na makovu kwenye kizazi.

Ndiomaana ni muhimu sana kupima magonjwa ya zinaa mara kwa mara, hasa kama una wapenzi wengi au kama umekutana bila kinga na mpenzi mpya.

Dalili kubwa za chlamydia na kisonono ni pamoja na

  • kuongezeka kwa kiwango cha uchafu ukeni
  • maumivu wakati wa kukojoa na kwenye tendo
  • kutokwa na bleed katikati ya mzunguko
  • maumivu makali ya nyonga

4.PID

Pid ni kifupi cha pelvic inlafammatory disease. Ni athari kwenye via vya uzazi kwa mwanamke, na inatokea pale magonjwa kama chlamydia na kisonono yasipotibiwa vizuri na kuisha mpaka kusambaa kwenye mirija, na mayai. Aina nyingi za maambukizi ya bakteria zaweza kupelekea uugue PID.

Endapo PID haitatibiwa vizuri yaweza kupelekea changamoto kama mimba kutunga nje ya kizazi, mimba kuharibika na maumivu makali ya nyonga.

Dalili za PID ni pamoja na

  • uchafu wa njano au kijani ukeni wenye harufu mbaya
  • hedhi kuvurugika
  • maumivu wakati wa tendo
  • maumivu wakati wa kukojoa
  • kutokwa damu wakati na baada ya tendo
  • kuhisi homa na kichefuchefu

Uchafu wa njano wakati wa ujauzito

Mimba inakuja na mabadiliko mengi sana kutokana na kuongezeka kwa baadhi ya homoni. Wajawazito wengi wanashuhudia ongezeko la uchafu unaotoka ukeni kutokana na kuongezeka kwa homoni za estrogen na progesterone.

Kama unapata uchafu mweupe , mwembamba usio na harufu mbaya hiyo ni kawaida. Kitaalamu uchafu unaitwa leukorrhea.

Kama utaona uchafu wa kijani au njano wenye harufu mbaya, hiyo yaweza kuashiria maambukizi. Wajawazito wanaugua sana fungus ukeni. Unatakiwa kwenda hospital mapema upate vipimo na dawa.

Endapo hujatibiwa fungus au magonjwa ya zinaa, inaweza kuhatarisha afya ya mtoto wakati anazaliwa. Maana mtoto anaweza kupata maambukizi.

Mwisho kabisa

Kama wewe ni mwanamke, ujue kwamba lazima utakutana na changamoto nyingi kwenye uke wako hasa wala la uchafu ukeni. Ni muhimu sana kujielimisha na kujua uchafu upi ni hatari na upi ni salama ili umwone daktari mapema.

Kwa ushauri na tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Tendo la ndoa

Maumivu ukeni wakati wa tendo

maumivu ukeni wakati wa tendo

Tendo la ndoa ni moja na tukio tamu na la kufurahisha sana katika maisha ya mwandamu. Tendo linaimarisha ukaribu na upendo baina ya mke na mume. Pamoja na hayo ,watu wengi wanapata maumivu makali wakati wa tendo na hawafurahii kabisa. Kuna mambo mengi yanapelekea maumivu ukeni wakati wa tendo. Soma zaidi kujua nini cha kufanya kuondoa tatizo.

Maumivu kwenye tendo la ndoa ni kitu gani hasa?

Kitaalamu huitwa dyspareunia ni neno linalomaanisha maumivu ya via vya uzazi wakati wa tendo au baada ya tendo. Tatizo hili linawapata karibu asilimia 75 ya wanawake wote duniani.

Maumivu kwenye tendo yanaweza kuvuruga mahusiano, kukufanya ujihisi mpweke na huna thamani na kukosa kujiamini mbele ya mpenzi wako. Baadhi ya wanawake huamua kutojihusisha tena na tendo la ndoa baada ya kupata maumivu.

Pamoja na kwamba tatizo linatibika kwa kiasi kikubwa, watu wengi ni waoga sana kuelezea changamoto hii kwa kuogopa aibu ama kudharaulika.

Dalili za maumivu kwenye tendo

  • maumivu ya haraka
  • hali ya kuungua ukeni
  • kukosa hamu ya tendo
  • kushindwa kufika kileleni
  • maumivu ya tumbo

Je haya maumivu yanatokea ukeni tu?

