Categories
Afya ya mwanamke na uzazi Afya ya uke

Uchafu wa kunata ukeni

uchafu wa kunata ukeni

Uchafu ukeni upo wa aina nyingi sana, kuna uchafu mzuri na uchafu mwngine unaashiria kuna changamoto ya kiafya. Uhafu mwingi unaotoka unakuwa ukeni ili kukulinda dhidi ya maambukizi mengi. Topic ya leo tutajifunza zaidi kuhusu uchafu wa kunata ukeni na nini cha kufanya.

Ni kwaida kupata kiwango cha uchafu kiasi cha kujiko kimoja kila siku, na wingi wa uhafu utategemea upo siku ipi kwenye mzunguko wako.

Pamoja na kukulinda dhidi ya maambukii, uchafu wawea kuashiria endapo unaugua tatizo flani na kama inahitaji kwenda hospital haraka.

Je ni kawaida kutokwa uchafu wa kunata ukeni?

Uhafu wa ukeni unatofautiana mwonekano, wningi na uzito kulingana na mabadiliko ya homoni kwenye mzunguko wako. Uteute unaotoka ukiwa period siyo sawa na ule unaotoka siku za hatari.

Hebu tusome kwa undani nini kinatokea kwenye kila hatua/phase ya mzunguko.

Mzunguko wako unagawanyika katoka hatua/phase mbili; Tunaziita follicula phase na luteal phase. Katikati ya hivi vipindi viwili ndio kuna kipindi cha yai lililokomaa kutolewa yani ovulation.

Mabadiliko ya homoni na uchafu wa kunata ukeni

Vipindi hivi vyote vinaratibiwa na mabadiliko ya homoni ama vichocheo, homoni kama etrogen na progesterone. Estrogen inasaidia kujena ukuta na kuandaa kubeba mimba na pia inaathiri namna ya uchafu unaotoka.

Kama uchafu unatoka wa kunata basi kwa kiasi kikubwa yaweza isiwe tatizo. Lakini usiishie kwa kuangalia mwonekano tu wa uchafu, tazama na dalili zingine kama unahisi muwasho, haurufu mbaya, kutokwa damu na maumivu.

Kama uchafu unatoka ukeni ni wa kunata, ni mweupe na hauna rangi na hakuna haufu mbaya au dalili zingine mbaya mwilini. Basi hapo ujue uko salama kabisa

Je kwanini napata uchafu wa kunata ukeni

Uchafu wa kunata maa nwingi unaanza kutoka baada tu ya kumaliza hedhi na baada ya ovulation. Uchafu unavokuwa wa kunata zaidi ndvyo inakuwa ngumu kwa mbegu kuogelea na kurutubisha yai.

Uchafu huu wa kunata ni tofautia kabisa na uchafu uanovutika kama yai ambao unataoka kwenye ovulation. Uteute huu unakuwa laini na kuvutika ili kufanya mbegu kuogelea vizuri kwenda kurutubisha yai.

Vipi kuhusu uteute unaotoka ukiwa na hisia za mapenzi

Mwanamke ukiamshwa na hisia za mapenzi zikapanda, utahisi unyevunyevu ukeni na ute wa kuteleza. Huu ni ute alama ili usipate maumivu kwenye tendo wakati wa msuguano. Ute huu unaweza kunata kadiri unavoendelea na tendo.

Uteute karibia na siku ya hedhi

Unapokarbia kuanza hedhi utaanza kuona uteute wa jkunata ukeni, sawa na unapomalizia hedhi. Kipini hiki waweza kupata uchafu wa pink, brown au mwekundu ambao ni kawaida kabisa.

Uchafu unaoashiria maambukizi

Japo uchafu wa kunata ukeni siyo ishu kubwa sana, ni muhimu kutazama pia dalili zingine ili uone kama hauna maambukizi. Tazama kama uchafu unaambatana na dalili zingine kama

  • maumivu ukeni na muwasho
  • uchafu wa kijani
  • uchafu mwingi sana katoka siku
  • Uchafu wa kama maziwa mtindi au usaha
  • maumivu wakati wa kukojoa au kwenye tendo
  • maumivu chini ya kitovu
  • harufu mbaya ukeni kama shombo la samaki

Lini unatakiwa kumwona daktari?