Maumivu kwenye tendo yanatofautiana kwa kila mtu. Baadhi ya wanawake wanahisi maumivu wakati uume unaingia, na wengine wanapata maumivu wakiguswa tu kwenye via vya uzazi. Baadhi wanapata maumivu ya tendo baada ya kukoma hedhi.

Maumivu yanaweza kutokea

  • ndani ya ukeni
  • kwenye mashavu ya ukeni
  • chini ya mgongo
  • ndani ya kizazi
  • kwenye nyonga
  • tumboni chini ya kitovu na
  • kwenye ukuta unaotenganisha uke na mkundu

Baadhi ya wanawake wanapata maumivu baada tu ya kumaliza tendo, na wengine wakati wa kukojoa.

Nini kinapelekea maumivu kwenye tendo?

Baadhi ya sababu kubwa zinazopelekea mwanamke kupata maumivu ni pamoja na

1.Ukavu ukeni

Hii ni sababu kubwa zaidi ya maumivu kwenye tendo kutokana na kukosekana na ute ukeni na hivo msuguano kuwa mkubwa. Ukavu ukeni inatokea zaidi baada ya kukoma hedhi. Mabadiliko ya homoni yanapelekea kupungua kwa uzalishaji wa ute kwenye uke baada ya kukoma hedhi.

Sababu zingine zinazopelekea ukavu ukeni ni pamoja na kutumia njia za kisasa kupanga uzazi, kunyonyesha, stress na mwanamke kutoandaliwa vya kutosha.

2.Maambukizi

Maambukizi aina tofauti yanaweza kupelekea maumivu kwenye tendo. Maambukizi haya ni pamoja na

  • maambukizi ya bakteria ya ni bacterial vaginosis
  • fungus ukeni: dalili zake ikiwa ni pamoja na kutokwa uchafu unaoganda mzito, muwasho
  • kisonono
  • UTI kali
  • PID na
  • Chlaydia

Pia magonjwa mengine kwenye kizazi yanaweza kupelekea maumivu kwenye tendo. Magonjwa haya ni pamoja na

  • Endometriosis- yani ukuta wa ndani wa kizazi kuvimba
  • vaginismus: hii ni hali ya uke kugoma kuruhusu kitu chochote kuingia
  • Fibroids: Vimbe kwenye ukuta wa kizazi
  • Ovarian cyst: Vimbe kwenye mayai
  • Bartholin abscess: hizi ni vimbe kweye tezi za uke
  • Cervicitis: yani maambukizi kwenye mlango wa kizazi na kupelekea kuvimba kwake

Kumbuka magonjwa haya ni ngumu kwako kuyagundua ukiwa nyumbani. Ni mpaka kwenda hospitali, na kufanyiwa vipimo ndipo daktari atakwmabie endapo una uvimbe nk

Nini cha kufanya kuondoa maumivu?

Tiba ya tatizo inategemea na chanzo chake. Unapojiskia vibaya, hatua ya kwanza ni kwenda hospital na kuonana na daktari ili akusaidie kugundua chanzo cha tatizo.
Daktari atakuuliza baadhi ya maswali kujua historia ya tatizo, na aatapendekeza vipimo vya kufanyiwa.

Baada ya vipimo ndipo utapewa dawa sahihi ili uanze tena kufurahia tendo la ndoa.

Mawasiliano baina ya wapenzi

Mawasiliano ni nguzo muhimu sana kwenye mahusiano, itasaidia wapenzi kujuana kuhusu changamoto zao. Mpenzi wako ataweza kukuvumilia wakati unaendelea na tiba. Kumbuka kuendelea kufanya tendo wakati unapata maumivu ni mbaya, kwani itakuathiri kisaikolojia na kukfanya uchukue tendo la ndoa.

Kama chanzo cha tatizo ni ukavu ukeni, ni muhimu sana mtumie muda mwingi kwenye kuandaana.

Weka kwenye akili kwamba kutumia vilainishi vya kuganda kulainisha uke, yaweza kuleta madhara kwenye tishui laini za uke. Ni vizuri kutumia vilainishi vye maji maji pamoja na condom.

Kama maumivu unapata siku kadhaa tu, basi jaribu kubadili style ya kufanya mapenzi. Ongea na mwenzi wako akuingilie taratibu bila nguvu nyingi.

Lini unatakiwa kumwona daktari?

Muone daktari haraka endapo tatizo linajitokeza mara kwa mara, na maumivu yanazidi kila unapojaribu kufanya tendo. Pia kama unajihisi unaugua magonjwa kama fungus, unatokwa uchafu usio kawaida ana unapata maumivu ya tumbo muone daktari haraka.

Categories
Afya ya uke

Uchafu mweupe ukeni kama mtindi

uchafu mweupe ukeni kama mtindi

Uchafu mweupe ukeni unatokea sana kwenye mzunguko wa mwanamke na yaweza kuashiria yai kupevuka. Japo katika mazingira flani yaweza kuashiria ugonjwa ama changamoto flani ya kiafya kama fungus.

Kwanini unatokwa na uchafu ukeni?

Kama ambayo mti huangusha matawi, ni kawaida kwa uke wako kujisafisha na kutoa bakteria waliokufa nje ya mwili.

Aina ya uchafu unaoona unabadilika kila siku kwenye mzunguko wako wa hedhi, lakini kwa kiasi kikubwa huwa inaashiria kwamba mwili wako unafanya kazi vizuri sana.

Ute wa ukeni unasaidia kufanya uke wako kuvutia na kuwa mlaini. Utokaji wa ute ni matokeo ya tezi zilizopo ndani ya uke na homoni zako, ndiomaana ute huu unabadilika katika vipindi tofauti vya mzunguko na hata ukiwa mjamzito.

kutoka ute unaashiria mwili kujisafisha

Kutokwa na uchafu ukeni pia ni namna ya mwili wako kubalansi kiwango cha tindikali. Uteute unaleta utelezi kwa ajili ya uchafu, bakteria na vimelea wabaya kutolewa nje ya uke.

Japo siyo kila unapopata uchafu ni kiashiria cha usalama, kuna kipindi waweza kuwa na shida kubwa sana ya kiafya. Endelea kusoma upate mwongozo ili ujue ni wakati gani ukamwone daktari.

Kwanini unapata uchafu mweupe ukeni?

Uchafu mzito mweupe ni kawaida, na unatokea sana kwenye mzunguko wako. Kitaalamu uchafu huu huitwa leukorrhea na ni wa kawaida. Uchafu unaweza kwa kuwa mzito siku chache kabla ya siku za hatari na baadae utakuwa na ute mlaini wa kuvutika kama yai.

Hii ni kiashiria kwamba upo kwenye muda mzuri wa kubeba mimba, maana yai linatolewa. Kama ulikuwa unatafuta mimba huu ndio muda wa kukutana kimapenzi.

Endapo ute unaotoka hauna harufu mbaya na wala hakuna dalili zingine mbaya kama maumivu kwneye tendo na maumivu chini ya kitovu, basi ni kawaida.

Nini kinasababisha Uchafu mweupe kama maziwa ukeni?

Kwenye siku za kwanza za mzunguko unaweza uona ute mwepesi , kama maziwa. Uchafu huu mweupe kama maziwa yaweza kuwa kiashiria kwamba una mimba. Kwenye hatua za mwanzo za mimba , baadhi ya wanawake wanazalisha uchafu mwembemba mweupe kama maziwa. Uchafu huu ni kutokana na mabadiliko ya vichocheo ama homoni na ni kawaida.

Uchafu mweupe kwa mjamzito

Kwa mjamzito uchafu huu unasaidia kutoa vimelea wabaya, bakteria na uchafu ukeni. Pia unasaidia kuweka kifuniko cha ute mzito kwenye mlango wa kizazi. Ute ambao utazuia kitu chochote kuingia kwenye kizazi wakati una mimba.

Kama tu uchafu wako hauna harufu wana kuleta muwasho na hakuna maumivu ya tumbo, basi ujue ni uchafu wa kawaida na huhitaji kupata mawazo.

Lakini kama rangi itabadilika na ya kijani au brown au njano, na inaambatana na harufu mbaya ya shombo la samaki, hapo ujue kuna maambukizi hasa ya bakteria.

Nini kinapelekea uchafu mweupe ukeni wa kunata?

Ukiwa kwenye siku zingine safe yani siku ambazo siyo za hatari, mwili wako unazalisha ute mzito wa kunata. Ute huu ni kama kizuizi cha mbegu kuingia kwenye kizazi.

Pia kazi ya uchafu huu wa kunata ni kuzuia usipate mamabukizi baada ya hedhi, pale ambapo uke unazalisha ute kidogo sana.