Mwone daktari mapema ukiona daklili mbaya hapo juu. Utapata vipimo na kuanza toba mapema, maana magonjwa kama ya zinaa siyo ya kuhelewa kupata tiba.

Hitimisho kuhusu uchafu wa kunata ukeni

Mhanganyiko wa uhafu ukeni, bakteria wazuri na uteute unasaidia kulinda uke wako na kufanya uwe mlaini

Uchafu mzuri ukeni unatofautiana kwa wingi na uzito kulingana na upo siku ya ngapi kwenye mzunguko wako

Hisia za mapenzi, Ujauzito , hedhi na pia maambukizi vyote hivi vinaathiri mwonekano na wingi wa ucchafu unaotoka

Kama una hofu juu ya uhafu wako unaooka ukeni, basi tizama kama una unatoa harufu, ni mwingi kupita kiasi, upo kama maziwa mtindi, wa kijani na una dalili zingine za muwasho na malengelenge. Hapo unatakiwa kumwona daktari mapema.

Kwa ushauri na Tiba asili tuandikie kwa namba 0678626254

Categories
Siku za hatari

Je kubana miguu baada ya tendo kunasaidia kushika mimba mapema?

kubana miguu baada ya tendo

Kwa mwanamke unapojaribu kushika mimba,unakuwa na shauku ya kujaribu mbinu mbalimbali ili jambo lako ilitimie mapema. Wengi wanasema kubana miguu baada ya tendo yaweza kusaidia, hili tutaona kwenye makala ya leo kama ni kweli ama siyo.

Wanawake wanaamini kwamba kubana miguu baada ya kutiwa mbegu ni mbinu ya kuanya ashike mimba mapema. Baada ya tendo mwanamke ananyoosha miguu juu na kuibana huku akiegemeza kwenye kitanda au ukuta kwa dakika kadhaa.

Kubana miguu baada ya tendo na nguvu ya uvutano(gavity)

Dhana hii inabebwa na imani kwamba nguvu ya uvutano ya dunia yani gravity inarahisisha mbeu kuogelea na kwenda kurutibisha yai mapema.

Ni ahisi sana kuamini jambo hili, lakini tumewauliza wataalamu wa afya na kupitia tafiti mmbalimbali, na hapa chini tutasoma ukweli kuhusu dhana hii tuone uhalisia wake.

Je urutubishaji unaanyikaje? na Je kubana miguu baada ya tendo kunasaidia?

Kabla ya kujua kama kubana miguu baada ya tendo inasaidia kuhika mimba, tuone kwanza urutubishaji unatokeaje.
Kuna njia mbili ambapo urutubishaji unaweza kufanyika, moja ni kwa kuingiliana mwanamke na mwanaume bila kina na mbili ni kwa mwanamke kupandikizwa mbegu hospitali kwa kutumia vifaa maalumu.

Kupandikizwa yani atifirtial insemination kunafanykika na mtaalamu wa afya aliyebobea. Mbegu za mwanaume zinakusanywa kwa uangaliffu na kutunzwa, kisha mwanamke ataandaliwa na kupandikiziwa mbegu kwenye siku zake za hatari

Kubana miguu baada ya tendo ni imani tu isiyo na ukweli

Kama wataalamu wanavosema hakuna ukweli wowote kwamba eti kubana miguu inasaidia mbeu kuogelea, pia hata kulala chali kwa mda siyo suluhisho la mbegu kufika kwenye yai. Kuna baadhi ya mambo mengine unaweza kuanya kuongeza hansi yako ya kushika mimba ikiwemo kuanya tendo kwenye siku za hatari.

Utajuaje siku za hatari?

Njia zifuatazo zitakusaidia kujua siku ya ovulation/siku za hatari

1.Kwa miezi 8 mpaka 12 rekodi siku ambayo unaanza hedhi na uhesabu siku zote za kila mzunguko. Siku ya kwanza ni ile unayoanza hedhi katika mwezi husika na hesabu mpaka siku unayoanza hedhi katika mwezi mwingine hapo mzunguko mmoja utakuwa umekamilika.

2.Rekodi mzunguko mfupi na mzunguko mrefu zaidi katika ufuatiliaji wako

3.Kupata siku yako ya kwanza ya hatari chukua namba ya mzunguko mfupi zaidi toa 18, mfano mzunguko wako mfupi ni siku 27-18 inabaki 9.

4.Kupata siku yako ya mwisho ya hatari kwenye mzunguko, chukua siku za mznguko wakko mrefu toa 11. Mfano mzunguko wako mrefu ilikuwa siku 30-11 inabaki 19.
5.Katika mahesabu hapo juu ni kwamba siku kati ya mzunguko mfupi na mrefu ndizo siku zako za hatari, kwa maaana ya kuanzia siku ya 9 na 19 ndizo siku zako za hatari. Kama unataka usishike mimba basi usifanye ngono siku ya 9 ya hedhi mpaka siku ya 19.

Kubana miguu baada ya tendo kunasaidia kushika mimba haraka? Lini unatakiwa kumwona daktari?

Kitu cha muhimu sana unatafuta mimba ni kutazama ushauri wa daktari na vipimo endapo unatafuta mimba kwa zaidi ya miezi 12 bila mafanikio.
Kama unajaribu mimba a una historia ya changamoto kama hedhi kuvurugika, magonjwa ya zinaa, kutoa mimba nyingi, kuugua vimbe kama fibroids nk unatakiwa kumwona specialist wa wanawake mapema.

Mwanaume pia inahitajika apime mbegu (semen analysis) maana yawezekana shida ikawa ipo kwake na siyo kwa mwanamke.

Kwa ushauri na tiba asili tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Tendo la ndoa

Kwanini Uende Haja Ndogo Baada ya Tendo

haja ndogo baada ya tendo

Kwanini unatakiwa kwenda haja ndogo baada ya tendo?

Kwenye makala hii fupi tutaeleza kwanini unatakiwa kupata mkojo baada ya tendo. Na uhusiano wake na magonjwa kama UTI.

Je nini faida za kwenda haja ndogo baada ya tendo?

Ni muhimu sana mwanamke kjwenda haja ndogo baada ya tendo. Hizi ni sababu kwanini ufanye hivo

1.Kuepuka UTI

UTI ni maambukizi kwenye viungo vya njia ya mkojo kama kibofu, mirija ya mkojo na figo. Maambukizi haya yanatokea pale bakteria wanapokua kupita kiasi kwenye njia ya mkojo na kuwa wengi kwenye kibofu. Kama kinga yako ya kwenye njia ya mkojo ikifeli , bakteria hawa hukua na kuleta maambukizi.

Je kwanini wanawake wanapata zaidi UTI?

UTI inawapata zaidi wanawake kutokana na sababu hizi

Maumbile ya mwanamke: Mrija wa mkojo kutoka kwenye kibofu mpaka kwenye uke ni mfupi zaidi kwa mwanamke na hivo kufanya njia ya bakteria kusafiri mpaka kwenye kibofu kuwa haraka zaidi.

Uzazi wa mpango wa kisasa: Wanawake wanaotumia zaidi kitanzi kupanga uzazi wanaweza kupata maambukizi kirahisi

Ngono: hatari ya kuugua UTI ni kubwa zaidi kwa mwanamke anayefanya tendo kuliko yule aliepumzika kufanya tendo

Kukoma hedhi(menopause): Kupungua kwa uzalishaji wa homoni ya estrogen, inapelekea kupungua uteute ukeni na hivo uke kuwa kwenye hatari zaidi ya kupata maambukizi.

Sababu zingine zinazopelekea mtu augue UTI kirahisi ni pamoja na

Maumbile yasiyo ya kawaida kwenye njia ya mkojo: watoto waliozaliwa na hitilafu kwenye mfumo wa mkojo wanaweza kupata maambukizi kirahisi

Kuziba kwa njia ya mkojo: changamoto kama mawea ya figo yanaweza kuepelekea kuziba njiani na hivo kufanya mkojo kubakizwa, mkojo unapobakizwa mda mrefu inasababisha maambukizi.