Uchafu mweupe mzito ulioganda kama mtindi

Kama unapata uchafu mwupe umekatika kama maziwa mtindi na ni mzito na unapata muwasho, basi hapo ujue una fungus.

Uke wako huwa unafanya kazi kubwa sana ya kubalansi mazingira ua utindikali ili bakteria wazuri wawepo kupabambana na vimelea wabaya. Endapo mazingira yakivurugika hapo ndipo fangasi watakuwa kupita kiasi.

Vimelea wa Fungus aina ya candida wanaweza kukua kupita kiasi na kuleta madhara kwenye uke, na hivo kupelekea utokwe na uchafu mzito wa kuganda. Uchafu huu ni matokeo ya kinga yako kupambana na vimelea hawa.

Watu wenye fungus ukeni wanapata dalili zingine kama

  • muwasho kwenye mashavu ya uke
  • kuvimba kwa mashavu ya uke
  • maumivu wakati wa tendo
  • maumivu na hali ya kuungua wakati wa kukojoa
  • uke kuuma na kuvimba

Kama unaugua fungus ama umeanza kuona dalili, unaweza kwenda pharmacy ya karibu na kupata dawa.

Ni jambo zuri kusitisha kufanya tendo wakati unatibiwa maambukizi yako ya fungus. Mwanaume hana sababu ya kutibiwa kwasababu hawezi kuambukizwa kwa ngono.

Kama umeshaugua fungus zaidi ya mara 4 katika mwaka, ni vyema umuone daktari specialist wa wanawake. Unaweza kuwa na tatizo lililojificha ambalo linakufanya uugue fungus mara kwa mara.

Jinsi ya kuzuia uchafu mwingi ukeni

Kama unapata uchafu mwingi kupita kiasi na usio wa kawaida, unaweza kuwa na maambukizi, na unahitaji tiba kupona tatizo.

Uchafu mwingi kupita kiasi ni kiashiria cha

Lini yatakiwa kumwona daktari?

Ni muhimu kumwona daktari endapo uchafu unaotoka unanuka ama unaambatana na dalili hizi

Kumbuka kuepuka kuvuruga mazingira ya kwenye uke kama kutumia sabuni, marashi na kusafisha uke mpaka ndani. Tumia maji pekee kujisafisha na safisha eneo la mwanzo tu la uke. Uke umeumbwa kujisafisha wenyewe kila siku, hihitajio kutumia kemikali kujisafisha.

Kwa ushauri zaidi na tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Maumivu ya tumbo chini ya kitovu

maumivu ya tumbo chini ya kitovu

Maumivu ya tumbo yanaweza kusababishwa na vitu vingi sana na yanaweza kuhusisha zaidi ya kiungo kimoja cha mwili. Na maumivu ya tumbo chini ya kitovu yanahusisha viungo vyote vya uzazi, na viungo vingine kama figo na kibofu. Maumivu yanapoanza inaweza kuwa ngumu kujua chanzo cha tatizo ndiomaana ni muhimu kwenda hospital.

Nini kinapelekea maumivu ya Tumbo chini ya kitovu?

Maumivu chini ya kitovu yanakuja kutokana na athari kwenye viungo vya karibu. Viungo hivi ni pamoja na

  • utumbo mdogo
  • utumbo mkubwa
  • kizazi
  • mifuko ya mayai
  • kibofu cha mkojo
  • mirija ya kubeba mkojo kutoka kwenye figo mpaka kibofu na
  • Nyonga

Mara chache inaweza kutokea athari ikaanzia viungo vya mbali kabisa, lakini maumivu yakasafirishwa mpaka eneo la chini ya kitovu. Wakati ukipata hitilafu kwenye figo, figo zipo eneo la juu na maumivu yake yaweza kusambaa mpaka chini ya kitovu. Pia kama korodani zako zinauma maumivu yanaweza kusambaa mpaka chini ya kitovu

Aina za maumivu ya tumbo chini ya kitovu

Maumivu ya tumbo yanaweza kuwa ya muda mfupi ama ya mda mrefu. Maumivu ya mda mfupi yanaweza kusababishwa na jeraha au maambukizi kwenye kiungo husika. Magonjwa makubwa yanaweza kupelekea maumivu ya mda mrefu. Muone daktari mapema endapo maumivu yako yanaongezeka kila siku na hayaishi.

Je maumivu ya tumbo chini ya kitovu ni tatizo kubwa?

Kama tulivoona hapo juu, maumivu ni kiashiria kwamba kuna tatizo fulani la kiafya kwenye mwili. Ni ngumu kutambua chanzo kwa kufatilia maumivu pekee. Ni muhimu kumwona daktari akupime kugundua chanzo cha tatizo. Daktari atakupa dawa za kupunguza maumivu wakati huo atashugulika kujua chanzo.

Nini chanzo kikubwa cha maumivu ya tumbo chini ya kitovu?

Viungo kama utumbo mkubwa na mdogo vipo eneo la tumbo la chini, na vinachukua nafasi kubwa sana pale. Kwa sababu hiyo changamoto yoyote inayoathiri utumbo basi yaweza kuwa chanzo cha maumivu chini ya kitovu.

Changamoto hizi za kila siku ni pamoja na

  • gesi tumboni
  • chakula kutosagwa vizuri
  • kuharisha na
  • kukosa choo na choo kigumu

Kama chakula hakisagwi vizuri na tumbo kujaa, waweza kuwa na aleji na aina fulani ya chakula, ama tumbo lako haliwezi kusaga aina fulani cha chakula. Suluhisho ni kuacha kabisa kutumia aina ya chakula ambacho unaona mwili umekikataa.

Pia yawezekana utumbo umebimba kwa ndani. Magonjwa yanayopelekea utumbo kuvimba ni pamoja na

  • vudonda vya tumbo
  • maambukizi ya bakteria
  • Celiac disease (ambapo mwili unashambulia kiambata cha guleten ambacho hupatikana kwenye ngano)
  • Majeraha kwenye utumbo mdogo na mpana na
  • Saratani kwenye utumbo

Je nini chanzo cha maumivu ya tumbo kwa mwanamke?

Kama wewe ni mwanamke, viungo vya uzazi vipo eneo la chini ya kitovu. Viungo hivi ni chanzo kingine kikubwa cha maumivu ya tumbo chini ya kitovu. Japo maumivu ya tumbo la hedhi ni kawaida kwa kila mwanamke, sometime yanaweza kuashiria uwepo wa changamoto flani ya kiafya kama

  • PID
  • Vimbe kwenye kizazi (fibroids)
  • Kizazi kututumka (endometriosis)
  • Saratani ya kizazi
  • Vimbe kwenye mayai

Magonjwa ya Figo

Kama tatizo siyo kwenye mfumo wa chakula, basi yawezekana kuna shida kwenye njia ya mkojo ambako figo zinahusika. Ugonjwa mkubwa kwenye njia ya mkojo ni UTI yani maambukizi ya bakteria kwenye njia ya mkojo. UTI inaweza kuathiri kibofu cha mojo, mirija ya kusafirisha mkojo na hata figo pia. Na matatizo yote haya huzalisha maumivu kwenye kitovu.

Vipi kama maumivu ya tumbo yanatokea upande wa kushoto au kulia?

Maumivu ya tumbo upande wa kushoto chini ya kitovu yanaweza kutokana na athari kwenye utumbo mpana. Yawezekana kukawa na bakteria waliojificha eneo hilo na kupelekea kututumka mpaka kuleta maumivu.

Maumivu yakiwa eneo la chini kulia, yaweza kuwa ni appendix. Hiki ni kifuko kidogo ambacho huhifadhi mawe. Kifuko kinaweza kushambuliwa na bakteria ama kikajaa uchafu na hivo suluhishi ikawa ni kukiondoa kabisa.

Pia Maumivu kulia na kushoto kwa chini inaweza kutokana na athari kwenye mifuko ya mayai ama figo. Uvimbe kwenye yaia au mawez kwenye figo vyote hupelekea upate maumivu. Pia kama yai linatolewa kwenye kikonyo siku ya hatari, laweza kupelekea maumivu haya.

Je lini natakiwa kumwona daktari?

Muone daktari haraka sana kama

  • Maumimvu yamekuja haraka na ni makali sana
  • Maumivu yanazidi kuwa makali siku hadi siku
  • umeshindwa kwenda haja ndogo au kubwa kwa siku kadhaa
  • unapata dalili za unjano kwenye macho
  • unapata homa kali, kichefuchefu na kutapika
  • Tumbo lako ni gumu au laini sana ukishika
  • ulipata ajali hivi karibuni na maumivu yameendelea
  • una mimba