Matumizi ya kifaa cha kusaidia kutoa mkojo yani catheter hasa kwa wagonjwa wa tezi dume na waliopata kiharusi

Dalili za UTI

Dalili kuu za UTI ni pamoja na

  • kukojoa mara kwa mara na kutoa mkojo kidogo
  • maumivu chini ya kitovu
  • mkojo wa njano wenye harufu
  • kuhisi uchovu sana
  • kuungua na maumivu wakati wa kukojoa
  • kupata hamu ya kwenda kokojoa mara kwa mara

Mrija wa mkojo kwa mwanamake

Mirija huu huitwa urethra, unasaidia kutoa mkojo kutoka kwenye kibofu kwenye njie ya uke. Kwa mwanamke mrija huuni mfupi(sm 2.5 mpaka 4) na kwa mwanaume ni (sm 15 mpaka 20). Hii inawafanya wanawake kuwa kwenye hatari zaidi ya kuugua UTI kuliko wanaume, kwasababu ili maambukizi yatokee ni lazima bakteria wapande mpaka kwenye kibofu. kama njia ni fupi maana yake ni rahisi zaidi kwa bakteria kufika kwenye kibofu na kwenda mpaka kwenye figo.

Kibofu cha mkojo

Kibofu cha mkojo n mfumo ulipo katikati ya mifupa na misuli ya nyonga, na kazi yake ikiwa ni kuhifadhi mkojo kutoka kwenye figo. Kibofu kinapojaa mkojo na kutanuka sana, kinatuma taarifa kwenye ubongo ili ukakojoe.

Wakati wa tendo la ndoa, bakteria wanaweza kuingia kwenye mrija wa mkojo na kupngeza chansi yako ya kuugua UTI. Ndiomaana ni muhimu sana baada ya tendo uende kukojoa ili kuflash vimelea kabla hawajaleta madhara.

Pia kufanya tendo wakati kibofu cha mkojo kimejaa kinapelekea kulegea kwa misuli ya kushikilia mkojo. Yani inafikia wakati unashindwa kuzuia mkojo kiasi kwamba ukocheka, ukipiga chanfya au hata kwenye tendo mkojo unakuponyoka.

Hakikisha unakojoa kabla na baada ya tendo siku zote.

Kwa ushauri na Tiba asili Tuandikie whatsapp namba 0678626254.

Categories
Uncategorized

Dalili za yai Kupevuka

yai kupevuka

Ikiwa unatafuta kushika mimba, kukwepa kushika mimba isiyotarajiwa au pengine unataka tu kuelewa mwenendo wa mwili wako, kuelewa mzunguko wako ni jambo la muhimu sana. Yai kupevuka kitaalamu tunaita ovulation. Ni kipindi kifupi sana lakini chenye matokeo makubwa kwa mwili wako.

Nini maana ya yai kupevuka?

Kwanza muhimu kujua ovulation ni nini? Ovulation ni kipindi katika mzunguko wa hedhi wa mwanamke ambapo yai lililokomaa linatolewa kwenye mfumo wa mayai(ovari), kwa ajili ya kufanyiwa urutubishaji na mimba ifanyike. Yai likishatolewa kwenye ovari, linaenda mpaka kwenye mrija wa uzazi, hapo yai linaweza kuishi mpaka saa 48. Endapo hakuna mbegu imerutubisha yai basi litavunjika na kutolewa nje.

Je ni Lini yai linapevuka kwenye mzunguko wa hedhi?

Hili ni swali zuri sana ambalo kila mwanamke huwa anajiuliza. yai linatolewa hasa baada ya siku 14 hedhi ilipoanza, kwa mzunguko wa siku 28.

Lakini muhimu ujue kwamba siyo kila mwanamke basi siku yake ya hatari ni ya 14. Wengine wana mzunguko mfupi zaidi mpaka siku 21 na wengine mizunguko mirefu mpaka siku 35. Endapo hujui mzunguko wako basi bofya makala hii (Jinsi ya kufatilia siku za hatari kwa mizunguko yote) usome kwanza kisha urudi kumalizia makala ya sasa.

Je ovulation inaisha baada ya masaa mangapi?

Mchakato mzima wa yai kutolewa inachukua masaa 36. Kitendo chenyewe cha yai kutoka kwenye ovari ni cha haraka, ispokuwa mabadiliko ya homoni kuelekea zoezi husika yanaanza mapema zaidi.

Ni zipi dalili za yai kupevuka?

Habari njema ni kwamba mwili wa mwanamke unatoa viashiria vingi kuonesha kwamba hizi ni siku za hatari na yai limevevuka tayari kwa kurutubishwa. Siyo kila mtu atapata dalili hizi zote, lakini lazima kuna dalili kadhaa utaziona endapo utausikiliza mwili vizuri. Kwahivo usijione mnyonge na kuhisi yai halijapevuka endapo utapata dalili chache katika hizi nitakazokuelezea leo.

1.Uteute wa kuvutika

Lazima utakuwa umewahi kusikia kuhusu ute wa uzazi ama ute wa ovulation, ama kuona uchafu mwembemba unaovutika kwenye chupi. Huu ndio ute unaoashiria kwamba yai limepevuka na litatolewa ndani ya masaa 24 tangu ute umeanza kutoka. Uteute huu unakuwa mwepesi kama yai, unavutika na hauna harufu.

2.Tumbo kujaa kipindi ya yai kupevuka

Yawezekana umewahi kuhisi tumbo kujaa katika siku flani katikati ya mzunguko wa hedhi na usijue kwanini. Mabadiliko ya homoni hasa kuongezeka kwa homoni la LH inaweza kufanya tumbo kubakiza maji na hivo kuvimba kiasi. Lakini usiogope sana hali hii ni ya masaa machache na utakuwa sawa.

3.Kichefuchefu kwenye siku za yai kupevuka

Unaweza kupata hali ya kuhisi kichefuchefu ukiwa kwenye siku ya ovulation, hii pia ni kutokana tu na mabadiliko ya homoni. Endapo utapata na hali hii, jaribu kutembea nje upate hewa safi na utafune tangawizi.

4.Mabadiliko ya joto la mwili kipindi cha cha yai kupevuka

Kwenye siku za hatari, hasa siku yenyewe yai linapotolewa, joto la mwili huongezeka kidogo kwa centigrade 0.3. Unaweza kununua kipimajoto pharmacy ukajipima mwenyewe nyumbani na kuona mbadiliko haya.

5.Maumivu ya tumbo upande mmoja, kutokwa na matone ya damu

Je wafahamu kwamba unaweza kupata maumivu kipindi cha yai kutolewa? Maumivu haya yanatokana na kitendo cha yai kutoka kwenye kikonyo chake ambacho ni mfumo wa mayai(ovari). Kitendo hiki pia chaweza kupelekea damu itoke kwenywe kovu na hivo ukaona matone kidogo kwenye chupi. Kuanzia sasa endapo utaona damu kidogo katikati ya mzunguko basi usiogope, jua tu kwamba ni yai linatolewa.

Ni muda gani sahihi kufanya tendo endapo unatafuta mimba kwa mda mrefu bila mafanikio?

Pengine sasa unajiuliza wewe na mwenzi wako mkutane lini ili kuongeza chansi ya kupata mimba haraka? Siku nzuri na yenye chansi kubwa kupata mimba ni siku ambapo yai limetolewa na masaa 24 yanayofuatia. Na pia siku 5 kabla ya yai kutolewa.

Kwanini siku 5 kabla? kwasababu mbegu zinaweza kuishi mpaka siku 5 kwenye kizazi baada ya kufanya tendo. Kwahivo kumbe mbegu zaweza kulisubiri yai litolewe hukohuko ndani.

Kwa ushauri na Tiba tuandikie kwa whatsapp namba 0678626254

Categories
Afya ya mwanamke na uzazi

Namna ya Kuhesabu umri wa mimba na Siku ya kujifungua

umri wa mimba

Nawezaje kujua umri wa mimba? Mpaka sasa umeshapima kwa UPT na umejua una mimba. Bilashaka una furaha sana maana sasa unakaribia kuitwa mama. Lakini pengine una kiu ya kujua mimba yako iliingia lini au ina umri gani. Pengine una wapenzi wawili na wote umekutana nao katika muda usiozidi wiki moja, sasa unawaza mimba hii ya nani?.

Lengo la makala hii ni kukwelekeza jinsi gani unaweza kuhesabu na ukajua umri wa mimba,bila hata kwenda hospitali.

Namna ya kuhesabu umri wa mimba

Kwanza muhimu ujue tafsiri ya hivi vifupi kwa maana vitatumika sana.
LMP yaani last menstural period, ikimaanisha siku ya kwanza kuanza hedhi yako ya mwisho kabla hujashika mimba na EDD-Estimated delivery date, yaani makadirio ya siku yako ya kujifungua.

Watoa huduma yani manesi na madaktari huwa wanapima umri wa mimba kwa kucheki kwanza lini ulipata hedhi yako ya mwisho. Kama mzunguko wako ni ule wa kawaida yani siku 28 maana yake siku ya hatari ni ya 14, kwahivo hapo mimba ilitungwa week mbili baada ya LMP. Sasa kwenye kuhesabu umri wa mimba hizi week mbili huwa zinaongezwa.

Kumbuka kwamba haya ni makadirio na siyo umri sahihi wa mimba. Kupima siku ya kujifungua, ongeza siku 280 ambazo ni wiki 40 kwenye siku yako ya kwanza kuanza hedhi ya mwisho, endapo una mzunguko wa siku 28.

Nitajuaje ni lini siku nilishika mimba?

Kitaalamu tunaita conception date- ni siku ambapo mimba ilitungwa. Kwasababu mbegu zinaweza kukaa kwenye kizazi mpaka siku 6, urutubishaji unaweza kutokea siku yoyote katika hizo siku 6 baada ya tendo. Mimba kutungwa kunategemea na yai limepevuka na kutolewa lini. Kama yai lipo tayari limeshatolewa na mbegu zimeingia, basi ndani ya masaa 24 mimba inatungwa.

Siku ya kujifungua

Mwanzoni utakuwa na hamu ya kujua umri wa mimba, ila kadiri miezi inavosogea sasa utakuwa na kiu ya kujua lini utajifungua? Muhimu fahamu tu kwamba unaweza kupata uchungu kabla a baada ya siku ya makadirio. Pengine daktari amekufatilia na ameona unahitaji kufanyiwa upasuaji, au kuchomwa sindano ya uchungu mapema. Vyote hivi vinachangia mabadaliko ya siku ya makadirio.

Kipimo cha utrasound kugundua umri wa mimba

Utrasound ni kipimo kinachotumia mawimbi ya sauti kupata picha za ndani ya mwili. Kujua ukubwa wa mimba na hata jinsia, watoa huduma wanaweza kutumia kipimo hiki cha utrasound. Pia utrasound inaweza kugundua kama mtoto ana changamoto za kiafya kama kushindwa kukua vizuri.

Vipi kama nilipandikiza kwa IVF, najuaje umri wa mimba?

Kwanza muhimu kujua IVF ni nini. IVF ni kifupi cha invitro fertilization, ni njia ya kupandikiza mimba ambapo mbegu na yai zinarutubishwa nje ya mwili, kisha kiume kinapandikizwa kwenye kizazi ili kikue.

Kwavile mimba hujapata kiasili, hata naman ya kufanya madadirio ya umri wa mtoto ni tofauti.

  • Kama yai fresh limetumika, utajumlisha siku 266 kutoka kwenye siku yai limetolewa kwenye kizazi chako kwa ajili ya urutubishaji
  • kama yai lilitunzwa kwa siku 3 basi jumlisha siku 263 kutoka kwenye siku ya upandikizaji
  • Kama mayai yalitunzwa kwa siku 5, basi utajumlisha siku 261 kwenye siku ya upandikizaji.

Namna ya kuhesabu siku ya kujifungua

Kujua siku ya makadirio yaako, muhudumu anaangalia siku ya mwisho kuanza hedhi na pia utrasound yako ya kwanza. Kisha watajumlisha siku 280 yani wiki 40 kwenye LMP. Baada ya hapo wnalinganisha na makadirio kwenye utrasound na kutoa siku ya kujifungua.